SERIKALI YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR

Size: px
Start display at page:

Download "SERIKALI YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR"

Transcription

1 SERIKALI YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR Mhe. Dkt. Ali Mohamed Shein Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi TAARIFA YA SERIKALI YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR YA UTEKELEZAJI WA ILANI YA UCHAGUZI YA CCM KWA KIPINDI CHA MIAKA MITANO (NOVEMBA, 2010 HADI JULAI, ) Imetayarishwa na Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais, Zanzibar 1

2 JULAI, 2

3 YALIYOMO SEHEMU YA KWANZA 1.0 UTANGULIZI... 1 SEHEMU YA PILI 2.0 HALI YA SIASA Matukio Makubwa ya Kisiasa Yaliyotokea Kufanyika kwa chaguzi ndogo kwa nafasi za Ubunge, Uwakilishi na Udiwani Maadhimisho ya Miaka 50 ya Mapinduzi ya Zanzibar Matukio ya Uvunjifu wa Amani Masuala ya Muungano Vikao vya Pamoja vya Mashirikiano Mchakato wa Kuandaa Katiba Mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania... 8 SEHEMU YA TATU 3.0 SEKTA YA KIUCHUMI Ukuaji wa Uchumi Mfumko wa Bei Mapato na Matumizi ya Serikali Kushuka kwa Kiwango cha Nakisi ya Bajeti Kuimarisha Maeneo Huru ya Kiuchumi ya Fumba Uwakilishi wa Sekta Binafsi katika Vikao Mbalimbali Kuandaa Mazingira Bora ya Kiuchumi ili Kuvishawishi Vyombo vya Fedha Kutoa Mikopo Yenye Masharti Nafuu Kuanzisha Maeneo Mapya ya Kiuchumi Miradi Iliyowekezwa kwa Kipindi cha SEHEMU YA NNE 4.0 SEKTA ZA UZALISHAJI MALI KILIMO Kutekeleza Mkakati wa Uimarishaji wa Zao la Karafuu Kuimarisha Miundombinu ya Umwagiliaji Maji i

4 4.1.3 Kuendeleza Programu za Tafiti za Kilimo na Maliasili kwa Kuwashirikisha Wakulima na Washiriki Wengine Utafiti wa Mazao ya Nafaka na Jamii ya Kunde Jaribio la Mbolea Mpya na Mafunzo kwa Wakulima Chini ya Mradi wa NAFAKA Ruzuku katika Kilimo Tafiti za Mazao ya Mizizi (Muhogo na Viazi Vitamu) Uboreshaji wa Miundombinu ya Utafiti Kuhimiza na Kushajiisha Matumizi ya Pembejeo na Mbinu Bora za Kilimo Kuendelea Kuhimiza na Kutilia Mkazo Mafunzo na Matumizi ya Kanuni za Kilimo Bora kwa Mazao ya Chakula, Biashara na Matunda Uimarishaji wa Chuo cha Kilimo Kizimbani Kutekeleza Mkakati wa Kuanzisha Akiba ya Chakula ya Zanzibar (National Food Reserve) Kuendeleza Kazi za Tafiti kwa Wanyama UVUVI NA MAZAO YA BAHARINI Uimarishaji wa Zao la Mwani MALIASILI Kutekeleza Mpango wa Muda Mrefu wa Usimamizi wa Rasilimali za Misitu na Maliasili Zisizorejesheka MAZINGIRA Kusimamia Utekelezaji wa Mpango wa Hifadhi ya Mazingira katika Maeneo ya Ardhi, Bahari na Ukanda wa Pwani Kufanya Mapitio ya Miradi Inayohusiana na Mazingira UTALII Kusimamia utekelezaji wa Sera, Sheria na Mpango Mkuu wa Utalii Kuitangaza Zanzibar Kiutalii Nje ya Nchi ili Kuongeza Kipato Kuimarisha Utalii wa Kumbukumbu za Kihistoria Kuibua Maeneo Mapya ya Vivutio vya Utalii Kumbukumbu na Mambo ya Kale Kuhifadhi Kumbukumbu za Kihistoria na Mambo ya Kale Kuendeleza Matengenezo ya Makumbusho Kufanya Uhakiki wa Hoteli za Kitalii Kuimarisha Huduma za Utalii kwa Kuziendeleza Jumuiya za Watoa Huduma Kupunguza Vituo vya Ukaguzi Katika Maeneo Wanayopita Watalii ii

5 4.6.9 Kukiimarisha Chuo cha Maendeleo ya Utalii VIWANDA NA BIASHARA Kuimarisha Mtandao wa Usambazaji Habari za Biashara kwa Wafanyabiashara Kufanya Utafiti wa Usarifu wa Zao la Karafuu VYAMA VYA USHIRIKA Kusimamia Utekelezaji wa Sheria ya Vyama vya Ushirika na Program Mbalimbali Kuendelea Kusajili na Kufanya Ukaguzi wa Vyama Vipya vya Ushirika SEHEMU YA TANO 5.0 MIUNDOMBINU YA KIUCHUMI BARABARA Kusimamia Utekelezaji wa Sheria Zinazohusiana na Usalama Barabarani USAFIRI WA BAHARINI Ujenzi wa Bandari ya Mpigaduri Kuliimarisha Shirika la Meli Ununuzi wa Meli Mpya ya Serikali Kubadili Mfumo wa Uendeshaji wa Ofisi ya Mrajis wa Meli na kuwa Mamlaka ya Usimamizi wa Usafiri wa Baharini Kuendeleza Mazingira ya Kuvutia Wawekezaji wa Nje na Ndani ili Kuekeza zaidi katika Usafiri wa Baharini USAFIRI WA ANGA Kuwajengea Uwezo Wafanyakazi Kusimamia Utekelezaji wa Mpango Mkuu wa Uendeshaji wa Kiwanja cha Kimataifa cha Zanzibar Uendelezaji Ujenzi wa Uzio na Jengo Jipya la Abiria Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume Ujenzi wa Maegesho na Njia ya Kupitia Ndege Uwanja wa Ndege wa Kimataifa Kukamilisha Kazi za Ujenzi wa Kiwanja cha Ndege Pemba UMEME Kuimarisha Mazingira ya Kuvutia Wawekezaji katika Sekta ya Nishati ya Umeme Kuwapatia Mafunzo Wafanyakazi katika Fani za Nishati na Madini Kuliimarisha Shirika la Umeme Zanzibar (ZECO) Kusimamia Uendeshaji wa Nishati ya Mafuta na Gesi ARDHI iii

6 5.6.1 Usajili za Ardhi kwenye Maeneo ya Fukwe na Miji Maeneo ya Fukwe Maeneo ya Miji SEHEMU YA SITA 6.0 HUDUMA ZA JAMII Elimu Elimu ya Maandalizi Utayarishaji wa Vifaa vya Kufundishia na Kujifunzia vya Elimu ya Maandalizi Kuongeza Idadi ya Madarasa ya Elimu ya Maandalizi Kukamilisha Sera ya Makuzi na Malezi ya Mtoto Kuimarisha mazingira ya Skuli za Msingi Kuimarisha Ufundishaji katika Madarasa ya Awali ya Msingi (Std 1-4) Kuondoshwa kwa Michango ya Wazee katika ngazi ya Elimu ya Msingi Elimu ya Sekondari Kuimarisha Elimu ya Sayansi na Hesabati kwa Kuendeleza Kambi za Sayansi Kutoa Mafunzo kwa Walimu Wakuu na Maafisa wa Elimu wa Wilaya na Mikoa Elimu Mbadala na Elimu ya Watu Wazima Huduma za Maktaba Kuendeleza Mafunzo ya Ukutubi Kuhamasisha Wananchi Kutumia Maktaba Elimu ya Juu Kuimarisha Mafunzo ya Ualimu Mafunzo ya Ualimu Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Amali Kuimarisha Taasisi ya Karume ya Sayansi na Teknolojia Kuimarisha Skuli ya Ufundi Kengeja Sekta ya Afya Huduma za Kinga Huduma za Tiba Huduma Bora za Afya kwa Wananchi Wote Kuendeleza Huduma za Tiba Asili Baraza la Tiba Asili iv

7 6.2.5 Kuimarisha Chuo cha Taaluma za Sayansi ya Afya Kuendeleza Mapambano dhidi ya Malaria, UKIMWI, Kifua Kikuu na Ukoma Malaria Usambazaji wa Vyandarua katika Vituo vya Afya UKIMWI Kifua Kikuu na Ukoma Kuipandisha Daraja Hospitali ya Wete Kuipandisha Daraja Hospitali ya Abdalla Mzee Pemba Kuipandisha Daraja Hospitali ya Micheweni Kuipandisha Daraja Hospitali ya Kivunge Kuimarisha Hospitali ya Makunduchi Kuendelea Kuimarisha Huduma za Hospitali ya Mnazi Mmoja ili kufikia Hadhi ya Hospitali ya Rufaa MAJI Kuzifanyia Mapitio Sera na Sheria ya Maji MAKAAZI Kukamilisha Ujenzi wa Nyumba ya Maendeleo Bambi Uendelezaji wa Mamlaka ya Mji Mkongwe SEHEMU YA SABA 7.0 MAENEO MENGINE YA KIPAUMBELE Utamaduni na Michezo Kuandaa Sera ya Utamaduni na Michezo Kusimamia Utekelezaji wa Sera na Sheria za Michezo na Utamaduni Kujenga Kiwanja cha Kisasa cha Michezo ya Ndani Kukamilisha Ujenzi wa Kituo cha Michezo Dole Ujenzi wa Uwanja Mpya wa Michezo Matengenezo ya Kuboresha Uwanja wa Gombani Pemba Kuendeleza na Kuimarisha Vipaji vya Wanamichezo Kuendeleza Kudumisha Mila, Silka na Maadili Mema ya Wazanzibari VYOMBO VYA HABARI Kusimamia Utekelezaji wa Sera ya Habari na Kuendeleza Uhuru wa Vyombo vya Habari Kusimamia Utekelezaji wa Muongozo, Kanuni na Sheria ya Vyombo vya Habari v

8 7.2.3 Kuendeleza Mafunzo kwa Watendaji wa Vyombo vya Habari na Utangazaji Kuviimarisha Vyombo vya Habari ikiwemo ZBC TV na ZBC Redio Ujenzi wa Studio ya Wasanii Kuendelea Kukiimarisha Chuo cha Uandishi wa Habari Kusimamia na Kudhibiti Uingizaji wa Vifaa vya Utangazaji Mradi wa E-Government MAJANGA NA HUDUMA ZA UOKOZI Kuanzisha na Kuimarisha Kamati za Maafa kwa Ngazi ya Taifa, Wilaya na Shehia Kuimarisha Vikosi vya Uokozi Wakati wa Maafa Kuimarisha Kikosi cha Zimamoto na Uokozi DAWA ZA KULEVYA Kusimamia Utekelezaji wa Sheria ya Udhibiti wa Dawa za Kulevya Kushirikiana na Asasi za Kijamii Kuanzisha Vituo Maalumu vya Kurekebisha Vijana Walioathirika na Dawa za Kulevya Taaluma na Ushauri Nasaha kwa Wananchi DEMOKRASIA NA UTAWALA BORA Kuzingatia Misingi ya Demokrasia na Utawala Bora Kusimamia Utekelezaji wa Kazi na Majukumu ya Serikali Kuendeleza Kazi ya Utekelezaji wa Mkakati wa Elimu ya Uraia, Kidemokrasia, Haki za Binaadamu na Utawala Bora Kuimarisha Ofisi ya Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali Kuanzisha Mahakama ya Biashara Zanzibar OFISI YA MKURUGENZI WA MASHTAKA Kuimarisha Kiwanda cha Upigaji Chapa na Mpiga Chapa Mkuu wa Serikali SERIKALI ZA MITAA Kusimamia Suala la Usafi Kuhamasisha Wananchi Kuunda Kamati za Maendeleo Kuvijengea Uwezo Vikosi Maalum vya SMZ Kikosi Maalum cha Kuzuia Magendo (KMKM) Jeshi la Kujenga Uchumi (JKU) Kikosi Cha Valantia Zanzibar Kikosi Cha Mafunzo Mfuko wa Hifadhi ya Jamii vi

9 SEHEMU YA NANE 8.0 KUYAENDELEZA MAKUNDI MBALIMBALI WATOTO VIJANA Kukamilisha Uanzishaji wa Baraza la Taifa la Vijana WANAWAKE WAZEE WATU WENYE ULEMAVU Kubaini Watu Wenye Ulemavu Wanaoweza Kufanyakazi za Uzalishaji Mali WAFANYAKAZI Kuandaa Sera ya Hifadhi ya Jamii na Kufanya Mapitio ya Sheria za Kazi Kusimamia Utekelezaji wa Sera ya Ajira Kuimarisha Mashirikiano kati ya Serikali, Shirikisho la Vyama Huru vya Wafanyakazi na Waajiri Kuendelea Kuimarisha Mazingira bora na Maslahi ya Wafanyakazi SEHEMU YA TISA 9.0 MAENEO MENGINEYO MUHIMU SEKTA YA SHERIA Kuwaendeleza Wataalamu wa Sheria za Mikataba Kuyatafutia Ufumbuzi Masuala ya Mrundikano wa Kesi Mahakamani Kuwapatia Mafunzo Mahakimu wa Mahakama ya Mwanzo Kukamilisha Mchakato wa Kutenganisha Shughuli za Upelelezi na Uendeshaji Mashtaka Msaada wa Kisheria Kupeleka Huduma za Mahakama Karibu na Wananchi Mapambano Dhidi ya Rushwa na Uhujumu wa Uchumi SEHEMU YA KUMI 10. Changamoto Zilizojitokeza na Hatua za Kukabiliana Nazo SEHEMU YA KUMI NA MOJA 11. HITIMISHO vii

10 ORODHA YA JADWELI Jadweli namba1: Takwimu za Ukuwaji Uchumi Zanzibar 10 Jadweli namba 2: Maeneo yaliyopimwa viwanja Zanzibar...66 Jadweli namba 3: Idadi ya Nyumba za walimu zilizojengwa Unguja na Pemba..73 Jadweli namba 4: Takwimu za usajili wanachama waajiri Jadweli namba 5: Takwimu za usajili wanachama waajiriwa Jadweli namba 6: Idadi ya Vijana waliosajiliwa kuomba kazi katika kituo cha kutoa taarifa za ajira Jadweli namba 7: Idadi ya Vijana walioajiriwa kwa kuunganishwa na waajiri kupitia Kituo cha kutoa taarifa za ajira Jadweli namba 8: Taasisi zilizofanyiwa Ukaguzi kazi Jadweli namba 9: Ukaguzi wa Usalama na Afya Kazini viii

11 UFAFANUZI WA VIFUPISHO AGOA - African Growth and Opportunity Act AMR - Automated Meter Reading AMREF - African Medical and Research Foundation ARV - Anti Retroval Viruses BADEA - Arab Bank for Economic Development in Africa CATC DSM - Civil Aviation Training Center Dar-es-Salaam CCM - Chama Cha Mapinduzi CFP - Community Forests Pemba CHAVIZA - Chama Cha Viziwi Zanzibar CHEC - China Habour Engeneering Company CPI - Consumer Price Index CUZA - Cooperative Union of Zanzibar DAMA - Department of Archives, Museum and Antiquities EAC - East African Community ECG - EchoCardioGraphy EIA - Environmental Impact Assessment EU - European Union FEASSA - Federation of East Africa Secondary School Associations GDP - Gross Domestic Product HIMA - Hifadhi Misitu ya Asili HIPZ - Health Improvement Project Zanzibar ICAP - International Center for AIDS Care and Treament Programs IFAD - International Fund for Agricultural Development IMF - International Monetary Fund IMO - International Maritime Organization IMS - Institute of Marine Science IRRI - Internationa Rice Reseach Institute JICA - Japan Internation Cooperation Agency JMZ - Jumuiya ya Maalbino Zanzibar ix

12 JUWAUZA - Jumuiya ya Wanawake Wenye Ulemavu Zanzibar KMKM - Kikosi Maalum cha Kuzuia Magendo KUC - Kenya Utalii College MACEMP - Marine and Coastal Environment Management Project MIMCA - Mnemba Island Marine Conservation Area MKUZA II - Mkakati wa Kukuza Uchumi na Kupunguza Umasikini Zanzibar MCC - Millenium Challenge Cooperation MCU - Marine Conservation Unit NACTE - National Council for Technical Education NEC - National Electoral Commission NGOs - Non Governmental Organizations NORAD - Norwegian Agency for Development Co-operation PECCA - Pemba Channel Conservation Area PUM - Programma Uitzending Managers (Manager Deployment Program) SACCOS - Savings and Credit Co-operatives Societies SADC - Southern African Development Community SADZ - Sports Association for Disable Physicaliy Zanzibar SMASSE - Strengthening of Mathematics and Science in Secondary Education SUMATRA - Surface and Marine Transport Regulatory Authority TAKUKURU - Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa TAMSA - Tanzanian Medical Students Assossiation TANESCO - Tanzania Electric Supply Company TAP - Teachers Advancement Programs TCRA - Tanzania Communication Regulatory Authority TRTF - Tax Reform Task Force TSP - Triple Supper Phosphates TUKUZA - Tumia Umeme kwa Uangalifu Zanzibar UKIMWI - Ukosefu wa Kinga Mwilini UNDP - United Nation Development Programs UNESCO - United Nation Education Scientific and Cultural Organization UWZ - Umoja wa Walemavu Zanzibar x

13 VAT - Value Added Tax VEHICLE - Vocational Education for Higher Categories and Levels VVU - Virusi Vya UKIMWI ZANAB - Zanzibar National Association of the Blind ZAPDD - Zanzibar Association for People with Developmental Disabilities ZAPHA+ - Zanzibar Assossiation for People Living with HIV/AIDS ZARI - Zanzibar Agricultural Research Institute ZATI - Zanzibar Association of Tourism Investors ZATO - Zanzibar Association of Tours Operators ZATOGA - Zanzibar Tour Guide Association ZAWA - Zanzibar Water Authority ZBC - Zanzibar Broadcasting Corporation ZBS - Zanzibar Board of Standard ZEC - Zanzibar Electoral Commission ZFDB - Zanzibar Food and Drugs Board ZIPA - Zanzibar Investment Promotion Authority ZMA - Zanzibar Maritime Authority ZSTC - Zanzibar State Trading Corporation ZURA - Zanzibar Utility Regulatory Authority xi

14 SEHEMU YA KWANZA 1.0 UTANGULIZI Awamu ya Saba ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inatekeleza mipango mbalimbali ya maendeleo kwa kuzingatia muelekeo na malengo ya Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) ya mwaka 2010 hadi. Malengo hayo yamewekwa katika Sekta za kiuchumi, uzalishaji mali, miundombinu na huduma za kiuchumi, uwezeshaji wananchi kiuchumi, huduma za kijamii na maeneo mengine ya kipaumbele. Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka imetoa mazingatio maalum kwa Zanzibar kwa kuzingatia maeneo maalumu ya kisekta. Katika kipindi cha miaka mitano ( ), Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imetekeleza Ilani ya Uchaguzi ya CCM kwa mafanikio makubwa (wastani wa asilimia 90). Mafanikio hayo yamepatikana chini ya uongozi wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mheshimiwa Dkt. Ali Mohamed Shein. Rais wa Zanzibar wa Awamu ya Saba, Dkt. Ali Mohamed Shein akiapa kuwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi tarehe 03 Novemba, 2010 Mafanikio hayo ni pamoja na kuendelea kwa hali ya amani na utulivu hapa nchini, kuongezeka kwa ukusanyaji wa mapato ya ndani kutoka vianzio mbalimbali kufuatia kuziba mianya ya uvujaji wa mapato hayo. Vilevile, mafanikio hayo yalitokana na kuimarika kwa utawala bora unaotilia 1

15 mkazo suala la uwajibikaji ndani ya sekta ya umma, kuongezeka kwa mshikamano wa wananchi, na kukua kwa sekta za kijamii na kiuchumi. Pia, mashirikiano kati ya Serikali na Sekta binafsi yameimarika kwa kiwango kikubwa. Sambamba na utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010 hadi, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar iliendelea kutekeleza Mkakati wa Kukuza Uchumi na Kupunguza Umasikini Zanzibar (MKUZA II) ambao unatekelezwa kupitia miradi mbalimbali ya kisekta kwa lengo la kuimarisha hali za maisha ya wananchi wa Zanzibar. Aidha, katika kipindi cha miaka mitano iliyopita miradi ya maendeleo imetekelezwa kwa mafanikio makubwa kwa kushirikiana na jamii pamoja na washirika wengine wa maendeleo. Miradi hiyo ni pamoja na ujenzi wa madarasa ya skuli, usambazaji wa maji, ujenzi wa vituo vya afya, ujenzi wa jengo jipya la abiria katika Uwanja wa Ndege wa Abeid Amani Karume na ujenzi wa njia ya maegesho katika uwanja huo pamoja na ujenzi wa barabara katika maeneo mbalimbali ya Unguja na Pemba. Taarifa hii ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inawasilisha maeneo mbalimbali ya utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM kwa kipindi cha miaka mitano ( ). Pia, inafafanua changamoto zilizojitokeza katika kipindi hicho cha utekelezaji wa malengo ya Ilani yaliyowekwa. SEHEMU YA PILI 2

16 2.0 HALI YA SIASA Hali ya kisiasa Zanzibar kwa kipindi cha miaka mitano iliyopita (2010-) imeendelea kuwa ya amani na utulivu. Hali hii imetokana na Sera ya Msingi ya Chama cha Mapinduzi ya kuenzi Umoja wa Kitaifa, Amani na Utulivu pamoja na wananchi kuzidi kuelewa umuhimu wa masuala haya. Aidha, hali ya sasa imewezesha kuondokana na siasa za chuki na uhasama na wananchi kushirikiana katika shughuli mbalimbali za kijamii, kiuchumi na maendeleo katika maeneo yao. 2.1 Matukio Makubwa ya Kisiasa Yaliyotokea Kufanyika kwa chaguzi ndogo kwa nafasi za Ubunge, Uwakilishi na Udiwani Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) iliendesha uchaguzi mdogo wa Ubunge katika Jimbo la Chambani Pemba. Aidha, Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) iliendesha chaguzi ndogo za Uwakilishi katika Majimbo matatu (3) ya Uzini, Bububu na Kiembe Samaki ambapo Wawakilishi wa CCM walishinda kwa kishindo katika chaguzi hizo. Pia, chaguzi ndogo mbili (2) za udiwani ziliendeshwa katika Wadi za Kiboje na Ng ombeni ambapo kwa Wadi ya Kiboje mgombea wa CCM alishinda Maadhimisho ya Sherehe ya Miaka 50 ya Mapinduzi ya Zanzibar Mheshimiwa Mahmoud Thabit Kombo kulia na Mheshimiwa Hussein Ibrahim Makungu kushoto wakila kiapo mbele ya Spika wa Baraza la Wawakilishi baada ya kushinda chaguzi za Majimbo yao ya Kiembe Samaki na Bububu 3

17 2.1.2 Maadhimisho ya Miaka 50 ya Mapinduzi ya Zanzibar Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ilifanya maadhimisho ya miaka 50 ya Mapinduzi Matukufu ambayo yalizinduliwa rasmi tarehe 15 Agosti, 2013 na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Ali Mohamed Shein na kufikia kilele chake tarehe 12 Januari, 2014 katika Uwanja wa Amaan, Zanzibar. Madhumuni ya maadhimisho hayo ni kukumbuka Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar ya tarehe 12 Januari, 1964 yaliyoleta maisha bora kwa kila Mzanzibari na kuondoa ubaguzi wa aina zote na kuleta umoja na maendelo ya kiuchumi, kijamii, kisiasa na kiutamaduni kwa makundi yote katika jamii. Siku ya Kilele cha Maadhimisho ya Sherehe za miaka 50 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar Januari, 2014 Katika maadhimisho hayo shughuli mbalimbali zilifanyika ikiwemo usafi wa mazingira, michezo na burudani, uwekaji wa mawe ya msingi pamoja na uzinduzi wa miradi. Jumla ya miradi 41 imewekewa jiwe la msingi na miradi 73 imezinduliwa wakati wa maadhimisho hayo. 4

18 Mnara wa Kumbukumbu za Miaka 5O ya Mapinduzi ya Zanzibar Ukiwa hatua za mwisho za Ujenzi katika Eneo la Michezani, Zanzibar Matukio ya Uvunjifu wa Amani Katika kipindi cha miaka mitano iliyopita, kulijitokeza matukio mbalimbali yaliyoashiria uvunjifu wa amani ambayo yalikuwa na nia ya kuifanya nchi isitawalike. Matukio hayo ni pamoja na kuuawa kwa kiongozi wa dini, kumwagiwa tindikali kwa wageni, viongozi wa dini na Serikali pamoja na mripuko wa bomu la kutupwa katika eneo la biashara la Darajani mjini Unguja. Aidha, vilijitokeza baadhi ya vikundi vya wananchi kufanya vurugu kwa kuandaa mihadhara iliyodaiwa kuwa ni ya kidini. Vikundi hivyo pia, vilifanya maandamano bila ya kupata kibali na kusababisha uharibifu mkubwa wa mali za Serikali, Chama cha Mapinduzi na za wananchi pamoja na nyumba za ibada. Vilevile, Maskani kadhaa na matawi ya Chama cha Mapinduzi yalichomwa moto na askari mmoja wa Jeshi la Polisi kuuawa kikatili katika eneo la Bububu. Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar chini ya uongozi mahiri wenye hekima na busara wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mpinduzi, Mheshimiwa Dkt. Ali Mohamed Shein ilifanikiwa kudhibiti vurugu hizo kwa kuwakamata waliohusika na kuwafikisha katika vyombo vya sheria. 5

19 Maskani ya CCM ya Mwembe Kisonge iliyopo Michenzani iliyotiwa Moto na wafuasi wa Kundi la Muamsho mwaka Masuala ya Muungano Katika kipindi cha miaka mitano ya (2010-) nchi yetu iliadhimisha miaka 50 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar. Kipindi hicho ni kirefu na nchi yetu ina kila sababu ya kujivunia kutokana na kuudumisha Muungano wetu kwa muda wote huo. Mafanikio makubwa yamepatikana kupitia Muungano wetu huu ikiwa ni pamoja na kuendelea kubaki katika hali ya amani na utulivu katika nchi yetu na kuwepo kwa fursa ya kuendeleza na kuimarisha mahusiano ya kidugu yaliyopo kati ya wananchi wa Tanzania bara na Zanzibar pamoja na kuimarisha maendeleo ya kijamii na kiuchumi. 6

20 Kushoto Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akikagua gwaride rasmi la maadhimisho ya miaka 50 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar. Kulia tamasha la halaiki siku ya Kilele cha miaka 50 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar Vikao vya Pamoja vya Mashirikiano Katika kuuimarisha Muungano wa Tanganyika na Zanzibar na kuzipatia ufumbuzi hoja za Muungano wetu, Vikao mbalimbali vya Kamati ya Pamoja, Sektretariat na Vikao vya Mashirikiano vya Kisekta vimefanyika ili kujadili na kutatua hoja zilizowasilishwa. Vikao vya Pamoja viliwashirikisha Mheshimiwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mheshimiwa Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar chini ya Uenyekiti wa Mheshimiwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Jumla ya hoja 15 zimewasilishwa kwa kipindi cha mwaka 2010 hadi ambapo hoja 10 tayari Serikali zetu mbili zimefikia makubaliano muafaka na hoja tano (5) zilizobakia ziko katika hatua ya kuzitafutia ufumbuzi wa kudumu. Hoja zilizopatiwa ufumbuzi ni:- i. Utekelezaji wa Sheria ya Haki za Binaadamu Zanzibar. ii. Uvuvi kwenye ukanda wa Bahari Kuu. iii. Utekelezaji wa Merchant Shipping Act katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Uwezo wa Zanzibar Kujiunga na IMO. iv. Mgawanyo wa Mapato. Hoja hii imegusa vipengele viwili. Mgawanyo wa Mapato yatokanayo na Misaada kutoka nje. Misaada ya mikopo ya fedha kutoka IMF. 7

21 v. Uwezo wa Zanzibar kukopa ndani na nje ya nchi. vi. vii. viii. ix. Malalamiko ya Wafanyabiashara wa Zanzibar kutozwa kodi mara mbili. Ongezeko la gharama za Umeme kutoka TANESCO kwenda ZECO. Mfuko wa Maendeleo ya Jimbo wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Ushiriki wa Zanzibar katika Jumuiya ya Afrika Mashariki. x. Ajira kwa Watumishi wa Zanzibar katika Taasisi za Muungano. Hoja ambazo ziko katika hatua za kutafutiwa ufumbuzi ni:- i. Utafutaji na Uchimbaji wa Mafuta na Gesi Asilia. ii. iii. iv. Usajili wa vyombo vya moto. Tume ya Pamoja ya Fedha. Kodi nyenginezo (PAYEE). v. Ushirikiano wa Zanizibar na Taasisi za Nje. Moja ya Kikao cha Kamati ya Pamoja cha SMT na SMZ chini ya Uenyekiti wa Makamu wa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mohamed Gharib Bilal akiwa na Waziri Mkuu Mheshimiwa Mizengo Kayanza Peter Pinda na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi Mchakato wa Kuandaa Katiba Mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar zilianzisha mchakato wa kutayarisha Katiba Mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mchakato huo ulipitia katika hatua mbalimbali ikiwemo utungwaji wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ya 2013, kuundwa kwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, ukusanyaji wa maoni ya wananchi, kuandaa na kujadiliwa Rasimu ya Awali ya Katiba katika Mabaraza ya Katiba na hatimae Bunge Maalumu la 8

22 Katiba na kupatikana kwa Katiba Inayopendekezwa ambayo inasubiri hatua ya kupigiwa kura na wananchi. Katiba hiyo inayopendekezwa inagusa makundi yote ya jamii wakiwemo watu wenye ulemavu, wanawake na watoto, vijana na wazee, wafanyakazi, wakulima, wavuvi, wafugaji na wafanyabiasha. Pia, Katiba hiyo inayopendekezwa imelenga kuimarisha zaidi Muungano wa Tanzania kwa kuyapatia ufumbuzi masuala yote yaliyotajwa kama ni changamoto za Muungano. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein Wakizionyesha Nakala za Katiba Inayopendekezwa katika Uwanja wa Jamhuri -Dodoma SEHEMU YA TATU 9

23 3.0 SEKTA YA KIUCHUMI Katika kutekeleza Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi ya 2010 hadi, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imeendeleza mafanikio yote ya kiuchumi yaliyopatikana nchini ikiwemo kutekeleza Sera na Sheria za Uwekezaji pamoja na ujenzi wa msingi wa uchumi endelevu unaoendeshwa kwa nguvu za soko. 3.1 Ukuaji wa Uchumi Uchumi wa Zanzibar umeendelea kuonyesha mwenendo mzuri wa ukuaji mwaka hadi mwaka. Katika kipindi cha miaka mitano, uchumi wa Zanzibar umekuwa kutoka asilimia 6.4 mwaka 2010 hadi asilimia 7.4 mwaka Aidha, mfumko wa bei ulikuwa ukipanda na kushuka katika kipindi cha miaka mitano (5). Mwaka 2010/2011 mfumko wa bei ulikuwa wa wastani wa asilimia 6.1 na ulipanda kufikia asilimia 14.7 mwaka 2011/2012 na mwaka 2013/14 ulishuka na kufikia kiwango cha asilimia 5. Takwimu za ukuaji huo zinaonekana katika jedwali namba 1. Jadweli namba 1. Takwimu za ukuaji wa uchumi Zanzibar ( ) KIASHIRIA 2010/ / / /14 Ukuaji wa Pato la Taifa % Mfumko wa bei % Chanzo: Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, 2014 Ukuaji huo wa uchumi wa mwaka hadi mwaka umechangiwa kwa kiasi kikubwa na mambo yafuatayo: Kuimarika kwa Sekta ya Kilimo, Misitu na Uvuvi; Kuimarika kwa Sekta ndogo ya Uzalishaji wa Viwanda; Kuimarika kwa Sekta ya Huduma kulikochangiwa na ongezeko la ukuaji wa Sekta ndogo ya Hoteli na Mikahawa; Kuongezeka kwa idadi ya watalii wanaoingia nchini mwaka hadi mwaka; Kuwepo kwa hali ya utulivu, amani na mshikamano wa wananchi ambayo imejenga mazingira mazuri ya kuwekeza na kufanyakazi kunakoleta tija kwa nchi yetu. 10

24 3.2 Mfumko wa Bei Kwa ujumla kasi ya mfumko wa bei imeshuka kutoka asilimia 6.1 mwaka 2010 hadi asilimia 5.0 mwaka Hata hivyo, kwa kipindi cha mwaka 2011 hali ya mfumko wa bei ilipanda zaidi hadi kufikia asilimia 14.7 kutokana na sababu za kupanda kwa bei ya mafuta katika soko la Dunia na kushuka kwa thamani ya Sarafu ya Tanzania. Kushuka kwa mfumko wa bei mwaka 2013 kulitokana na juhudi za Serikali katika kudhibiti mfumko wa bei ikiwemo kutoa ruzuku za pembejeo za kilimo kwa wakulima ambako kulipelekea kuongezeka kwa uzalishaji wa mazao ya chakula nchini. Aidha, mfumko wa bei uliendelea kushuka kutokana na Serikali kuendelea kutoa misamaha ya kodi kwa bidhaa muhimu za chakula kama vile Unga, Sukari na Mchele na kushuka kwa bei za bidhaa za mafuta na chakula katika Soko la Dunia. 3.3 Mapato na Matumizi ya Serikali Miongoni mwa mafaniko ya utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM kwa kipindi cha miaka mitano ni ongezeko la ukusanyaji wa mapato kutoka vianzio mbalimbali vilivyopo nchini. Kwa ujumla mapato ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar yameonyesha kuongezeka kutoka Shilingi bilioni 181 kwa mwaka 2010/11 hadi kufikia Shilingi bilioni 330 mwaka 2013/2014. Makusanyo hayo ya Shilingi bilioni zilizokusanywa ni sawa na asilimia 94 ya makadirio ya Shilingi bilioni Ongezeko hilo la mapato ya ndani limetokana na juhudi mbalimbali zilizofanywa na Serikali zikiwemo kuziba mianya ya uvujaji wa mapato ya nchi kwa kuyafanyia kazi mapendekezo yaliyotolewa kupitia maabara ya upatikanaji wa rasilimali fedha resource mobilization na mapitio ya Sekta ya Fedha Kushuka kwa Kiwango cha Nakisi ya Bajeti Katika kukabiliana na ukuaji mkubwa wa mahitaji ya nchi, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imefanya jitihada mbalimbali kuhakikisha upatikanaji wa rasilimali fedha ambao utaendana na mahitaji ya nchi yetu ili kushusha nakisi ya bajeti kutoka uwiano wa asilimia 9.2 ya Pato la Taifa la mwaka 2007/2008 na kufikia asilimia 8.0 katika mwaka 2014/. Miongoni mwa jitihada zilizofanikisha ushushaji wa nakisi ya bajeti ni pamoja na kuimarika kwa usimamizi wa ukusanyaji mapato pamoja na kutumika kwa hatua kadhaa za mikakati ya kuimarisha mapato katika kipindi hicho. Mikakati hiyo ni pamoja na kufanya marekebisho ya sheria na viwango vya kodi na ada mbalimbali zikiwemo marekebisho ya Sheria ya Ongezeko la Thamani (VAT), Sheria ya Kodi za Hoteli, Sheria ya Ada za Bandari, Ushuru wa Stempu, Sheria ya Kodi ya Mafuta pamoja na Sheria 11

25 ya Usafiri wa Barabarani. Pamoja na jitihada zilizofanywa, Serikali ilichukua hatua kadhaa za kiutawala na utendaji ambazo zimesaidia sana kuongeza ukusanyaji wa Mapato ya Serikali. 3.4 Kuimarisha Maeneo Huru ya Kiuchumi ya Fumba. Serikali imeanza kutekeleza ahadi ya Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka ya kuendeleza Maeneo Huru ya Kiuchumi ya Fumba. Katika utekelezaji wa ahadi hii, Serikali imechukuwa hatua mbalimbali ikiwa ni pamoja na kutayarisha Mpango Mkuu wa Matumizi ya Ardhi Fumba, upimaji na utayarishaji wa mchoro wa ramani ya eneo hilo. Jumla ya hekta 3,000 zimepimwa na kugaiwa kwa matumizi tofauti ambapo hekta 743 zimetengwa kwa ajili ya uwekezaji wa shughuli za kibiashara, hekta 1,310 kwa ajili ya vijiji vya asili na makaazi na hekta 946 kwa ajili ya eneo la akiba. Pia, Serikali imefanikiwa kukamilisha ujenzi wa njia kuu ndani ya eneo la uwekezaji Fumba yenye urefu wa kilomita 10 kwa kiwango cha lami. Hatua ya kutengeneza njia ndogondogo tatu za ndani ambapo njia moja yenye urefu wa kilomita mbili kuanzia skuli ya Bwefum-Kororo imekamilika na kazi ya kushughulikia njia nyengine mbili za Bweleo Pwani na Dimani Fumba inaendelea. Vilevile, katika uendelezaji wa utekelezaji wa Mpango Mkuu wa Eneo Huru la Kiuchumi Fumba, Serikali imekamilisha mazungumzo na Muwekezaji wa Kampuni mama ya Bakheressa Group juu ya kushirikiana katika uwekezaji wa Mradi wa Ujenzi wa Mji wa Kisasa wa Fumba (Fumba Bay Satillite City). Kwa sasa kiwanda kikubwa cha usarifu maziwa cha Azam Dairy Milk na Zanzibar Fiber Glass tayari vimeanzishwa na vinaendelea na kazi na miradi mengine ya huduma na nyumba za makaazi imo katika hatua za awali. Kutekelezwa kwa miradi ya aina hii katika eneo hilo la Fumba kunatarajiwa kuzalisha ajira zaidi kwa wananchi pamoja na kukuza Pato la Taifa. Aidha, Serikali imeanza hatua za utekelezaji wa miradi mikubwa ikiwemo mradi wa ujenzi wa mji mdogo wa kisasa, mradi wa uanzishaji wa Eneo la Viwanda (Industrial Park) na mradi wa kujenga Kituo kikubwa cha Mikutano cha Kimataifa (Zanzibar International Convention Centre). 12

26 Jengo na Mitando ya Kiwanda cha Fiber Glass katika Maeneo Huru ya Kiuchumi - Fumba 3.5 Uwakilishi wa Sekta Binafsi katika Vikao Mbalimbali Serikali kupitia Wizara ya Fedha imeendelea kushirikiana na Sekta Binafsi katika vikao mbalimbali ambavyo vinaimarisha utendaji kazi wa Serikali. Kwa sasa Sekta Binafsi zinauwakilishi katika vikao vya kuimarisha mapato Tax Reform Task Force (TRTF), vikao vya kujadili Pato la Taifa (GDP), Faharisi ya Bei ya Mlaji Consumer Price Index (CPI) na vikao vya kuratibu misaada kwa taasisi zisizo za kiserikali ( Aid Cordination Meeting for NGOs ). Lengo kuu la uwakilishi huo ni kuendelea kuwavutia wawekezaji wa ndani ili wawekeze katika sekta mbalimbali za kijamii na kiuchumi. 3.6 Kuandaa Mazingira Bora ya Kiuchumi ili Kuvishawishi Vyombo vya Fedha Kutoa Mikopo Yenye Masharti Nafuu. Katika kuandaa mazingira bora ya kiuchumi, Serikali imeifanyia marekebisho Sheria ya Fedha ili kuweza kuendana na mazingira halisi ya kiuchumi. Aidha, Serikali imefanya mapitio ya Sekta ya Fedha na kuweza kuziona kasoro zilizopo na kuzifanyia kazi. Vilevile, Sera ya Sekta ndogo ndogo za Fedha imeandaliwa na kuanza kutumika. Sera hiyo inatoa muongozo wa kuwawezesha wajasiriamali wadogo kujipatia mitaji kwa urahisi. 13

27 Pia, Serikali imeimarisha huduma za mikopo kwa wajasiriamali wadogo wadogo kwa kuunganisha mifuko iliyokuwepo na kuanzisha Mfuko mmoja unaojulikana kama Mfuko wa Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi. Madhumuni ya kuanzishwa kwa Mfuko huo ni kutanua fursa za mikopo nafuu kwa wajasiriamali, hususan wanawake, vijana na watu wenye kipato cha chini, ili waweze kuanzisha na kuimarisha shughuli za kiuchumi zitakazowasaidia kujiajiri na kunyanyua kipato chao. Mfuko wa Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi una mtaji wa mikopo (Revolving Loan Fund) wenye thamani ya Shilingi bilioni 2.3. Sambamba na hayo, Serikali katika kipindi cha miaka mitano iliyopita imetoa mikopo 1,603 yenye thamani ya Shilingi bilioni 1.45 katika Shehia 305 za Unguja na Pemba, ambayo imetoa jumla ya ajira za moja kwa moja 20,614 kwa makundi mbalimbali. Kati ya waliofaidika na ajira na kujihakikishia kipato ni wanaume 8,741 na wanawake 11,873. Aidha, Serikali imeweka fedha za dhamana (Shilingi 100,000,000) katika Benki ya CRDB ili kuviwezesha vikundi vya vijana kujipatia mikopo kutokana na dhamana hiyo. 3.7 Kuanzisha Maeneo Mapya ya Kiuchumi Serikali imeendelea kuzitangaza fursa za uwekezaji zilizopo nchini kwa kupitia njia mbalimbali, ikiwemo kuimarisha tovuti yake ( na kuitafsiri katika lugha za kigeni (Kichina, Kituruki na Kirusi) ili kufikia Soko la Kimataifa. Hatua hii itasaidia kutangaza fursa zilizopo za uwekezaji kwa kuwavutia wawekezaji kutoka nchi hizo kuja kuwekeza nchini. Kupitia juhudi hizo wawekezaji kutoka Poland wamewekeza miradi minne (4) yenye mtaji wa Dola za Kimarekani 29,471,549. Aidha, Serikali katika kipindi hiki imepokea ujumbe wa wawekezaji kutoka Marekani, Uholanzi, Urusi, Croatia, Uturuki na China kwa lengo la kuona fursa zaidi za uwekezaji nchini. Pia, Serikali ilipokea ugeni kutoka Ubalozi wa Thailand ulioko Nairobi na kukubaliana kushirikiana katika uwekezaji. Serikali kupitia Mamlaka ya Uwekezaji imefanya ziara za kujitangaza katika nchi mbalimbali ikiwemo Marekani, China, Uturuki na Uholanzi. 3.8 Miradi Iliyowekezwa kwa Kipindi cha Katika kipindi cha Serikali imeweza kuidhinisha jumla ya miradi 153 ya uwekezaji yenye mtaji wa Dola za Kimarekani 1,493,139,968. Kati ya miradi hiyo, miradi 63 inamilikiwa na wawekezaji wazalendo. Miradi hiyo inatarajiwa kutoa ajira zipatazo 6,658 kwa wananchi, hali hii itasaidia kupunguza tatizo la ajira nchini. Sekta ya Utalii inaongoza kwa kuwa na asilimia 52 ya miradi iliyoidhinishwa kwa kipindi hiki. Aidha, Serikali imefanya tafiti mbalimbali ikiwemo 14

28 utafiti wa kuibua maeneo mapya ya kuwekeza na kufanya utafiti wa mwenendo wa Mitaji Binafsi ili kuona namna gani mitaji hiyo inatoa mchango katika uchumi wa nchi. SEHEMU YA NNE 15

29 4.0 SEKTA ZA UZALISHAJI MALI 4.1 KILIMO Sekta ya Kilimo bado inaendelea kuwa ni mhimili mkuu wa uchumi wa Zanzibar na inatoa mchango wa moja kwa moja kwa wananchi katika kujikimu kimaisha. Sekta hii pia ni muhimu kwa kukuza hali ya uhakika wa chakula na kuimarisha lishe na afya za wananchi walio wengi vijijini na mijini. Kwa wastani Sekta hii inachangia asilimia 30 ya Pato la Taifa na inakadiriwa kuwa zaidi ya asilimia 70 ya wananchi wanategemea Sekta ya Kilimo kwa kuwapatia ajira na kipato. Kwa kipindi cha miaka mitano, Serikali imetekeleza mambo mbalimbali katika kuimarisha na kuendeleza Sekta ya Kilimo Kutekeleza Mkakati wa Uimarishaji wa Zao la Karafuu Serikali imetekeleza mkakati wa kuliimarisha zao la karafuu ambao umeanza kutoa mafanikio kwa kuongezeka kwa kiwango cha uoteshaji wa miche na uzalishaji wa zao la karafuu kwa ujumla. Jumla ya miche 2,216,328 katika vitalu mbalimbali vya Unguja na Pemba imezalishwa katika kipindi cha Kati ya miche hiyo, miche 1,339,192 imetolewa na kusambazwa kwa wakulima bila malipo kwa ajili ya kupandwa mashambani ambapo wastani wa asilimia 44 ya miche hiyo imeota. Vilevile, Serikali imeongeza bei ya zao la karafuu kwa wakulima kutoka Shilingi 4,500 (2010) hadi kufikia Shilingi 14,000 (2014) kwa kilo moja. Hali hii imewahamasisha zaidi wakulima kulishughulikia na kuongeza uzalishaji wa zao hilo kutoka tani 2,673 mwaka 2010 na kufikia tani 5,340 mwaka

30 Rais wa Zanzibar Dkt. Ali Mohamed Shein akikagua miche ya mikarafuu katika vitalu - Pemba Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akiangalia zao la karafuu alipotembelea katika shamba la Bw.Said Sinani Shumbageni Kusini Pemba Pia, Serikali imefanya tathmini ya Sensa ya Miti (Woody Biomass Survey) mwaka 2013 ambayo imeonesha kwamba, Zanzibar kwa sasa ina idadi ya mikarafuu 4,131,783 (Unguja 277,196 na Pemba 3,854,587). Tathmini hiyo pia inaonyesha kuwa asilimia 60 ya Mikarafuu ni midogo yenye umri kati ya mwaka mmoja hadi sita. Hivyo, Zanzibar bado inayo nafasi ya kuongeza uzalishaji 17

31 wa karafuu kwa wingi zaidi kwa siku zijazo. Aidha, Serikali katika kuendeleza zao la karafuu, mwaka 2013 ilianzisha mashamba darasa 20 ya mikarafuu (Pemba 12 na Unguja 8) kwa ajili ya kuotesha miche bora na kutoa taaluma ya uzalishaji wa mikarafuu kwa wakulima Kuimarisha Miundombinu ya Umwagiliaji Maji Serikali inaendelea kuimarisha miundombinu ya umwagiliaji maji ili kukabiliana na mabadililiko ya hali ya hewa pamoja na kuongeza uzalishaji na kipato kwa wakulima. Katika kipindi cha miaka mitano, jumla ya hekta 800 (2014) kutoka hekta 600 (2010) zimeimarishwa miundombinu ya umwagiliaji maji. Pia, mita 170 za misingi zimejengwa kwa saruji na mita 200 kwa udongo, mita 670 zimefanyiwa matengenezo na vigingi 50 vimejengwa kwa Unguja na Pemba. Aidha, matuta kwa ajili ya misingi ya kumwagilia maji mita 2,000 yamejengwa pamoja na kazi ya kupima na kusanifu misingi ya kutolea maji machafu (Drainage) mita 4,000 imefanyika. Aidha, maeneo 40 ya uvunaji wa maji ya mvua yameanzishwa na wakulima 2,000 wamefaidika Unguja na Pemba. Kushoto Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akipata maelezo wakati alipotembelea na kukagua miundombinu na maendeleo ya Kilimo cha Umwagiliaji wa Mpunga katika Bonde la Bumbwisudi Zanzibar Pia, kazi ya ujenzi wa bwawa la kukusanyia maji imeanza katika bonde la Mtwango. Jumla ya wakulima 8,000 kati ya wakulima 28,000 wanaolima zao la mpunga wameongeza uzalishaji kutoka tani 1.3 na kufikia tani 3.8. Aidha, Serikali inaendelea na kazi ya kupima, kuchora ramani na kusanifu miundombinu ya umwagiliaji maji katika vituo vya Cheju, Kilombero, Chaani, Mlemele na Makwararani maeneo ambayo yanajumuisha hekta 2,

32 4.1.3 Kuendeleza Programu za Tafiti za Kilimo na Maliasili kwa Kuwashirikisha Wakulima na Washiriki Wengine Serikali imeendelea na jitihada zake katika kuendeleza tafiti tofauti za kilimo na maliasili pamoja na kusambaza matokeo ya tafiti hizo kwa wakulima na wadau wengine wa kilimo kupitia Taasisi ya Utafiti wa Kilimo ili kuongeza uzalishaji na tija Utafiti wa Mazao ya Nafaka na Jamii ya Kunde Taasisi ya Utafiti wa Kilimo ya Zanzibar (ZARI), imefanya na kuendeleza tafiti mbalimbali katika mazao ya nafaka na jamii ya kunde kwa mashirikiano na taasisi za utafiti za Kanda ya Afrika Mashariki na Kati chini ya uratibu wa Kanda ya IRRI. Katika tafiti za zao la mpunga, ZARI ilifanya uchunguzi wa awali wa mbegu 28 za mpunga kutoka IRRI katika bonde la umwagiliaji maji la Mtwango, aina 15 ya mbegu za mpunga kutoka IRRI zilijaribiwa katika bonde la utafiti wa mpunga Mwera-Barabarani. Uchunguzi wa awali wa aina 7 za mbegu za mpunga kutoka Vietnam katika kituo cha utafiti wa mpunga Mwera (Unguja) na Tungamaa (Pemba) umeonesha kuwa mbegu zote zinafaa kuendelezwa na hatua nyengine za jaribio zinaendelea. Katika tafiti shirikishi ya uchunguzi wa Kanda ya Afrika Mashariki na Kati, kila nchi ilitakiwa itoe mbegu mbili kwa ajili ya jaribio hilo ambapo mbegu ya SUPA BC ilijitokeza kuwa ni miongoni mwa mbegu zilizofanya vizuri. Shamba la majaribio la mpunga la Cheju juu ya Utafiti wa matumizi ya mbolea aina ya YARAMILLA Jaribio la Mbolea Mpya na Mafunzo kwa Wakulima Chini ya Mradi wa NAFAKA Katika kipindi cha miaka mitano, Serikali imeendelea na majaribio ya mbolea mpya za kilimo zikiwemo za YaraMilla na UDP. Majaribio hayo yalifanyika katika vituo vya kilimo Kizimbani, Ole na Bumbwisudi. Matokeo ya awali ya tafiti hizo yamepatikana na kuonyesha kuwa YaraMilla 19

33 na UDP zimefanya vizuri kwa asiliamia 60 katika mpunga wa kutegemea mvua na asilimia 49 katika mpunga wa umwagiliaji maji ukilinganisha na TSP na Urea ambazo zimezoeleka. Serikali imetoa mafunzo ya nadharia na vitendo kwa wakulima 400 juu ya mbinu bora za kilimo cha mpunga cha umwagiliaji maji. Aidha, wakulima 2,000 (700 Pemba na 1,300 Unguja) walipatiwa mafunzo ya mbinu bora za uzalishaji mpunga katika mashamba darasa 40 ambapo kila shamba walifundishwa wakulima 50. Picha ya Shamba darasa la Mpunga huko Bumbisudi Ruzuku katika Kilimo Serikali inaendelea kutoa ruzuku za pembejeo na huduma za matrekta kwa lengo la kuimarisha uzalishaji wa mazao mbali mbali, hasa zao la mpunga. Katika kipindi cha miaka mitano (2010 ), Serikali imetoa ruzuku ya jumla ya shilingi 7,129,591,148 za kuendeleza kilimo, kwa ajili ya ununuzi wa mbolea, madawa, mbegu na kutoa huduma za matrekta kwa wakulima. Katika kufanikisha suala hili la ruzuku, Serikali imepunguza bei ya mbolea kutoka bei halisi ya soko ya shilingi 80,000 hadi shilingi 10,000 kwa mfuko wa kilo 50 (sawa na ruzuku ya asilimia 88). Pia, imepunguza bei ya madawa kutoka shilingi 25,000 hadi shilingi 10,000 kwa lita (ambayo ni ruzuku ya asilimia 60), na bei ya mbegu ya mpunga kutoka shilingi 2,500 hadi shilingi 200 kwa kilo (ikiwa ni ruzuku ya asilimia 92). Vile vile, wakulima wanalipia shilingi 16,000 tu kwa ekari moja kwa ajili ya kupatiwa huduma za matrekta (kuchimba na kuburuga) kutoka bei halisi ya shilingi 30,000 (hii ni ruzuku ya asilimia 57). Zaidi ya kaya 60,000 (wastani wa wakulima 360,000) zinafaidika na ruzuku zinazotolewa na Serikali katika Kilimo kwa Unguja na Pemba. 20

34 Tafiti za Mazao ya Mizizi (Muhogo na Viazi Vitamu) Katika jitihada za kutafuta mbegu bora za mazao ya mizizi, Serikali imefanya majaribio ya mbegu bora aina saba (7) za muhogo katika maeneo matano (5) ya mashamba ya wananchi Unguja na Pemba. Maenoeo hayo yapo katika vijiji vya Kizimbani, Bungi na Chaani kwa Unguja na Matangatuani na Pembeni kwa Pemba. Tafiti hizo zinaonyesha kwamba asilimia 50 ya mbegu zinafaa kutokana na kuvumilia maradhi na wadudu. Aidha, Serikali imefanya majaribio ya viazi vitamu yalioyojumuisha aina 34 za mbegu katika maeneo sita (6) ambayo ni Bambi, Kizimbani na Kilombero kwa Unguja na Makangale, Mjimbini na Matangatuani kwa Pemba. Sambamba na kazi hizo, Serikali kwa kushirikiana na Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Zanzibar imeendelea kuhifadhi mbegu 36 za kienyeji na za kigeni kwa ajili ya kutunza viini vya kijenitiki (Genetic Resources Conservation). Muhogo uliolimwa kutokana na Mbegu Bora iliyofanyiwa Utafiti na Ushauri wa Kitaalamu katika Shamba la Kizimbani Uboreshaji wa Miundombinu ya Utafiti Serikali kupitia Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Zanzibar kwa kushirikiana na wadau wengine wa maendeleo imekamilisha ujenzi wa maabara mpya ya utafiti wa mpunga pamoja na ukarabati wa maabara ya udongo na maabara ya usarifu wa mazao. Maabara hizo zimechangia katika kuongeza juhudi za utafiti wa mazao ya chakula na biashara. 21

35 Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akiangalia tafiti mbalimbali katika maabara ya utafiti katika Chuo cha Kilimo Kizimbani Kuhimiza na Kushajiisha Matumizi ya Pembejeo na Mbinu Bora za Kilimo Serikali imenunua Matrekta mapya 45 kutoka SUMA JKT Tanzania Bara (18 Pemba na 27 Unguja) na imepokea matrekta 20 kutoka SUMA JKT Bara, Matrekta 10 yamepelekwa Pemba. Vile vile, Serikali imenunua mashine za kuvunia mpunga 14 (Combine harvester) na kuyafanyia matengenezo matrekta 37 (Pemba 13 na Unguja 24). Aidha, Serikali imenunua jumla ya Tani 5,870.5 za mbolea ya TSP na Urea na kusambazwa kwa wakulima Unguja na Pemba pamoja na lita 68,000 za dawa ya kuulia magugu. Aidha, Jumla ya tani 2,145.6 za mbegu ya mpunga, tani 20 za mbegu ya kunde zimenunuliwa na kusambazwa kwa wakulima na tani 623 ya mbegu ya mpunga aina ya BKN Supa imezalishwa kupitia wakulima wa Zanzibar. Matrekta kutoka SUMA JKT yakifanya kazi za kutayarisha mashamba katika Bonde la Kilombero 22

36 Jitihada hizi zimewezesha kuongeza eneo la uzalishaji kutoka ekari 10,000 mwaka 2010 hadi kufikia ekari 34,000 mwaka Aidha, kumekuwepo na ongezeko la idadi ya kaya zinazojihusisha na kilimo cha mpunga kutoka kaya 10,000 mwaka 2010 hadi kufikia kaya 70,000 mwaka Vilevile kumekuwepo ongezeko la uzalishaji wa mpunga kutoka tani 20,000 mwaka 2010 hadi kufikia tani 33,655 mwaka Kuendelea Kuhimiza na Kutilia Mkazo Mafunzo na Matumizi ya Kanuni za Kilimo Bora kwa Mazao ya Chakula, Biashara na Matunda Serikali imeendelea kutoa mafunzo kwa wakulima kupitia njia ya kuwatembelea wakulima mashambani, mashamba darasa na skuli za wakulima. Aidha, mafunzo kwa wakulima pia yamekuwa yakitolewa kupitia Chuo cha Kilimo cha Kizimbani. Katika kuendeleza utoaji wa huduma za elimu kwa wakulima, Serikali imeongeza idadi ya mabwanashamba/mabibishamba kutoka 172 mwaka 2010 hadi kufikia 212 mwaka. Pia, mitego 85,000 ya kunasia nzi waharibifu wa matunda imesambazwa kwa wakulima, Unguja na Pemba Uimarishaji wa Chuo cha Kilimo Kizimbani Katika utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM Serikali imekiimarisha Chuo cha Kilimo Kizimbani katika utoaji wa mafunzo na ujenzi wa miundombinu. Kwa upande wa mafunzo, jumla ya vijana 48 wamemaliza mafunzo ya kilimo na mifugo katika ngazi ya Diploma na Vijana 300 katika ngazi ya Cheti. Aidha, Chuo kinaendelea kutoa mafunzo kwa wanafunzi 140 wa ngazi ya cheti na 50 kwa ngazi ya Diploma. Pia, walimu 10 wa chuo hicho wanaendelea na masomo ngazi ya Shahada ya Pili (Masters) na mwalimu mmoja (1) anaendelea na masomo ya Shahada ya Tatu (PhD). Kwa upande wa miundombinu, Serikali imejenga Dakhalia ya wanafunzi wa kike yenye uwezo wa kuchukua wanafunzi 28 kupitia msaada kutoka IFAD pamoja na michoro ya Ujenzi wa Dakhalia yenye ghorofa 4 na uwezo wa kuchukua wanafunzi 500 umekamilika. Aidha, ukarabati wa mabweni mawili (2), madarasa manne (4) na majengo mawili (2) ya ofisi umefanyika pamoja na matengenezo na ununuzi wa vifaa vya maabara ya mifugo, maktaba, samani na vifaa mbalimbali. Vilevile, katika kuimarisha elimu inayotolewa, ununuzi wa vifaa vya kufundishia na vitendea kazi ikiwemo vitabu 860 vya kiada na ziada na kompyuta 50 zimenunuliwa na kuanza kutumika. 23

37 Makamu wa Pili wa Rais Mheshimiwa Balozi Seif Ali Iddi akifungua na kukagua Jengo la Dakhalia ya Chuo cha Kilimo Kizimbani 24

38 Wanafunzi wa Chuo cha Kilimo Kizimbani wakiwa katika masomo kwa vitendo Kutekeleza Mkakati wa Kuanzisha Akiba ya Chakula ya Zanzibar (National Food Reserve) Katika utekelezaji wa Mkakati wa Kuanzisha Akiba ya Chakula Zanzibar kwa lengo la kuhakikisha upatikanaji wa kuaminika wa chakula pamoja na kuwa na chakula cha akiba kwa ajili ya kukabiliana na dharura ya ukosefu na upungufu wa chakula nchini unaoweza kusababishwa na hali ya ukame, mafuriko na majanga mengine ya asili, Serikali inaendelea kutekeleza mpango wake wa kuanzisha Hifadhi ya Chakula kwa kuanza kuyafanyia ukarabati maghala mawili makubwa yaliyopo Tibirinzi - Pemba na Malindi - Unguja. Vilevile, Serikali imetayarisha miongozo ya kisheria na taratibu juu ya uendeshaji na usimamiaji wa hifadhi hiyo ikiwemo; Muongozo wa Kazi na Taratibu za Uendeshaji na Kanuni za Kusimamia hifadhi kwa lengo la kuweka utaratibu na mfumo wa kisheria katika uendeshaji na usimamiaji wa hifadhi ya chakula nchini. Aidha, Serikali imeanza utayarishaji wa Programu maalumu ya kuongeza uzalishaji wa mpunga kwa ajili ya Hifadhi ya Chakula. Mikakati ya Serikali ni kuongeza ufanisi katika uzalishaji wa mpunga na hatimae Hifadhi ya Chakula iendeshwe kwa kutegemea mpunga unaozalishwa nchini na kupunguza utegemezi wa mchele kutoka nje ya nchi. 25

39 Ghala za Akiba ya Chakula kwa Unguja na Pemba 4.2 UFUGAJI Ili kuleta mapinduzi ya ufugaji nchini, Chama cha Mapinduzi kupitia Ilani ya Uchaguzi ya mwaka iliagiza Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kushughulikia utekelezaji wa sera na sheria ya mifugo pamoja na programu na miradi mbalimbali zitakazowezesha wafugaji wadogo wadogo kuendeleza ufugaji wa kisasa. Aidha, Ilani hiyo iliagiza kuimarishwa kwa kazi za utafiti na huduma za kinga na tiba ya mifugo na kuendeleza vituo vya huduma za ufugaji na huduma za kinga na tiba ya mifugo. Katika kusimamia utekelezaji wa Ilani, Serikali imesimamia matibabu ya wanyama ambapo jumla ya wanyama 240,108 walitibiwa, wanyama 258,350 walichanjwa na wanyama 103,688 walikogeshwa. Pia, katika kuikinga Zanzibar na magonjwa yasiyo na mipaka, jumla ya sampuli 3,658 za maziwa na 2,505 za damu zimefanyiwa uchunguzi wa bacteria na fungus, sampuli 4,034 za kinyesi kwa ajili ya uchunguzi wa minyoo, na sampuli tofauti 3,000 (2,922 za maziwa, 30 za kuku na 48 za maji) zimeoteshwa katika maabara za Wizara. Aidha, wanyama 14,626 walikaguliwa katika Kituo cha Karantini cha Kisakasaka, wanyama hao ni pamoja na ng'ombe, mbuzi, kondoo, jamii ya ndege na wanyama wengineo. Katika kituo cha bandarini jumla ya wanyama na jamii za ndege 5,105,352 walikaguliwa na katika kituo cha Uwanja wa Ndege wanyama na ndege 731,802 pia walikaguliwa. Vilevile, katika ukaguzi wa wanyama waliochinjwa, Ng ombe 41,180, Mbuzi 5,538 na Kondoo 3,310 walikaguliwa. 26

40 Wanyama wakifanyiwa Ukaguzi na Matibabu Aidha, kupitia mradi wa kichaa cha mbwa, jumla ya mbwa 19,822 na paka 5,577 walipatiwa chanjo dhidi ya maradhi hayo. Vilevile, jumla ya mbwa 3,507 na paka 1,693 walifungwa uzazi. Mbwa 3,595 na paka 1,319 walipatiwa matibabu ya maradhi mbalimbali, kati yao mbwa 9,945 na paka 2,142 walipatiwa dawa za minyoo, na mbwa 4,702 na paka 1,258 waliogeshwa ili kuwakinga na kupe. Serikali imetoa mafunzo kwa watoa huduma za msingi (CAHWs) 42, na madaktari wasaidizi 90 kwa Unguja na Pemba. Pia, mafunzo juu ya kujikinga na ugonjwa wa kichaa cha mbwa yalitolewa kwa skuli mbalimbali za Unguja na Pemba na vipindi mbalimbali vya kuhamasisha jamii juu ya athari za kichaa cha mbwa vimerushwa kupitia vipindi vya redio na televisheni Kuendeleza Kazi za Tafiti kwa Wanyama Katika kipindi cha miaka mitano , Serikali imendeleza kazi ya utafiti wa upandishaji wa wanyama wakiwemo ng ombe, mbuzi na kuku. Upandishaji wa ngombe kwa njia ya sindano ulifanyika ili kupata mbegu bora ya ng ombe wa maziwa na nyama. Jumla ya ng'ombe 5,500 wamepandishwa Unguja na Pemba. Ng'ombe 1,874 waliangaliwa ushikaji wa mimba na ndama 547 wamewekewa kumbukumbu. Aidha, jumla ya wafugaji 21,793 wa ng'ombe, mbuzi, kuku na vikundi vya ushirika wametembelewa na kupewa ushauri juu ya ufugaji wa kisasa. Wafugaji 40 wamepewa mafunzo ya usindikaji wa mazao ya maziwa (jibini, siagi, samli na mtindi). Vilevile, 27

41 uzalishaji wa maziwa umeongezeka kutoka lita 24,343,351 (2010) hadi lita 27,243,351 () ikiwa ni sawa na asilimia 12, na uzalishaji wa mayai umeongezeka kutoka mayai 164,270,132 (2010) hadi mayai 186,870,292 () sawa na asilimia 14. Mashamba ya Wafugaji Waliopatiwa Taaluma ya Ufugaji Bora wa Kuku na Ng ombe Pia, Serikali inaendeleza utafiti wa kuchanganya damu za kuku wetu wa asili na kuku wa kigeni kwa kutumia kuku asili wa kabila la kishingo na kuku wa kigeni aina ya White Leghorns/Rhode Island Red/Australop. Matokeo ya utafiti huu umeonyesha kuwa kuku chotara anayezalishwa anataga mayai maradufu ya kuku wetu wa asili. Kuku hawa hutaga wastani wa mayai 200 kwa mwaka badala ya mayai 60 yanayozalishwa na kuku wetu wa asili. Katika suala la kushajiisha utunzaji wa mazingira na matumizi ya samadi katika jamii ya wafugaji, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imeweza kushajiisha wafugaji juu ya utumiaji wa samadi kama nishati mbadala kwa ujenzi wa mitambo ya Biogesi. Hadi sasa jumla ya mitambo 32 imejengwa Unguja na Pemba. 28

42 Ujenzi wa Mtambo wa Biogesi na Matumizi ya Nishati hiyo Serikali imeendelea kushajiisha Sekta binafsi kuwekeza katika Sekta ya mifugo na hadi hivi sasa wawekezaji wawili (2) wamejitokeza kuwekeza katika sekta hii. Mwekezaji mmoja (mzalendo) ameanzisha kiwanda cha maziwa Fumba na mwengine (mgeni) ameanzisha kiwanda cha kusarifu kuku Maruhubi Zanzibar. Viwanda hivi vinatoa fursa ya soko la bidhaa za maziwa na nyama ya kuku kwa wafugaji. 4.3 UVUVI NA MAZAO YA BAHARINI Sekta ya Uvuvi ni moja ya sekta inayochangia katika Pato la Taifa na kipato cha mtu mmoja mmoja kutokana na mazingira yetu kuwa ni visiwa na kuzungukwa na bahari pande zote. Kutokana na umuhimu huo, Serikali inaendeleza mikakati mbalimbali ya kusaidia wavuvi wadogo wadogo ili kuwawezesha kuwa na uvuvi wenye tija na kuhifadhi mazingira. Kwa kipindi cha miaka mitano iliyopita, Sekta ya Uvuvi imechangia katika Pato la Taifa kwa wastani wa asilimia 7.2. Jumla ya tani 148,535 za samaki zenye thamani ya Shilingi bilioni zilivuliwa kufikia mwaka Aidha, katika kipindi hicho, Serikali imewezesha kuundwa kwa vikundi vya uvuvi 167 na kupatiwa misaada ya boti, mashine pamoja na vifaa vyengine vya uvuvi. Vilevile, Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi imeendelea kutoa elimu kwa wavuvi wadogo wadogo na wananchi kwa ujumla juu ya uvuvi bora na utunzaji wa mazingira. 29

43 Serikali imesimamia Mpango Shirikishi wa Maeneo ya Hifadhi ya Baharini ikiwemo eneo la Menai, MIMCA na PECCA na imetoa mafunzo ya uvuvi wa Zanzibar na changamoto zake, usimamizi wa shughuli za doria, majukumu ya Kamati za Uvuvi za vijiji na utatuzi wa migogoro. Aidha, katika kuwajengea mazingira mazuri wananchi wetu ili waweze kushiriki katika uwekezaji wa uvuvi wa bahari kuu, Serikali imewasomesha wavuvi vijana 55 juu ya uvuvi wa bahari kuu katika Chuo cha Uvuvi cha Mbegani Tanzania Bara. Pia, Serikali inaendelea na kupambana na Uvuvi haramu na uharibifu wa mazao ya baharini kwa kufanya doria, ambapo jumla ya doria 127 zimefanywa. Katika mwaka jumla ya leseni 32,900 za wavuvi zimetolewa na vyombo 10,210 vimesajiliwa. Vilevile, shughuli za usimamizi shirikishi zimeanzishwa kwa kuanzisha Kitengo cha Kusimamia Maeneo yote ya Hifadhi za Baharini (MCU), ambapo pia vikundi 48 vya uhifadhi wa mazingira vimeanzishwa. Samaki wa aina ya Nduwari aliyevuliwa katika Bahari ya Nungwi akishushwa katika Soko la Darajani Uimarishaji wa Zao la Mwani Katika juhudi za kuimarisha zao la mwani, Serikali kwa kushirikiana na Taasisi za Sayansi ya Bahari (IMS) na Kampuni ya ununuzi wa mwani ya Birr imefanya utafiti juu ya mwani mnene wa cottonii utafiti ambao umetoa mafanikio mazuri kwa kuzalisha zaidi ya tani 64, Aidha, tani 60,433 zenye thamani ya Shilingi bilioni 24.7 zimesafirishwa na kuuzwa nje ya nchi kwa kipindi cha miaka mitano. Vilevile, jumla ya vikundi vya wakulima wa mwani 85 na wakulima binafsi 15 wamefaidika na Mpango wa Ugawaji wa Vihori vya kubebea mwani kwa Unguja na Pemba. Vihori hivyo vinaweza kubeba kilo 400 za mwani mbichi kwa mara moja. Mpango huu 30

44 ulitekelezwa na Serikali kwa mashirikiano na Shirika la Kujitolea la Canada baada ya utafiti mdogo uliofanywa kwa wakulima wa mwani na kugundua kuwa wakulima wa zao hilo wanatembea masafa marefu hadi kwenye mashamba yao na wanamudu kubebe kilo 50 hadi 100 za mwani mbichi kupeleka fukweni. Aidha, utafiti huo umeonyesha kuwa wakulima hawana uwezo wa kulima zao hilo katika maji ya kina kirefu ambapo maeneo hayo mwani humea vizuri zaidi kulinganisha na maji ya kina kifupi. Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mheshimiwa Dkt. Ali Mohamed Shein akikagua Vihori vya Kubebea Mwani Baada ya Kukabidhiwa na Shirika la Kujitolea la Canada katika Hoteli ya Bwawani Zanzibar 31

45 Wakulima wa Mwani Wakipanda, Wakivuna na Kuonyesha Njia Bora za Uanikaji wa Zao hilo Katika kuimarisha ufugaji wa viumbe wa baharini (samaki, kaa, chaza, lulu na majongoo) vikundi 144 vya ufugaji wa viumbe vya baharini vimeanzishwa na jumla ya wavuvi 2,320 wamepatiwa taaluma, vifaa na mbinu bora za uvuvi na ufugaji wa samaki unaozingatia hifadhi ya mazingira ya bahari. Pia, Serikali imeanzisha mabwawa matano (5) ya mfano ya kufugia samaki ambayo ni mashamba darasa Unguja na Pemba pamoja na kusaidia vifaa kama vile mashine za kuvutia maji katika mabwawa hayo. Vilevile, jumla ya vifaranga vya samaki 33,081 vimetolewa kwa wafugaji wa samaki Unguja na Pemba, kwa lengo la kuwasaidia kuinua uzalishaji wa samaki na kuwaongezea kipato wafugaji hao. Aidha, jumla ya wajasiriamali 59 wa mazao ya baharini walipelekwa nchini China kwa lengo la kujifunza teknolojia bora za ufugaji wa mazao ya baharini itakayowasaidia kuimarisha kazi zao za ufugaji wa samaki na mazao mengine ya baharini hapa nchini. 32

46 Shamba Darasa la Ufugaji Samaki Linalotumika Kuwafundishia Wakulima lililopo Pujini - Pemba Katika kuendeleza uhifadhi wa viumbe hai na adimu vya baharini mfano pomboo, kasa na nyangumi na kuvitumia kama vivutio vya utalii, Serikali imetoa mafunzo kwa wavuvi yanayohusu utengenezaji wa mitego ya jarife yenye uwezo wa kuwaachia viumbe hao pindipo wanaponasa. Aidha, utafiti wa majaribio umefanywa wa kuiwekea mitego ya jarife vifaa vyenye kutoa sauti (pingers) ili kuwatahadharisha pomboo wasinase katika mitego hiyo. Vilevile, Serikali imeendelea na kufuatilia uhifadhi wa wanyama adimu hasa kasa katika maeneo ya bahari yetu ya Zanzibar pamoja na maeneo yote ya hifadhi. Vikundi vipya viwili (2) vimeanzishwa na vinajihusisha na ufugaji wa kasa kwa ajili ya kuwahifadhi na kuwatumia kama kivutio cha utalii. Aidha, jumla ya kasa 130 waliohifadhiwa katika mabwawa huko Nungwi wameweza kuachiliwa kwa kurejeshwa baharini kwa lengo la kuongeza idadi na kuhifadhi aina ya viumbe hivi visipotee. 4.4 MALIASILI Kutekeleza Mpango wa Muda Mrefu wa Usimamizi wa Rasilimali za Misitu na Maliasili Zisizorejesheka Serikali kupitia Idara ya Misitu na Maliasili zisizorejesheka imeendelea na udhibiti wa maliasili zikiwemo rasilimali za misitu na maliasili zisizorejesheka pamoja na kulinda na kuhifadhi wanyama pori na bayoanuai zilizomo. Jumla ya miche 6,020,861 ikiwemo miti ya mikarafuu, misitu, matunda na viungo imesambazwa kwa ajili ya upandaji katika mashamba ya Serikali, barabarani, maeneo yaliyoathirika kwa uchimbaji wa mchanga na kwa wanajamii ambapo miche 33

47 358,263 imepandwa katika hekta 600 za mashamba ya Serikali. Aidha, miche 5,662,598 ya misitu imepandwa katika mashamba ya wakulima, pembezoni mwa barabara na maeneo yalimochimbwa mchanga. Vilevile, vikosi na maafisa misitu na maliasili wamekuwa wakifanya doria katika maeneo mbalimbali ya misitu aina ya mikoko Unguja na Pemba ambapo matukio ya ukataji wa mikoko yaliyowahi kugunduliwa ni pamoja na maeneo ya Pujini na Sizini na hatua za kisheria zimechukuliwa dhidi ya wahusika. Katika juhudi za kuhifadhi misitu, Serikali inaendelea na uandaaji wa Sera na Sheria za uhifadhi Misitu. Aidha, Serikali imeipandisha hadhi misitu ya Jambiani-Muyuni na Ufufuma-Pongwe yenye ukubwa wa hekta 405. Vilevile, Maeneo 12 ya uhifadhi wa Misitu ya Jamii yametayarishiwa mipango ya uhifadhi na kufanya idadi ya maeneo yote ya uhifadhi ya wanajamii kuongezeka kutoka 45 hadi 57 (Unguja 33 na Pemba 24). Pia, Serikali imeendelea kushirikiana na wananchi katika usimamizi na uhifadhi wa Maeneo Tengefu ya Jozani na Ngezi pamoja na Misitu ya asili ya Masingini na Msitu Mkuu wa Kiwengwa. Kazi hizi zinajumuisha kufanya doria za pamoja na wananchi, kuelimisha jamii/watendaji pamoja na kuanzisha miradi yenye faida za Kiuchumi na Mazingira. Eneo Tengefu la Msitu wa Hifadhi ya Jozani Mafanikio ya utekelezaji wa misitu ya jamii umetokana na kukamilika kwa Mradi wa Uhifadhi wa Misitu ya Asili (HIMA), Wananchi wengi wameelimishwa na kuhamasishwa katika matumizi endelevu ya maliasili. Aidha, Mipango 50 ya Usimamizi wa Misitu ya Jamii kwa Unguja na Pemba 34

48 imetayarishwa na kuanza kutumika. Katika juhudi za kupunguza matumizi ya kuni na mkaa, Serikali kwa kushirikiana na Washirika wa Maendeleo imewezesha Mpango wa kuzipatia kaya 4,500 gesi bila ya malipo. Pia, jumuiya 40 (15 Pemba na 25 Unguja) zimepatiwa jumla ya Shilingi 430,400,000 kwa ajili ya kuendeleza miradi ya maendeleo inayohusiana na utunzaji wa rasilimali zetu. Matokeo ya uwezeshaji huo yamepelekea kupunguza matumizi ya rasilimali misitu ambapo hivi sasa maeneo mbalimbali nchini ikiwemo watu binafsi na maeneo ya biashara wameanza kutumia gesi kwa matumizi ya nishati. Serikali imeandaa Kanuni ya Udhibiti wa Matumizi ya Misumeno ya Moto kudhibiti uingizaji na matumizi yake kwa lengo la kupunguza uharibifu wa misitu unaotokana na misumeno hiyo. Jumla ya wafanyakazi 21 wa Hifadhi ya Taifa ya Jozani na Ghuba ya Chwaka wamepatiwa mafunzo ya Zimamoto na Uokozi. Aidha, vifaa vya kuzimia moto vimenunuliwa na jumla ya visima 10 vimechimbwa katika maeneo tofauti ya Hifadhi ya Jozani ambavyo vinatarajiwa kutoa maji kwa ajili ya kazi ya uzimaji moto pale utakapotokea. Vilevile, kazi ya uwekaji wa mipaka ya kudumu na uchoraji wa ramani katika Msitu wa Jozani imekamilika. Katika juhudi za kuwahamasisha shughuli za ufugaji wa nyuki, Serikali imetoa jumla ya mizinga 3,000 kwa vikundi mbali mbali vya wafugaji wa nyuki. Hatua hii imepelekea ongezeko la uzalishaji wa asali na kufikia wastani wa tani tano za asali kila mwaka kuanzia Ufugaji wa Nyuki kisiwani Pemba chini ya Mradi wa CFP Pia, Serikali katika utekelezaji wa mkakati wa kuwaangamiza ndege aina ya Kunguru, imewaelimisha wanajamii 1,500 na wafanyakazi 27 wa Baraza la Manispaa na kuhamasishwa 35

49 kushiriki katika kazi ya kuangamiza ndege hao. Kutokana na juhudi hizo, jumla ya kunguru 200,736 wameuliwa kwa kutumia sumu na mitego Unguja na Pemba. Katika kuendeleza utunzaji na hifadhi ya wanyama pori walio katika hatari ya kutoweka hasa Kimapunju, Popo wa Pemba na Paa Nunga na kuwatumia kama vivutio vya utalii, Serikali imewezesha kuongezeka idadi ya wanyamapori hao adimu wakiwemo Popo wa Pemba kutoka 4,000 hadi 37,000 na Kima Punju kutoka 2,500 hadi 3,000. Juhudi hizi zimetokana na uanzishwaji wa maeneo ya uhifadhi na mazalio kwa wanyama hao. Wanyama adimu na kivutio kikubwa cha watalii ambao ni Kimapunju, Popo wa Pemba na Paa Nunga wanaopatikana katika Misitu ya Zanzibar 4.5 MAZINGIRA Kusimamia Utekelezaji wa Mpango wa Hifadhi ya Mazingira katika Maeneo ya Ardhi, Bahari na Ukanda wa Pwani Katika kusimamia utekelezaji wa Mpango wa Hifadhi ya Mazingira, Serikali imeandaa Sera ya Mazingira ya mwaka 2013 na Sheria ya Mazingira ya mwaka ambazo zinatoa muongozo na kuweka mfumo bora wa kisheria na kitaasisi juu ya usimamizi wa mazingira Zanzibar. Aidha, 36

50 Serikali imepiga marufuku matumizi ya mifuko ya plastiki kwa kuandaa Kanuni ambayo inakataza kuingiza, kutumia, kusafirisha na kuhifadhi mifuko ya aina zote ya plastiki hapa Zanzibar. Kanuni hii imetayarishwa kwa ajili ya kupunguza uchafuzi wa mazingira unaotokana na mifuko hiyo. Vilevile, Serikali imeandaa Kanuni ya usimamizi wa maliasili zisizorejesheka ili kupunguza wimbi la uchimbaji kiholela wa maliasili hizo. Serikali pia imeandaa Mpango wa Utekelezaji wa Usimamizi wa Mazingira wa Zanzibar ambao umeshaanza kutekelezwa. Aidha, vikosi kazi vimeundwa vya kufanya operesheni za kudhibiti uchimbaji kiholela wa maliasili zisizorejesheka na matumizi ya mifuko ya plastiki. Tokea kuanzishwa kwa vikosi kazi hivyo, mafanikio makubwa yamepatikana katika kudhibiti uchimbaji kiholela wa maliasili zisizorejesheka na uingizaji na utumiaji wa mifuko ya plastiki. Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abrahman Kinana akijumuika na wananchi wa kikundi cha kuhifadhi Mazingira Fuoni Kibondeni katika Upandaji wa Miti ya Mikoko Aidha, Serikali imefanya utafiti wa kuangalia athari za mabadiliko ya tabianchi kwa uchumi wa Zanzibar. Utafiti huo umebaini kuwa karibu sekta zote kuu za Uchumi wa Zanzibar kwa njia moja ama nyengine zinaathiriwa na mabadiliko ya tabianchi. Pia, utafiti umeorodhesha maeneo 148 yanayoingia maji ya Chumvi kwa Unguja na Pemba kutokana na kupanda kwa kina cha baharí kunakosababishwa na athari za mabadiliko ya tabianchi. Kutokana na hali hii, Serikali imeandaa taratibu maalum ili maeneo hayo yaendelee kutumika kwa shughuli mbalimbali za kilimo na nyenginezo. Vilevile, wananchi wa kijiji cha Nungwi wapatao 8,000 wamepatiwa maji safi na salama kupitia mradi wa kuhimili mabadiliko ya tabianchi. 37

51 Makamu wa Kwanza wa Rais Mheshimiwa Maalim Seif Sharif Hamad akiangalia Baadhi ya Maeneo yaliyoathirika na Matokeo ya Mabadiliko ya Tabianchi (Kilimani na Kinazini-Unguja) Kufanya Mapitio ya Miradi Inayohusiana na Mazingira Jumla ya Miradi 221 imefanyiwa ukaguzi kupitia Mamlaka ya Uwekezaji wa Vitega Uchumi Zanzibar (ZIPA). Pia, Miradi 71 ya uwekezaji imefanyiwa Tathmini ya Athari ya Kimazingira (EIA) na kutolewa vyeti vya Mazingira. Vilevile, ripoti 66 za maelezo yakinifu (Feasibility Study) za miradi mbalimbali zimewasilishwa Idara ya Mazingira kwa ajili ya kupatiwa ushauri wa kimazingira Kuwaelimisha Wananchi Juu ya Umuhimu wa Utunzaji na Hifadhi ya Mazingira. Katika kuelimisha jamii juu ya umuhimu wa utunzaji na hifadhi ya mazingira vipindi mbalimbali vya Radio na TV vinavyohusiana na usimamizi wa mazingira vimetayarishwa na kurushwa hewani. Aidha, Semina, Mikutano na Makongamano juu ya athari za mifuko ya plastiki na uchafuzi wa mazingira zimefanywa kwa Skuli za Msingi na Sekondari, Kamati za Shehia, Polisi Jamii, Waheshimiwa Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi, Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya na Madiwani nchini. 4.6 UTALII Kwa kutilia maanani kwamba Zanzibar ni visiwa vyenye vivutio vingi vya utalii kama vile fukwe zinazovutia, wanyama adimu kama popo, kima punju, paa nunga pamoja na urithi wa kimataifa wa mji mkongwe, Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka imetilia mkazo suala la utalii nchini. Katika kulitekeleza hili, Serikali imechukua hatua mbalimbali za kuimarisha sekta hii ili 38

52 kuongeza mchango wake katika Pato la Taifa na kuinua maisha ya wananchi. Miongoni mwa hatua zilizochukuliwa na zinazoendelea kuchukuliwa na Serikali ni kama zifuatazo Kusimamia utekelezaji wa Sera, Sheria na Mpango Mkuu wa Utalii Serikali imeweza kuimarisha shughuli za utalii kwa kufanya marekebisho ya Sheria ya Utalii yanayolenga kwa kiasi kikubwa kutekeleza Sera ya Utalii kwa Wote na kuanzisha awamu mpya ya uendeshaji wa utalii nchini. Aidha, Serikali imechukua hatua mahsusi kwa kuzishirikisha taasisi nyingine muhimu za kiuchumi ikiwemo Sekta Binafsi na taasisi mbalimbali za Serikali katika kuendeleza utalii. Vilevile, Serikali imeanzisha Programu ya Uendelezaji wa Sekta ya Utalii kwa kupitia Mpango wa Matokeo kwa Ustawi (Result for Prosperity) unaotokana na matokeo ya Maabara ya Utalii (Tourism Lab). Mpango huo unakisiwa kugharimu jumla ya Shilingi bilioni 5,595,375,000 na umeandaliwa kwa kuzihusisha taasisi mbalimbali za Serikali na Sekta Binafsi Kuitangaza Zanzibar Kiutalii Nje ya Nchi ili Kuongeza Kipato Serikali kupitia Kamisheni ya Utalii imeendelea kushiriki katika maonesho mbalimbali ya Kitaifa na Kimataifa kwa lengo la kuitangaza Zanzibar ili kuwavutia watalii wengi zaidi kutembelea nchi yetu. Katika jitihada za Serikali juu ya kuitangaza Zanzibar kiutalii, vyombo vya habari tofauti vya kitaifa na kimataifa vimeshirikishwa kwa lengo la kutoa taarifa za vivutio vya kiutalii vilivyopo Zanzibar. Taarifa hizo zimetolewa katika vyombo vya habari ikiwemo Magazeti na Majarida ya Masoko na mafanikio makubwa yamepatikana kwa kuongozeka kwa idadi ya watalii wanaotembelea Zanzibar kutoka 132,836 mwaka 2010 na kufikia watalii 310,500 mwaka 2014, hii ni sawa na ongezeko la asilimia

53 Katika kuendeleza utekelezaji wa mikakati ya kuitangaza Zanzibar kiutalii, Zanzibar imekuwa ikishiriki katika maonesho 10 ya kimataifa kila mwaka katika masoko ya zamani na mapya yakiwemo China na Urusi kwa lengo la kuwavutia watalii wengi zaidi kutembelea Zanzibar. Vilevile, Zanzibar imejiunga na Jumuiya ya Utalii wa Visiwa vya Vanila (Vanila Islands Tourism Association) ili kufaidika na fursa za kiutalii zilizopo katika jumuiya hiyo. Watendaji wa Kamisheni ya Utalii wakishiriki katika maonyesho ya Kimataifa ya Utalii ili kuitangaza Zanzibar Kuimarisha Utalii wa Kumbukumbu za Kihistoria Serikali imejikita zaidi katika kuyatangaza maeneo ya kihistoria yaliyopo Zanzibar na kutoa nafasi maalumu kwa kuyaimarisha makumbusho ikiwa ni pamoja na kuyapatia vifaa mbalimbali vya kihistoria na mambo ya kale ambavyo ni vivutio vya msingi kwa watalii. Aidha, katika kuendeleza utalii wa ndani, Serikali imeshajiisha ziara za wanafunzi na wananchi kutembelea maeneo ya kihistoria na pia wananchi wameshajiishwa kuanzisha matamasha ya kiutamaduni katika maeneo yao ili kuvutia watalii zaidi Kuibua Maeneo Mapya ya Vivutio vya Utalii Katika kuongeza vivutio vya utalii nchini, Serikali inaendelea kutafuta na kuibua maeneo mapya na kuyafanyia matengenezo maeneo ya kihistoria, Unguja na Pemba. Miongoni mwa maeneo mapya yaliyoibuliwa ni pamoja na Kuumbi, Kiwengwa, Muyuni, Dimani, Mwanampambe, 40

54 Mwana wa Mwana, Tazari na kijiji kilichozama Mkumbuu pamoja na maeneo ya uhifadhi wa wanyama. Aidha, katika kuyafanyia matengenezo maeneo ya kihistoria, Serikali imetekeleza Mradi wa Ukarabati wa Uhifadhi wa Maeneo ya Kihistoria wenye thamani ya Shilingi milioni 230. Mradi huu unajumuisha ukarabati, upimaji wa maeneo, ulipaji wa hati miliki, utangazaji, uwekaji mabango ya matangazo na kuonesha njia. Maeneo yanayohusika na mradi huo ni Mkama Ndume, Mkumbuu, Chwaka, Unguja Ukuu, Kizimkazi na Bikhole. Msikiti wa kihistoria wa Kizimkazi ambao ni kivutio kwa watalii Serikali imeendelea kuchukua juhudi za kuyafufua mashindano ya Trithlon kwa kushirikiana na Jumuiya ya Mashirika ya Ndege Duniani na wataalamu wa Trithlon kutoka Afrika ya Kusini na Ethiopia. Aidha, Serikali kwa kushirikiana na kampuni ya DISALVAMENTO kutoka Italia inaendelea na utaratibu wa kufufua mbio za Marathon. Pia, katika kuongeza kuwavutia watalii wengi wa hadhi ya juu kuja kutembelea Zanzibar na kuongeza Pato la Taifa, Serikali kwa kushirikiana na Hotel ya Manta Reef iliopo Makangale Pemba walizindua Chumba cha chini ya bahari ambapo watalii wengi wa hadhi ya juu wanategemewa kutembelea chumba hicho. 41

55 Makamu wa Pili wa Rais Mheshimiwa Balozi Seif Ali Iddi akikagua chumba cha chini ya baharí mara baada ya kukizindua rasmi, novemba Kumbukumbu na Mambo ya Kale Kwa azma ya kuendeleza kumbukumbu na mambo ya kale, Serikali imetekeleza mambo muhimu yafuatayo Kuhifadhi Kumbukumbu za Kihistoria na Mambo ya Kale Miongoni mwa hatua zilizochukuliwa na Serikali katika kuimarisha uhifadhi wa kumbukumbu na mambo ya kale, Serikali imefanya utafiti wa uchimbaji wa Ngome ya Mazrui, Chwaka na Tumbe uliofanyika kwa ufadhili wa MACEMP/DAMA pamoja na utafiti wa kiaikolojia katika eneo la Ngome Kongwe, Forodhani Unguja chini ya Udhamini wa African Archaelogy Network na DAMA. Katika uchimbaji huo kulingunduliwa vigae vya vyungu, Kwale pottery vya karne ya kwanza Kuendeleza Matengenezo ya Makumbusho Serikali imeyafanyia matengenezo majengo ya Mangapwani kwenye Mahandaki ya Vita Vikuu vya Pili vya Dunia, Magofu ya Kizimbani, Mahodhi ya Hamamni (Hamam Baths) pamoja na kusafisha kisima cha maji na mnara katika Chemba ya Watumwa Mangapwani ili kuyarejeshea hadhi yake ya awali kwa ajili ya kuwavutia wageni wengi zaidi kuitembelea Zanzibar. Aidha, Serikali imejenga jengo la Makumbusho ya Kuumbi Jambiani, Mkoa wa Kusini Unguja kwa lengo la kuhifadhi na kutunza kumbukumbu za mambo ya kale. 42

56 Makumbusho ya Kuumbi yaliopo Jambiani pamoja na baadhi ya vifaa vya kihistoria vilivyomo Unguja Kufanya Uhakiki wa Hoteli za Kitalii Serikali imefanya uhakiki wa hoteli za kitalii ili kuziwekea daraja zinazostahiki hoteli hizo. Matokeo ya uhakiki huo yameonesha kuwa hoteli 74 zilifikia vigezo vilivyowekwa na Jumuiya ya Afrika Mashariki. Kati ya hizo, hoteli za nyota tano ni 16, nyota nne tisa (9), nyota tatu 43 na nyota mbili sita (6). 43

57 Hoteli mbalimbali za Kitalii Zanzibar Kuimarisha Huduma za Utalii kwa Kuziendeleza Jumuiya za Watoa Huduma Katika hatua za kuimarisha huduma za utalii na kuziendeleza Jumuiya za Watoa Huduma, Serikali imeendelea kushajiisha Kampuni za Watembezaji na Wasafirishaji Watalii kuwa na wahudumu wenye taaluma na wenye kuithamini Sekta ya Utalii. Aidha, Wanajumuiya wamehamasishwa kushiriki katika Maonesho mbalimbali ya Kitalii ya Kitaifa na Kimataifa ili wawe na muamko mkubwa zaidi wa namna Sekta ya Utalii inavyokua na jinsi ya kuhudumia wageni ipasavyo. Vilevile, Serikali imeiongezea uwezo Jumuiya ya Watoa Huduma ili iweze kukabiliana na ushindani wa Jumuiya na Mashirika mbalimbali ya kimataifa. Pia, wadau wote wanaoshughulikia mambo ya utalii wamekutanishwa katika kutathmini hali halisi ya mwenendo na changamoto zinazoikabili Sekta ya Utalii ikiwemo masuala ya ulinzi na usalama wa watalii na mali zao na jinsi ya kuzipatia ufumbuzi changamoto hizo Kupunguza Vituo vya Ukaguzi Katika Maeneo Wanayopita Watalii Serikali imeendelea kuhakikisha upatikanaji wa huduma bora kwa watalii kwa kushirikiana na wadau wa Sekta hiyo wakiwemo Jumuiya za ZATI, ZATO, ZATOGA, pamoja na taasisi 44

58 zinazosimamia Sekta ya Utalii ikiwemo Jeshi la Polisi. Wadau hao wanakutana kila baada ya miezi mitatu kwa lengo la kuimarisha huduma za utalii nchini bila kuathiri taratibu za kiusalama Kukiimarisha Chuo cha Maendeleo ya Utalii Serikali imekiimarisha Chuo cha Maendeleo ya Utalii kwa ujenzi wa jengo la madarasa na ofisi za Chuo uliogharimu jumla ya Shilingi 800,000,000. Aidha, Serikali imewapatia mafunzo wakufunzi sita (6) wa Chuo hicho katika vyuo mbalimbali ndani na nje ya nchi. Vilevile, Chuo kimefanya makubaliano ya mashirikiano baina yake na Chuo cha Utalii Kenya (KUC) kwa ajili ya kubadilishana uzoefu na utaalamu. Pia, mitaala ya Chuo imefanyiwa mapitio kwa mashirikiano na taasisi ya Programma Uitzending Managers ya Netherland. Chuo kinatekeleza Mradi wa Vocational Education for Higher Categories and Level (VEHICLE) ambao umesaidia Chuo kujitangaza kibiashara na kujenga mahusiano mazuri na wadau wengine wa utalii. Jengo jipya la Chuo cha Maendeleo ya Utalii Zanzibar kilichopo Maruhubi 4.7 VIWANDA NA BIASHARA Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi ya imeiagiza SMZ kusimamia utekelezaji wa Sera ya Uendelezaji wa Viwanda Vidogo vidogo na vya Kati na kuifanyia mapitio Sera ya Biashara ya Mwaka 2006 ili kubaini mapungufu na kuchukua hatua zinazopaswa pamoja na kuweka mfumo bora zaidi katika utoaji wa leseni. Katika kulitekeleza hilo, Serikali inasimamia kikamilifu utekelezaji wa Sera ya Uendelezaji wa Viwanda Vidogo Vidogo na vya Kati. Pia, Serikali imeunda Kamati ya Ushauri yenye wajumbe 12 (wajumbe 6 kutoka Sekta ya Umma na 45

59 wajumbe 6 kutoka Sekta Binafsi) ili kuishauri juu ya utambuzi na utatuzi wa changamoto zinazoikabili Sekta ya Viwanda. Kutokana na mazingira mazuri ya uwekezaji yaliyowekwa na Serikali, Kampuni ya Azam imeweza kuanzisha Kiwanda cha Maziwa (Azam Diary Factory) katika eneo la Fumba na kinatarajiwa kuajiri zaidi ya watu 200. Hivi sasa Kiwanda kimeshaanza rasmi uzalishaji na usambazaji wa maziwa. Kiwanda cha Maziwa cha Azam kilichopo katika Maeneo Huru ya Uwekezaji - Fumba Vilevile, ukarabati mkubwa umefanyika katika Kiwanda cha Sukari Mahonda kwa kuweka mashine mpya na kuimarisha mashamba ya miwa. Kiwanda kimeajiri wafanyakazi 350 na kazi ya uzalishaji inaendelea na tayari sukari inayozalishwa katika Kiwanda hicho iko sokoni. Kiwanda cha Sukari Mahonda na bidhaa ya sukari iliyozalishwa kiwandani hapo 46

60 Kwa upande wa biashara, Serikali inaendelea na hatua za kuifanyia mapitio Sera ya Biashara ya Mwaka 2006 kwa lengo la kubaini mapungufu na kuchukua hatua zinazofaa zitakazoimarisha shughuli za biashara nchini. Pia, Serikali imetunga Sheria ya Utoaji Leseni za Biashara na Usajili Nam.13 ya mwaka 2013 ambayo tayari inatumika. Sheria hii inaweka mfumo bora zaidi wa utoaji wa leseni za biashara nchini. Aidha, Serikali imezifanyia mapitio Sheria Namba.2 ya Kusimamia Mwenendo wa Biashara na Kumlinda Mlaji ya mwaka 1995, Sheria Nam.4 ya Mizani na Vipimo ya mwaka 1983 na Sheria Nam.4 ya Biashara ya mwaka 1989 na kutunga Sheria mpya Nam.14 ya Biashara ya Zanzibar ya Sheria hizi zimetungwa kwa lengo la kukidhi mazingira ya sasa ya biashara ikiwemo uendeshaji uchumi na biashara kwa kuzingatia misingi ya nguvu za soko, maendeleo ya teknolojia na kuzigeuza sheria kuwa rafiki wa kukuza uchumi na ustawi wa biashara. Serikali pia imeanzisha Taasisi ya Viwango ya Zanzibar (ZBS) kwa mujibu wa Sheria ya Viwango Namba. 1 ya 2011 kwa lengo la kusimamia biashara nchini kwa kuzingatia viwango vya bidhaa vinavyohitajika. Aidha, Kamati 10 za kitaalamu zimeundwa kwa ajili ya kuzingatia mapendekezo ya viwango vya bidhaa. Kamati hizo zina jukumu la kuainisha viwango vya kipaumbele katika bidhaa za vyakula na vinywaji, mafuta ya mimea na viungo, umeme na eletroniki, nishati na gesi, sabuni, vifaa vya ujenzi na mazingira. Vilevile, Serikali imezingatia na kupitisha jumla ya viwango 25 vya bidhaa mbalimbali na kutoa taaluma ya viwango na ubora wa bidhaa kupitia maonesho ya biashara, vipindi vya redio na TV, ziara kwa wajasiramali na wazalishaji pamoja na kuandaa taratibu za upimaji na udhibiti wa ubora wa bidhaa. Serikali kupitia ZBS imetengeneza alama ya utambulisho (logo) na alama ya ubora wa bidhaa (Standard Mark) ambayo itaonesha ubora wa bidhaa hizo. Katika kuwajengea uwezo wazalishaji na wajasiriamali ili waweze kuzalisha bidhaa bora zaidi na kwa kiwango cha juu, Serikali imetoa mafunzo kwa wazalishaji wadogo wadogo 285 Unguja na Pemba juu ya usindikaji mazao, ujasiriamali, kuongeza thamani ya mazao na mbinu bora za kuendesha biashara. Kwa upande wa masoko, Serikali imefanya jitihada za kuitangaza Zanzibar na kuwatafutia masoko wafanyabiashara, wajasiriamali na wazalishaji wa bidhaa mbalimbali ili waweze kutumia fursa za masoko ya EAC, SADC, AGOA na EU. Aidha, Serikali inaendelea na kutayarisha michoro ya ujenzi wa Uwanja wa Maonesho ya Biashara ya Kimataifa unaotarajiwa kujengwa 47

61 katika eneo la Dimani. Aidha, Serikali kupitia Wizara ya Biashara, Viwanda na Masoko imeratibu ushiriki wa wajasiriamali na wafanyabiashara 500 kushiriki katika maonesho ya biashara mbalimbali ya Kitaifa, Kikanda na Kimataifa ili kutangaza na kuuza bidhaa zao Kuimarisha Mtandao wa Usambazaji Habari za Biashara kwa Wafanyabiashara Serikali imeunda Kitengo cha Habari na Mawasiliano ili kiweze kusambaza taarifa mbalimbali za biashara kwa wafanyabiashara na wadau wengine. Kitengo hicho kinakusanya taarifa kumbukumbu mbalimbali zinazohusiana na biashara, uendelezaji wa viwanda na masoko zikiwemo tafiti, sera, hotuba za bajeti na picha za matukio kwa ajili ya Maktaba ya Wizara ili wadau wanaozihitaji waweze kuzipata. Aidha, Serikali imetayarisha taarifa za maendeleo ya biashara kwa kipindi cha miaka 50 ya Mapinduzi ya Zanzibar na kusambaza kwa wadau. Vilevile, Serikali imezindua Mpango wa Elimu kwa wananchi kuhusu Sheria Mpya ya Biashara Nam.14 ya Kufanya Utafiti wa Usarifu wa Zao la Karafuu Serikali kupitia Shirika la Taifa la Biashara (ZSTC) imeanza kuchukua hatua za kuilinda na kuipa hadhi zaidi karafuu ya Zanzibar pamoja na kuitangaza Zanzibar ulimwenguni kupitia bidhaa nyengine za viungo zikiwemo Mdalasini, Pilipili Hoho na Pilipili Manga. Kazi hii inatekelezwa kupitia mradi wa Tasnia Malibunifu (Branding). Aidha, Serikali kupitia Shirika la ZSTC imeanzisha Kituo Maalum (Eneo Tengefu) katika eneo la Saateni kwa ajili ya utekelezaji wa Mradi huu pamoja na kutoa mafunzo maalum kwa wakulima 50 Unguja na Pemba wa mazao hayo ili kuwatayarisha na kuwajengea uwezo. Serikali kupitia Wizara ya Biashara Viwanda na Masoko imesajili Jina la Biashara (Trade Mark) ambalo litatumika kwa ajili ya Mradi huu ambalo ni Zanzibar Exotic Original. Aidha, Serikali imetayarisha kitabu maalum kwa lengo la kuelezea historia ya zao la karafuu, jinsi ilivyoingia Zanzibar na utamaduni wa Zanzibar katika matumizi ya zao hilo. na 48

62 Bidhaa mbalimbali zitokanazo na zao la karafuu zinazouzwa ndani na nje ya nchi Pia, Serikali imeingia makubaliano ya kibiashara na Kampuni ya Land Co. ya Japan ambapo Kampuni hiyo inasaidia uimarishaji wa bidhaa za mafuta ya mimea ikiwemo karafuu ili yaweze kuuzwa katika soko la Japan. 4.8 VYAMA VYA USHIRIKA Serikali imetathmini na kuziwekea madaraja ya ubora SACCOS 203 zilizopo nchini. Aidha, matokeo ya tathmini hiyo yameonesha kuwa mitaji ya Shilingi bilioni 3.5 imechangwa na wananchi na mikopo ya Shilingi bilioni 7 imetolewa na SACCOS hizo. Aidha, Serikali imeziunganisha SACCOS 17 na Taasisi za kifedha na kupata mikopo ya thamani ya Shilingi bilioni 3. Hatua hii imesaidia kuongeza utoaji wa mikopo kwa wanachama na kuimarisha biashara zao. 49

63 Kikwajuni SACCOS Benki iliyopo katika Jimbo la Kikwajuni Katika kuendeleza Vyama vya Ushirika, Serikali imetoa mafunzo juu ya ushindani, ubunifu na ujasiriamali kwa washiriki 73 kutoka vyama vikuu vya mikoa mitano ya Zanzibar na Muungano wa Vyama vya Ushirika Zanzibar (CUZA). Aidha, Serikali imetoa mafunzo ya ubunifu, haki na wajibu kwa Vyama vya Ushirika 79 vilivowashirikisha wanachama 697 (wanawake 459 na wanaume 238) wa Vyama vya Ushirika kutoka Wilaya zote za Unguja na Pemba. Kati ya vyama hivyo, SACCOS ni 28 na vyama vya uzalishaji 51. Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mheshimiwa Dkt. Ali Mohamed Shein akikagua Kazi na Bidhaa za Wajasiriamali na SACCOS Vilivyoshiriki Maonesho Mbalimbali ya Biashara 50

64 Katika hatua za utunzaji wa rasilimali na hesabu za ushirika, Serikali imefanya ukaguzi wa hesabu za Vyama vya Ushirika 200 (Unguja 139 na Pemba 61) zikiwemo SACCOS 49 na vyama vya ushirika vya uzalishaji mali na utoaji huduma 151. Pia, Serikali imefanya upekuzi na kutoa mafunzo ya vitendo kwa Vyama vya Ushirika 1,222 ili kuimarisha utendaji wao Kusimamia Utekelezaji wa Sheria ya Vyama vya Ushirika na Program Mbalimbali Katika kusimamia utekelezaji wa Sheria ya Vyama vya Ushirika na Programu mbalimbali, Serikali imevifanyia ukaguzi wa kawaida vyama 2,243 ili kutathmini hali ya uendeshaji, utekelezaji wa sheria, uandishi na utunzaji wa vitabu vya hesabu. Pia, Vyama vya Ushirika 485 vimefanyiwa ukaguzi wa hesabu na ripoti kuwasilishwa kwenye Mikutano Mikuu ya vyama hivyo kwa kutolewa maamuzi. Matokeo ya kaguzi hizo yameonesha Vyama vya Ushirika vinaimarika na vinaendeshwa kwa kuzingatia Sera na Sheria ya Vyama vya Ushirika Namba. 4 ya mwaka Serikali pia, imekamilisha Sera ya Maendeleo ya Ushirika Zanzibar na inaendelea kufanya mapitio ya Sheria ya Ushirika, ili iendane na malengo ya Sera na mahitaji yaliyopo sasa Kuendelea Kusajili na Kufanya Ukaguzi wa Vyama Vipya vya Ushirika Serikali imesimamia usajili wa Vyama vya Ushirika 826 vya aina mbalimbali. Kati ya hivyo Vyama vya Kuweka na Kukopa (SACCOS) 16 na Vyama vya Uzalishaji Mali na Utoaji Huduma ni 770. Idadi ya Vyama vya Ushirika imeongezeka na kufikia vyama 2,493 vilivyo hai na ambavyo vimeweza kuwajumuisha wananchi 39,664 katika harakati za kiuchumi. SEHEMU YA TANO 51

65 5.0 MIUNDOMBINU YA KIUCHUMI Miundombinu ya kiuchumi inajumuisha barabara, viwanja vya ndege, usafiri wa baharini, umeme na bandari. Chama cha Mapinduzi kupitia Ilani yake ya Uchaguzi ya mwaka imeelekeza Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kutoa kipaumbele katika kuendeleza sekta hii muhimu. 5.1 BARABARA Serikali inaendelea na ujenzi wa Barabara za Unguja na Pemba ili ziendelee kupitika kwa wakati wote na kuwarahisishia wananchi usafiri. Katika utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ( ), Serikali imejenga na kuzifanyia matengenezo barabara mbalimbali zenye jumla ya Kilomita kwa Unguja na Pemba kwa kiwango cha lami. Kwa Unguja barabara hizo ni:- i. Mfenesini - Bumbwini (Km. 13) ii. Welezo - Dunga (Km ) iii. Amani - Mtoni (Km. 4) iv. Mahonda - Donge (Km. 14) v. Njia nne Umbuji (Km. 5) Aidha, Serikali kupitia msaada wa Watu wa Marekani (MCC) imejenga barabara tano (5) za vijijini katika Mkoa wa Kaskazini Pemba zenye urefu wa kilomita Barabara hizo ni:- i. Bahanasa Daya Mtambwe (Km. 13.6) ii. Mzambarau Takao Pandani Finya (Km. 8) iii. Mzambarau Karim Mapofu (Km. 8.9) iv. Chwale Kojani (Km. 2) v. Kipangani Kangagani(Km. 3) 52

66 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein akiwa pamoja na Balozi Mdogo wa Marekani wakati wa ufunguzi wa Barabara tano za vijijini zilizojengwa kwa Msaada wa MCC Mkoa wa Kaskazini-Pemba. Pia, Serikali kwa kushirikiana na Benki ya Kiarabu kwa Maendeleo ya Africa (BADEA) na Mfuko wa Maendeleo wa Saudi Arabia (Saud Fund) imekamilisha ujenzi wa barabara tatu (3) Pemba zenye urefu wa kilomita 54. Barabara hizo ni:- i. Wete Konde (Km. 15). ii. Wete Gando (Km. 15). iii. Chake chake Wete (Km 24). Baadhi ya Barabara zilizokamilika kujengwa, Pemba 53

67 Aidha, Serikali imekamilisha ujenzi wa barabara zenye urefu wa kilomita 43.4 Pemba kwa kiwango cha lami. :-Barabara hizo ni:- iv. Mtambile Kengeja Mwambe (Km. 9) v. Kenya Chambani (Km. 3.2) vi. Mizingani Wambaa (Km. 10) vii. Chanjamjawiri Tundaua (Km. 10) viii. Chanjaani Pujini (Km. 5) ix. Mtambile Kangani (Km. 6.2) Baadhi ya Barabara zilizojengwa na Kufanyiwa Matengenezo kwa Unguja na Pemba Pia, barabara saba (7) zenye ukubwa wa kilomita 36.5 zimejengwa kwa kiwango cha kifusi kwa Unguja na Pemba. Barabara hizo ni:- i. Fukuchani Kigongoni (Km. 8) ii. Utambi - Tazari(Km. 0.8) iii. Boshoa Kilimani (Km. 4) iv. Donge Mtambile Mwanda (Km. 3.8) v. Mgagadu Kiwani (Km. 7.5) vi. Shumba Viamboni Tumbe (Km. 5) 54

68 vii. Kiyuni Ngomeni (Km. 4) Aidha, Serikali inaendelea na hatua za ujenzi wa barabara tatu (3) za Unguja zenye jumla ya kilomita Barabara hizo ni:- i. Mkwajuni Kijini (Km. 9.5). ii. Jendele Cheju Kaibona (Km. 11.6). iii. Jumbi Koani (Km. 6.4). Vilevile, Serikali inaendelea na ujenzi wa barabara ya Ole-Kengeja Pemba yenye urefu wa kilomita 35 kwa Mkopo wa riba nafuu wa Dola za Kimarekani 11,000,000 kutoka Benki ya OFID Kusimamia Utekelezaji wa Sheria Zinazohusiana na Usalama Barabarani Serikali imeendelea kuimarisha usalama barabarani kwa kuwapatia elimu watumiaji wa barabara na kutunga Sheria ya Barabara Road Act pamoja na kuweka kanuni zake ili kupunguza ajali. Pia, Kanuni ya adhabu za papo kwa papo imetengenezwa na kuanza kutumika. Aidha, Serikali imeandaa Sheria ya Vyombo vya Usafiri ya mwaka 2014 pamoja na miongozo ya kusimamia matumizi ya vyombo vya usafiri. 5.2 USAFIRI WA BAHARINI Katika kuimarisha Shirika la Bandari, Serikali kwa kushirikiana na Kampuni binafsi ya AZAM MARINE imeiimarisha Bandari ya Malindi kwa kujenga majengo ya kuhudumia abiria ikiwemo jengo la Watu Mashuhuri (VIP), Ofisi ya Uhamiaji, Ofisi ya afya na Ofisi ya ushuru wa bandari pamoja na kuimarisha huduma nyengine za abiria. 55

69 Rais wa Zanzibar Dkt. Ali Mohamed Shein akifungua na kukagua jengo jipya la abiria katika bandari ya Malindi -Zanzibar Serikali imelifanyia matengenezo eneo la kuhifadhia makontena bandarini lenye ukubwa wa mita za mraba 6,000. Pia, Serikali imenunua vifaa vitatu vipya vya kunyanyulia mizigo bandarini ambavyo ni Reach Staker moja yenye uzito wa tani 45, Fort lift Compty Handle yenye uzito wa tani saba (7) na Fork lift yenye uzito wa tani tano (5) ili kuongeza ufanisi katika huduma za bandari. Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mheshimiwa Balozi Seif Ali Iddi akikagua utendaji kazi Bandarini-Zanzibar 56

70 Miongoni mwa vifaa vya kuinulia mizigo kikitoa huduma hiyo katika bandari ya Malindi Vilevile, Serikali imekamilisha matengenezo makubwa ya gati ya Mkoani Pemba na kuondoa tatizo la kutuama kwa maji juu ya gati, pamoja na kukamilisha matengenezo ya kiungo cha gati hiyo ambacho kiliathirika kutokana na nguvu za mawimbi ya bahari. 57 Gati ya Mkoani Pemba inayoendelea kufanyiwa matengenezo

71 5.2.1 Ujenzi wa Bandari ya Mpigaduri Ilani ya uchaguzi ya CCM ya 2010 imeiagiza Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kuendelea na mkakati wa ujenzi wa Bandari mpya ya Mpigaduri. Katika kulitekeleza agizo hili, Serikali tayari imeshatiliana saini Hati ya Makubalinao (MoU) na Kampuni ya China Habour Engineering (CHEC) ya China kwa ajili ya kufanya upembuzi yakinifu na uchunguzi wa kimazingira kwa Mradi wa Ujenzi wa Bandari hiyo kwa Awamu ya Kwanza. Mapendekezo ya upembuzi yakinifu huo ni kujenga bandari yenye urefu wa mita 300 na upana wa mita 490 itakayo hudumia meli zenye uzito wa 50,000DWT na makontena yenye uzito wa 200,000 TEU na mizigo ya mchanganyiko yenye uzito wa tani 300,000 kwa mwaka. Aidha, Serikali tayari imetiliana saini mikaba ya ujenzi wa Bandari ya Mpigaduri baina yake na Kampuni hiyo ya Kichina na maombi ya mkopo kwa ajili ya ujenzi wa bandari hiyo tayari yamewasilishwa Benki ya Exim ya China. Kukamilika kwa ujenzi wa Bandari hiyo kutaongeza uwezo wa bandari yetu kuhudumia mizigo mingi na meli kubwa zaidi na kwa kiasi kikubwa itaondosha tatizo lilopo sasa la msongamano wa mizigo katika bandari ya Malindi pamoja na kuongeza Pato la Taifa. 5.3 Kuliimarisha Shirika la Meli Katika kuliimarisha Shirika la Meli na kuwapatia wananchi usafiri wa uhakika, Serikali imetunga Sheria Namba. 3 ya mwaka 2013 kwa madhumuni ya kulianzisha upya Shirika hilo. Mpango wa Mageuzi wa Kimuundo na Uendeshaji wa Shirika umeandaliwa ambao pia umehusisha Mpango Mkakati wa Shirika tayari umeridhiwa na Serikali. Aidha, Serikali kupitia Shirika la Meli imezifanyia matengenezo makubwa meli zake mbili (2) MV. Maendeleo na MV. Ukombozi ili kuendelea kutoa huduma bora zaidi za usafiri baharini Ununuzi wa Meli Mpya ya Serikali Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imeamua kununua meli mpya ili kupunguza tatizo la usafiri wa baharini kati ya visiwa vya Unguja na Pemba na maeneo mengine ya mwambao wa Afrika Mashariki jambo ambalo limeleta usumbufu kwa wananchi wetu kwa muda mrefu. Katika utekelezaji wa maamuzi haya mwezi wa Julai 2013, Serikali ilitiliana saini Mkataba na Kampuni 58

72 ya DAEWOO International ya Korea Kusini kwa ajili ya ujenzi wa meli mpya ya abiria na mizigo. Meli hiyo itakuwa na uwezo wa kubeba abiria 1,200 na mizigo yenye uzito wa tani 200. Ujenzi wa meli hiyo tayari umekamilika na mwezi Machi ilishushwa rasmi baharini kwa majaribio (sea trials) ambayo yameanza kufanyika mwishoni mwa mwezi Juni na meli hiyo tayari iko safarini kuja Zanzibar na inatarajiwa kuwasili mwishoni mwa mwezi wa Julai Kubadili Mfumo wa Uendeshaji wa Ofisi ya Mrajis wa Meli na kuwa Mamlaka ya Usimamizi wa Usafiri wa Baharini Serikali imebadilisha mfumo wa uendeshaji wa Ofisi ya Mrajis wa Meli kwa kuanzisha Mamlaka ya Usafiri wa Baharini ijulikanayo kama Zanzibar Maritime Authority (ZMA). Mamlaka hii imeimarisha ukaguzi wa vyombo vya baharini kwa kushirikiana na SUMATRA, hatua ambayo imepelekea kupungua kwa ajali za vyombo vya baharini kwa kiasi kikubwa Kuendeleza Mazingira ya Kuvutia Wawekezaji wa Nje na Ndani ili Kuekeza zaidi katika Usafiri wa Baharini Serikali kupitia Shirika la Meli imezidi kutoa ushirikiano na kushajiisha wawekezaji wa ndani na nje kuendelea kuwekeza katika Sekta ya Usafari wa Baharini ambapo jumla ya Kampuni 23 zimewekeza katika usafiri wa baharini. Aidha, kazi za uimarishaji wa miundombinu na huduma mbalimbali za bandari pamoja na kuandaa taratibu za matumizi bora ya bandari zinaendelea. Boti ya Kilimanjaro III inayomilikiwa na Kampuni ya Azam Marine 59

73 5.4 USAFIRI WA ANGA Kuwajengea Uwezo Wafanyakazi Serikali imewapatia mafunzo wafanyakazi wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege katika fani za Basic Airport Operation Course katika chuo cha CATC DSM, mafunzo ya kutangaza kwa kutumia mtambo wa kutolea matangazo na mafunzo ya customer care training katika chuo cha Diplomasia Dar-es-Salaam Kusimamia Utekelezaji wa Mpango Mkuu wa Uendeshaji wa Kiwanja cha Kimataifa cha Zanzibar Katika utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka kuhusu kusimamia Mpango Mkuu wa Uendeshaji wa Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Abeid Amani Karume na ujenzi wa jengo jipya la abira, Serikali imekamilisha uundaji wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Zanzibar na kuipa jukumu la kusimamia na kuendesha viwanja vya ndege vilivyopo Zanzibar. Aidha, Serikali imekamilisha ujenzi wa eneo la kuegesha magari na njia za kuingilia zenye ukubwa wa mita za mraba 15, Uendelezaji Ujenzi wa Uzio na Jengo Jipya la Abiria Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume Katika kuimarisha huduma za Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Abeid Amani Karume, Serikali imeendelea na kazi ya kujenga uzio wenye urefu wa kilomita 11.9 katika kiwanja hicho. Aidha, Serikali inaendelea na ujenzi wa jengo jipya la abiria lenye ukubwa wa mita za mraba 25,000. Jengo hilo litakuwa na uwezo wa kuhudumia abiria 1,600,000 kwa mwaka. Serikali inaendelea kufanya marekebisho na kuongeza eneo la kuegeshea ndege lenye ukubwa wa mita za mraba 37,000. Marekebisho hayo yatabadilisha mfumo wa uegeshaji wa ndege kubwa kutoka mbele ya jengo (airside) na badala yake kuegesha upande wa kusini ya jengo. 60

74 Ujenzi unaoendelea wa jengo la abiria la Terminal II na mchoro wa hali ya jengo hilo litakavyoonekana baad ya ujenzi kukamilika Ujenzi wa Maegesho na Njia ya Kupitia Ndege Uwanja wa Ndege wa Kimataifa Serikali imefanya marekebisho makubwa ya sehemu ya maegesho ya ndege (apron) kwa kujenga eneo jipya la maegesho (apron) lenye ukubwa wa mita za mraba 48,000 pamoja na kuzitanua njia za kupitia ndege (taxiways) kutoka mita 1,800 hadi kufikia mita 3,400 katika Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Abeid Amani Karume. Matengenezo yaliyofanyika yamepelekea kiwanja hicho kuwa na uwezo wa kuchukua aina zote za ndege. Aidha, eneo la maegesho ya ndege lina uwezo wa kuchukua ndege kubwa mbili (2) na ndogo moja (1) kwa wakati mmoja na uimara wa run way umefikia PCN 61 kutoka PCN 42. Ndege mbalimbali zikiwa katika eneo la Maegesho ya Ndege katika Uwanja wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume -Zanzibar 61

75 Kukamilisha Kazi za Ujenzi wa Kiwanja cha Ndege Pemba Serikali imeimarisha Uwanja wa Ndege wa Pemba kwa kufanya ukarabati wa jengo la abiria, kuongeza urefu wa njia ya kutulia na kurukia ndege kutoka mita 1,500 hadi 2,300, uwekaji wa taa, uzio katika barabara ya kurukia na kutulia ndege na kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa huduma mbalimbali katika kiwanja hicho. Rasimu ya Upembuzi yakinifu wa kifedha na kimazingira imekamilika na sasa Serikali ipo katika hatua za manunuzi ili Wakandarasi waweze kukamilisha kazi hiyo. Uwanja wa Ndege wa Karume - Pemba 5.5 UMEME Nishati ya Umeme ni muhimu katika kujenga msingi wa uchumi wa kisasa wa Taifa linalojitegemea. Lengo kuu la Serikali ni kuendeleza mpango wa upatikanaji wa umeme mbadala ambapo hatua ya matayarisho kwa uchambuzi yakinifu wa kuzalisha umeme mbadala tayari yameanza. Serikali imesimamia kikamilifu utekelezaji wa Mradi wa Kujenga Njia ya Pili ya Umeme inayopita chini ya bahari kutoka Ras Kiromoni Tanzania Bara hadi Fumba Unguja kupitia mradi wa MCC. Kukamilika kwa mradi huu kumeiwezesha Serikali kupata mafanikio makubwa kwa kuongezeka kwa kiwango cha umeme hadi kufikia Megawatt 100 kwa Unguja. Kwa upande wa Pemba, Serikali imejenga njia ya umeme ya Megawati 20 inayopita chini ya bahari kutoka Tanga hadi kisiwani Pemba kupitia mradi wa NORAD na kukiwezesha kisiwa cha Pemba kupata umeme wa uhakika kutoka katika gridi ya Taifa. 62

76 Rais wa Zanzibar Dkt Ali Mohamed Shein akikagua Kituo cha Umeme Mtoni Kazi ya Kulaza Nyaya za Umeme kutoka Tanga kwenda Pemba 63

77 Katika kuimarisha na kuendeleza mipango ya usambazaji wa huduma ya umeme kwa wananchi wa mijini na vijijini, Serikali imeimarisha njia na miundombinu ya umeme kwa ujenzi wa njia za kusambaza umeme kuanzia Mtoni-Tunguu, Mtoni-Fumba na Mtoni-Mahonda kwa lengo la kuimarisha upatikanaji wa umeme katika maeneo hayo. Aidha, Serikali imejenga vituo vya kusambaza umeme katika maeneo ya Mtoni, Welezo na Mwanyanya ili kurahisisha upatikanaji wa umeme kwa wananchi. Mradi huu umefadhiliwa na Serikali ya Japan kwa kushirikiana na SMZ na umegharimu Shilingi Bilioni 55. Pia, Serikali imejenga laini kubwa ya Umeme (H/T) yenye urefu wa kilomita 5.2 katika vijiji vya Kibonde Maji na Pongwe kwa Unguja na vijiji vya Kivugo na Kichuwani kwa Pemba. Aidha, vijiji 129 badala ya 123 vilivyokusudiwa awali vimefikishiwa huduma za umeme Unguja na Pemba. Sambamba na hayo Serikali inaendelea na jitihada zake za kuyapatia nishati ya umeme maeneo ya Kisiwa cha Makongwe, Kisiwa Panza na Kisiwa cha Shamiani Pemba. Katika kuendeleza juhudi za utafiti wa vyanzo vya nishati ya umeme mbadala ukiwemo umeme wa jua, mawimbi ya bahari, upepo na gesi asilia, Serikali imeyakagua upya na kuyafanyia uhakiki maeneo yote ambayo yalifanyiwa utafiti wa awali na kupendekezwa na wataalamu kutoka EU ili kutumika kwa ajili ya nishati mbadala kabla ya kuanza hatua ya utekelezaji. Rais wa Zanzibar Dkt. Ali Mohamed Shein akiwa katika Picha ya Pamoja baada ya Ufunguzi wa Umeme katika Kijiji cha Ukunjwi 64

78 5.5.1 Kuimarisha Mazingira ya Kuvutia Wawekezaji katika Sekta ya Nishati ya Umeme Serikali inaendelea kuweka mazingira mazuri ya kuvutia wawekezaji kwa kufanya utafiti yakinifu katika nyanja za umeme mbadala wa upepo, jua na takataka ili kuwapa wepesi wawekezaji kuja kuekeza. Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imetiliana saini na Kampuni ya Italia ambayo itafunga minara itakayotumika kufanyia tafiti hizo kwa kupitia ufadhili wa Umoja wa Ulaya (EU). Vilevile, Serikali kupitia Shirika la Umeme imetayarisha Customer charter ambayo inatarajiwa kuwasilishwa kwa wananchi na wawekezaji wote Kuwapatia Mafunzo Wafanyakazi katika Fani za Nishati na Madini Serikali imeendelea na juhudi za kuwapata wataalamu wa mafuta na gesi. Jumla ya vijana 30 wanaendelea na mafunzo ya fani hizo kupitia vyuo mbalimbali vya ndani na nje ya nchi. Vilevile, Serikali kwa kushirikiana na Kampuni ya RAKGAS imedhamini mafunzo kwa vijana wawili (2) katika fani ya uhandisi wa mafuta na gesi, kati ya hao mmoja (1) ameshamaliza masomo yake katika Shahada ya Pili na mmoja (1) anaendelea na Shahada ya Kwanza Kuliimarisha Shirika la Umeme Zanzibar (ZECO) Serikali inaendelea kulisaidia Shirika la Umeme ili kuweza kujiendesha kibiashara kutekeleza miradi ambayo ni muhimu sana kwa Shirika hilo, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Serikali ya Sweden wametiliana saini kuhusu ZECO kupatiwa msaada wa kubadilisha mita zote za kawaida Post paid na kufungwa mita za TUKUZA Pre-paid kwa Unguja na Pemba. Pia, Serikali imepanga kufunga mita maalum kwa matumizi ya wateja wakubwa AMR ambazo zitarahisisha kupata mapato na kugundua udanganyifu wowote utakaofanywa na mteja. Aidha, Serikali kupitia Shirika la Umeme inawaungia wananchi huduma ya umeme kwa njia ya mkopo kwa wananchi ambao kipato chao ni cha chini ili kuwawezesha kupata huduma hiyo na kuliongezea Shirika mapato Kusimamia Uendeshaji wa Nishati ya Mafuta na Gesi Katika kusimamia utekelezaji wa Sera ya Nishati, Serikali imeandaa Mpango Mkakati wa Utekelezaji wa Sera ya Nishati. Vilevile, Serikali imekamilisha utayarishaji wa Sheria ya Udhibiti wa Huduma ya Maji na Nishati na Sheria ya Uanzishwaji wa Mamlaka ya Kusimamia Nishati ya 2013 (ZURA). Aidha, suala la Mafuta na Gesi lilijadiliwa katika Baraza la Nane la Wawakilishi ambapo Serikali imeshauriwa kwa namna mbalimbali kuhusiana na suala hili. Katika kuufanyia 65 kwa

79 kazi ushauri huo, Serikali imelifuatilia kwa karibu zaidi suala hili, na kwa kuanzia imefanya mazungumzo na kusaini makubaliano ya awali na Kampuni zinazojishughulisha na Uchimbaji wa Mafuta na Gesi Asilia ikiwemo Kampuni ya RAK GAS ya Ras Al khaima na Kampuni ya Shell ya Uholanzi. Dhamira ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar ni kuona kuwa katika kipindi kifupi kijacho Mafuta na Gesi yanachimbwa Zanzibar baada ya kufanyiwa kazi masuala ya Kisheria. 5.6 ARDHI Kwa kujua umuhimu wa ardhi kwa maendeleo ya kisasa ya uchumi na ya kijamii, Ilani ya CCM ya mwaka imeiagiza Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kukamilisha Sera ya Ardhi ya Zanzibar na kusimamia utekelezaji wa Mpango wa Kitaifa wa Matumizi Bora ya Ardhi. Serikali katika kulitekeleza agizo hili imeendaa Sera ya Ardhi ambayo itasimamia matumizi bora ya ardhi kwa faida ya sasa na vizazi vijavyo. Aidha, kazi za kupitia na kutayarisha upya Mpango Mkuu wa Kitaifa wa Matumizi Bora ya Ardhi wa Zanzibar (National Land Use Plan) umefikia asilimia 80. Vilevile, utayarishaji wa mipango ya kina ya vijiji vya ukanda wa pwani kwa ajili ya maendeleo ya utalii kwa kijiji cha Nungwi imefikia asilimia 85. Kazi inayoendelea ni utayarishaji wa Mpango Mkakati wa Kitaifa wa Maendeleo ya Miji (National Spatial Development Strategy) unaokusudiwa kutoa muongozo maalum wa uendelezaji wa miji yetu ya Unguja na Pemba ili kuwezesha ukuaji endelevu wa miji hiyo. Mpango huu unakwenda sambamba na Mpango Mkuu wa Matumizi Bora ya Ardhi nchini. Vilevile, ripoti za hali halisi ya Mji wa Zanzibar, na uchambuzi wa taarifa kwa ajili ya utayarishaji wa Mpango Mkuu wa Matumizi ya Ardhi ya Mji wa Zanzibar zimetayarishwa. Pia, Serikali imeongeza kazi ya upimaji wa viwanja ambapo jumla ya viwanja 1,185 vimepimwa kama inavyoonekana katika jedwali Namba 2. Jedwali Namba 2: Maeneo yaliyopimwa viwanja Zanzibar Na. MAENEO IDADI 1. MAKAAZI HUDUMA VITEGA UCHUMI TAASISI MASHAMBA

80 JUMLA 1,185 Serikali imeendeleza kazi ya usajili wa ardhi katika maeneo mbalimbali hasa maeneo ambayo hayajapimwa ili kuyapima na kuwapatia wahusika hati za umiliki wa ardhi kwa mujibu wa Sheria. Katika juhudi za kupunguza migogoro ya ardhi na kupunguza kesi za malalamiko ya ardhi, Serikali imeziimarisha Mahakama za Ardhi na kuanzisha Mahakama nyengine za ardhi katika Mikoa yote ya Unguja na Pemba na kuongeza idadi ya Mahakimu katika Mahakama hizo. Pia, Serikali imezifanyia mapitio na marekebisho ramani zote kwa mujibu wa mabadiliko yanayojitokeza, pamoja na kuzihuisha ramani za miji ya Zanzibar (Unguja Mjini, Chake Chake, Wete na Mkoani) vikiwemo visiwa vidogo vidogo. Katika hatua hii Serikali imechapisha ramani mpya ya visiwa vya Unguja na Pemba ambazo zimeanza kutumika. Aidha, Serikali imefanya matayarisho ya mipaka ya kiutawala ya Mikoa na Wilaya za Unguja na Pemba, ambapo kwa upande wa Unguja, upimaji wa maeneo tayari umefanyika:- Wilaya ya Kaskazini A na Kaskazini B, Wilaya ya Kaskazini B na Wilaya Magharibi A na Wilaya ya Kati, Wilaya ya Magharibi A na Wilaya Magharibi B na Wilaya ya Kati Wilaya ya Mjini na Wilaya ya Magharibi A na Wilaya ya Magharibi B Na kwa upande wa Pemba pia upimaji huo unaendelea ambapo maeneo yafuatayo yamepimwa:- Wilaya ya Micheweni na Wilaya ya Wete, Wilaya ya Wete na Wilaya ya Chake Chake Usajili za Ardhi kwenye Maeneo ya Fukwe na Miji Maeneo ya Fukwe Serikali imefanya kazi ya utambuzi wa umiliki wa ardhi katika maeneo ya fukwe za Nungwi, Paje na Chwaka kwa Unguja na maeneo ya Michenzani kwa Pemba. Jumla ya wamiliki 1,600 wametambuliwa kwa upande wa Nungwi na wamiliki 1,000 kwa upande wa Paje Maeneo ya Miji Katika maeneo ya miji, kazi ya utambuzi wa umiliki wa ardhi ilifanyika kwa kipindi cha majaribio (Pilot) ambapo jumla ya wamiliki 6,000 walitambuliwa na tayari wameshasajiliwa. Maeneo ya 67

81 miji ambayo yameshasajiliwa ni Shehia zote za Mji Mkongwe, Mchangani, Vikokotoni, Mwembetanga, Mlandege, Kikwajuni bondeni, Mwembeladu, Mwembeshauri, Miembeni, Rahaleo, Gulioni, Kwahani, Kwalinatu, Chukwani na Kidongochekundu. SEHEMU YA SITA 6.0 HUDUMA ZA JAMII 6.1 Elimu Serikali imetoa kipaumbele kwa Sekta ya Elimu kwa sababu ndio msingi wa maendeleo ya jamii na Taifa kwa jumla. Katika kulitilia uzito suala hilo Serikali imechukua hatua mbalimbali katika kuboresha elimu Elimu ya Maandalizi Katika kuendeleza juhudi za kuongeza ushiriki wa wanafunzi katika ngazi ya maandalizi, Serikali imendelea kutekeleza Sera ya Elimu ya mwaka 2006, ambayo imeelekeza kuwa elimu ya maandalizi ni sehemu ya elimu ya lazima. Madarasa ya elimu ya awali yamefunguliwa katika skuli 73 za msingi Unguja na Pemba. Aidha, idadi ya wanafunzi wa skuli za maandalizi imeongezeka kutoka 29,732 (15,216 wanawake na 14,516 wanaune) mwaka 2010 hadi kufikia wanafunzi 38,808 (19,654 wanawake na 19,154 wanaume) mwaka. 68

82 Utayarishaji wa Vifaa vya Kufundishia na Kujifunzia vya Elimu ya Maandalizi Skuli za Maandalizi zimepatiwa vifaa vya kufundishia na kujifunzia ili kupunguza mzigo kwa wazazi wa kuchangia ununuzi wa vifaa vya skuli. Serikali imewapatia mafunzo watendaji 48 wanaohudumia watoto katika skuli za maandalizi juu ya elimu ya afya, maji na usafi wa mazingira ili waweze kuwatunza vyema watoto hao. Aidha, Serikali imekamilisha uchapishaji wa moduli ya nne (4) na ya tano (5) kwa ajili ya kutolea mafunzo kwa wakufunzi wa walimu kwa njia ya TEHAMA. Vilevile, vifaa vya kujifunzia wanafunzi wa elimu ya maandalizi vimenunuliwa vikiwemo vibao vya kuandikia (slates), kadi za nambari na za maneno. Pembea kwa ajili ya michezo ya wanafunzi wa maandalizi zimejengwa katika skuli 30. Mafunzo ya Mtaala wa masomo ya Kiingereza na Kiarabu yametolewa kwa walimu wa skuli za maandalizi za Serikali za Unguja na Pemba. Serikali imewapatia mafunzo walimu wapatao 201 ya kuinua uwezo wa kufundisha watoto wadogo, walimu 280 walipatiwa mafunzo juu ya mtaala mpya wa elimu ya maandalizi. Aidha, wakufunzi 63 watasomesha walimu wa maandalizi kwa njia ya redio Unguja na Pemba Kuongeza Idadi ya Madarasa ya Elimu ya Maandalizi Idadi ya skuli za maandalizi imeongezeka kutoka skuli 238 mwaka 2010 hadi 279 mwaka, ongezeko hili ni sawa na asilimia 17. Aidha, Serikali imekamilisha ujenzi wa skuli za maandalizi za Kama, Potoa, Tunduni, Jongowe na Konde na kuzipatia samani za madarasani na ofisini. Aidha, ukarabati wa skuli ya maandalizi ya Machomane umefanyika. Vilevile, jumla ya madawati (meza na viti) 545 yamesambazwa katika skuli mbalimbali katika kipindi cha miaka mitano. 69

83 Rais wa Zanzibar Dkt. Ali Mohamed Shein akifungua Skuli Mpya ya Maandalizi ya Saemaul Cheju Zanzibar Pia, Sekta Binafsi imeitikia wito wa Serikali wa kuanzisha skuli za maandalizi. Hadi kufikia mwaka 2014/, jumla ya skuli za maandalizi za Watu Binafsi zimefikia 244 zikiwa na idadi ya wanafunzi 30,256 na Skuli za maandalizi za Serikali ni 35 zenye jumla ya wanafunzi 16, Kukamilisha Sera ya Makuzi na Malezi ya Mtoto Serikali inaendelea na mchakato wa kutengeneza sera mpya ya watoto itakayojulikana kama Sera ya Watoto Zanzibar (Zanzibar Children Policy). Sera hiyo itachukua nafasi ya Sera ya mwanzo iliyojulikana kama Sera ya Hifadhi na Maendeleo ya Mtoto ya mwaka Sera hiyo mpya pamoja na mambo mengine itazingatia mambo makuu yaliyozuka mfano Sheria ya Mtoto Namba 6 ya 2011, Mahakama ya Mtoto, MKUZA II na Vision Sera hiyo pia, itazingatia masuala ya Makuzi na Malezi ya Mtoto Kuimarisha mazingira ya Skuli za Msingi Serikali inaendelea kuhamasisha wananchi na wadau wengine wa maendeleo kujenga skuli mpya za msingi. Kutokana na uhamasishaji huo, idadi ya skuli za msingi imeongezeka kutoka 299 mwaka 2010 hadi kufikia 359 mwaka, ongezeko hilo ni sawa na asilimia 20. Vilevile, katika kipindi hichi cha miaka mitano, Serikali imekamilisha ujenzi wa madarasa 326 (180 Unguja na 70

84 146 Pemba). Pia, jumla ya madawati 7,955, seti za viti vipatavyo 2,371 na meza za walimu 2,329 zimechongwa na kusambazwa katika madarasa yaliyokamilishwa kujengwa Unguja na Pemba. Mabanda sita mapya ya skuli ya Msingi Jojo Wilaya ya Wete Mkoa wa kaskazini Pemba Aidha, Serikali imeboresha mazingira ya skuli nyingi mpya na kongwe Unguja na Pemba kwa kujenga ramp ambazo watoto wenye ulemavu wanaweza kuingia madarasani kwa urahisi. Aidha, ujenzi wa vyoo unaendelea katika skuli mbalimbali Unguja na Pemba, Serikali imetenga vyoo maalumu kwa matumizi ya wanafunzi wenye mahitaji maalum. Jumla ya wanafunzi 203 wenye aina mbalimbali za ulemavu wameandikishwa skuli katika ngazi ya elimu ya msingi kupitia elimu mjumuisho Kuimarisha Ufundishaji katika Madarasa ya Awali ya Msingi (Std 1-4) Serikali imeajiri walimu 975 wa ngazi ya cheti na kupangiwa kazi katika skuli za mikoa mitano ya Unguja na Pemba. Aidha, walimu 1,823 wanaofundisha katika ngazi ya elimu ya msingi wamepatiwa mafunzo ya ngazi ya Stashahada ya Elimu ya Msingi katika chuo cha Kiislamu Mazizini Unguja, Chuo cha Kiislamu Micheweni Pemba na Chuo cha Ualimu cha Benjamin William Mkapa kwa kipindi cha miaka mitano iliyopita. Vilevile, jumla ya vitabu vya kiada 711,054 vya elimu ya msingi (Std 1-4) vimechapishwa na kusambazwa katika skuli za Unguja na Pemba. Vitabu husika ni vya masomo ya Kiswahili, Hesabati, Sayansi, Sayansi Jamii na Kiingereza. Idadi ya wanafunzi walioandikishwa katika darasa la kwanza imeongezeka kutoka 38,743 (19,163 wanawake na 19,580 wanaume) mwaka 2010 hadi kufikia 43,062 (21,129 71

85 wanawake na 21,933 wanaume) mwaka. Pia, uandishi wa vitabu vya masomo 10 (kati ya 12) ya madarasa ya tano (5) na sita (6) unaendelea Kuondoshwa kwa Michango ya Wazee katika ngazi ya Elimu ya Msingi Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imeondosha michango ya wazee wa wanafunzi wa ngazi ya msingi ili kuhakikisha fursa sawa ya elimu inapatikana kwa watoto wote wa Unguja na Pemba bila kujali kipato cha wazee wao. Katika kulitekeleza hili, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kupitia Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali, itazipatia skuli zote, za msingi za serikali, vifaa vya kujifunzia na kusomeshea kwa ajili ya wanafunzi wao. Vifaa hivyo ni Mabuku, Chaki, Daftari la Mhudhurio, Manilla, Karatasi za A4, Gundi, Mkasi, Marker Pen, Vifaa vya Maabara na Vitabu. Dhamira hii itasaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza au kuondosha kabisa tatizo la watoto kutopelekwa skuli kwa sababu ya umasikini wa wazee wao katika kuwahudumia watoto wao mahitaji yao ya skuli Elimu ya Sekondari Katika kuendeleza juhudi za ujenzi wa skuli mpya za sekondari, Serikali imekamilisha ujenzi wa skuli 19 Unguja na Pemba. Ujenzi huo umefanya idadi ya skuli za Sekondari kuongezeka na kufikia jumla ya skuli 263 mwaka kutoka skuli 194 mwaka Skuli zenyewe ni Mlimani (Matemwe), Mwanda, Mapinduzi (Chaani), Umoja Uzini, Mikindani (Dole), Jumbi, Kombeni, Mtule, Kiembesamaki, Faraja (Kwa Mtipura) na Mpendae kwa upande wa Unguja na Shamiani, Wawi, Ngwachani, Kiwani Mauani, Utaani, Pandani, Konde na Chwaka Tumbe kwa upande wa Pemba. Aidha, ujenzi wa skuli ya Sekondari za Kibuteni, Donge na Mkanyageni unaendelea. Vilevile, katika kipindi cha miaka mitano, Serikali imekamilisha ukarabati wa madarasa 263 ya skuli za sekondari Unguja na Pemba. 72

86 Jengo la Skuli ya Sekondari ya Faraja lililofunguliwa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mheshimiwa Balozi Seif Ali Iddi, Kwamtipura Mjini Zanzibar Jengo la Skuli ya Madungu Sekondari lililojengwa hivi karibuni Kukamilika kwa skuli hizo kumesaidia kupunguza msongamano wa wanafunzi kwa baadhi ya skuli za sekondari. Kutokana na juhudi hizi, idadi ya wanafunzi katika ngazi ya sekondari kidato cha kwanza hadi cha nne imeongezeka kutoka 78,165 (41,804 wanawake na 36,361 wanaume) mwaka 2012 na kufikia 79,662 (43,544 wanawake na 36,118 wanaume) mwaka Vilevile, Serikali imechonga na kusambaza jumla ya madawati 80,806, viti 4,934 na meza 5,800 kwa Skuli 73

87 za Sekondari mpya zilizojengwa kwa Ufadhili wa Benki ya Dunia pamoja na zile za wananchi Unguja na Pemba. Katika kuhakikisha upatikanaji wa vitabu kwa Skuli za Sekondari, Serikali imesambaza jumla ya vitabu 201,162 katika skuli za Unguja na Pemba. Jumla ya vitabu vya kiada vipatavyo 748,316 na vya maktaba 30,260 kwa skuli za sekondari vimenunuliwa na kusambazwa. Vitabu hivyo ni vya masomo ya Kiswahili, Kiingereza, Jiografia, Civics, Historia, Kompyuta na masomo ya Ualimu. Pia, vifaa vya maabara vya skuli za sekondari kwa kidato cha nne (4) na sita (6) vimenunuliwa na kusambazwa katika skuli 100 za Unguja na Pemba.Vilevile, Serikali imekamilisha ujenzi wa nyumba 27 za walimu katika skuli za Unguja na Pemba kama zinavyoonekana katika jedwali namba 3. Jadweli namba 3: Idadi ya nyumba za walimu zilizojengwa Unguja na Pemba Na. SKULI IDADI YA NYUMBA 1 Mwanda 3 2 Uzini 3 3 Paje (Mtule) 3 4 Pandani 3 5 Chwaka Tumbe 3 6 Kiwani 3 7 Wawi 3 8 Utaani 3 9 Matemwe 3 Jumla Kuimarisha Elimu ya Sayansi na Hesabati kwa Kuendeleza Kambi za Sayansi Katika juhudi za kuimarisha ufundishaji wa masomo ya sayansi, jumla ya walimu 10 wamepatiwa mafunzo nje ya nchi na walimu 450 wa Sekondari wamepatiwa mafunzo ya kuinua uwezo wao wa kufundisha masomo ya hesabati na sayansi ikiwemo utumiaji wa vifaa vya maabara kikamilifu. Aidha, Kambi za sayansi zimeendeshwa kwa washiriki 560 katika Vituo vya Walimu viliopo 74

88 Unguja na Pemba ili kuwavutia wanafunzi wapende masomo ya sayansi na hesabati. Pia, Serikali imeziteuwa Skuli za Benbella kwa Unguja na Utaani kwa Pemba kuwa skuli maalum za sayansi kwa wanawake. Maabara Mpya katika Skuli ya Sekondari ya Kiembesamaki Kutoa Mafunzo kwa Walimu Wakuu na Maafisa wa Elimu wa Wilaya na Mikoa Serikali imewapatia mafunzo Walimu Wakuu 350 juu ya miiko na maadili ya kazi ya ualimu. Vilevile, mafunzo ya uongozi kwa walimu wakuu na wasaidizi walimu wakuu wapya wa skuli 32 za Unguja yametolewa. Pia, mafunzo ya kuwajengea uwezo wakaguzi pamoja na walimu wakuu 92 yametolewa ili kuimarisha kazi ya ukaguzi wa skuli Elimu Mbadala na Elimu ya Watu Wazima Juhudi za kufuta ujinga wa kutojua kusoma na kuandika zimendelezwa. Hivi sasa kuna madarasa 431 yenye wanakisomo 6,963 (5848 wanawake na 1,115 wanaume). Aidha, uandaaji wa mitaala kwa ajili ya mafunzo ya wakufunzi wa Mafunzo ya Amali umekamilika. Kazi ya kuandika mihutasari mipya ya masomo imekamilika na kazi ya kuandika vitabu vya wanafunzi vya masomo 11 pia imekamilika. Serikali inaendelea kutoa elimu mbadala kwa lengo la kuwapatia masomo vijana wenye umri kati ya miaka 10 hadi 15 walioko nje ya skuli, wakiwemo walioacha masomo njiani kwa sababu mbalimbali na waliokosa fursa ya kuanza masomo wakiwa na umri mdogo. 75

89 Kituo cha Elimu Mbadala Rahaleo kinatoa fani mbalimbali zikiwemo ushoni, upishi, umeme, uchongaji na utunzaji nyumba. Idadi ya wanafunzi katika kituo hicho imeongezeka kutoka 256 mwaka 2011 (wanawake 67 na wanaume 179) hadi kufikia wanafunzi 305 (wanawake 73 na wanaume 232) mwaka Huduma za Maktaba Katika kuimarisha huduma za maktaba, Serikali imekamilisha Ujenzi wa Maktaba Kuu ya Zanzibar na ujenzi wa Maktaba Kuu Pemba unaendelea. Aidha, jumla ya vitabu 7,116 mwaka 2011 vya masomo mbalimbali vikiwemo vitabu vya watoto, vitabu vya kiada vya msingi, sekondari, elimu ya juu pamoja na masomo ya ualimu vimenunuliwa. Kwa mwaka huu, jumla ya vitabu 5,467 vimenuuliwa kwa ajili ya matumizi kwa Maktaba Kuu Unguja na Maktaba Kuu Pemba. Maktaba Kuu ya Zanzibar iliyopo eneo la Maisara Mpirani Kuendeleza Mafunzo ya Ukutubi Serikali imeanzisha mafunzo ya ukutubi ya awali ambapo jumla ya wakutubi 151 wamehitimu mafunzo ya ukutubi ngazi ya awali. Aidha, wafanyakazi saba (8) wameendelezwa katika ngazi ya Stashahada ya Ukutubi na utunzaji kumbukumbu. Vilevile, mafunzo ya ukutubi yametolea kwa walimu wa skuli 44 za Unguja na skuli 40 za Pemba ili wapate taaluma sahihi juu ya namna bora ya kutoa huduma za maktaba na kukuza maendeleo ya elimu nchini. Pia, jumla ya walimu

90 kutoka skuli za Wilaya ya Kaskazini A, Kusini Unguja, Chake Chake na Mkoani walipatiwa mafunzo juu ya usimamizi wa maktaba Kuhamasisha Wananchi Kutumia Maktaba Serikali imeendelea kushajiisha na kutoa ushauri kwa wananchi juu ya kuanzisha maktaba katika maeneo mbalimbali yakiwemo skuli na maeneo ambayo jamii zinaishi. Aidha, Shirika la Maktaba kwa kushirikiana na Jumuiya isiyo ya kiserikali MJUKIZA limeanzisha utaratibu wa kuwa na maktaba za jamii ili ziweze kutoa huduma kwa jamii kwa ukaribu zaidi. Hadi sasa jumla ya maktaba nane (8) za jamii katika maeneo ya Chumbuni, Welezo, Kiembesamaki, Mpapa, Uzini, Fumba, Bweleo na Tumbatu zinatoa huduma. Pia, Programu 182 za watoto zimeendeshwa katika Maktaba Kuu za Unguja na Pemba Elimu ya Juu Serikali inatilia mkazo katika kuendeleza elimu ya juu kwa kushirikiana na Sekta Binafsi. Kwa kuzingatia hili, Serikali inashirikiana na Benki ya Kiarabu kwa Maendeleo ya Kiuchumi Afrika (BADEA) katika ujenzi wa Chuo Kikuu cha Taifa (SUZA) Tunguu. Ujenzi huo umekamilika kwa majengo manne (4) pamoja na kuwekwa samani, kompyuta na vifaa vya maabara na majengo hayo tayari yameanza kutumika. Pia, Chuo kimewapeleka masomoni ndani na nje ya nchi wafanyakazi 51 (31 ngazi ya shahada ya uzamivu, 14 ngazi ya shahada ya uzamili, 3 shahada ya kwanza na 3 stashahada) ili kuwaendeleza wakufunzi wake na kuimarisha ufanisi katika Chuo hicho. Vilevile, Chuo kimeanzisha Diploma ya Sayansi ya Ualimu yenye jumla ya wanafunzi 102 na Diploma ya Uongozi yenye jumla ya wanafunzi 100. Serikali kupitia Chuo Kikuu cha Taifa Cha Zanzibar (SUZA) imeanzisha Skuli ya Afya na Sayansi za Tiba katika Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar (SUZA). Skuli hii imeanza na fani ya udaktari (Medical Doctor MD) kwa msaada wa madaktari kutoka Cuba na inaendesha shughuli zake katika majengo ya Wizara ya Afya yaliyopo katika hospitali ya Mnazimmoja. Hadi sasa skuli imeshaandikisha jumla ya wanafunzi 81 kati ya hao 31 wapo mwaka wa pili na 51 wapo mwaka wa kwanza. Chuo kwa upande wake kinafanya jitihada za kufundisha vijana wa Kizanzibar ambao watakuja kufundisha katika skuli hiyo. Hivi sasa tayari yupo mwalim Mzanzibar mmoja na wengine wako masomoni kupitia ufadhili wa mradi wa Oman (OAF). 77

91 Udahili wa wanafunzi katika Chuo hicho umeongezeka kutoka wanafunzi 1,972 mwaka 2010 (wanawake 853 na wanaume 1,119) na kufikia wanafunzi 2,078 (wanawake 1,244 na wanaume 834) mwaka. Aidha, Chuo kimeongeza kutoa wahitimu wa fani mbalimbali kutoka 524 mwaka 2010 (wanawake 347 na wanaume 177) na kufikia 749 (418 wanawake na wanaume 331) mwaka. Majengo ya Vitivo vya Sayansi na Kompyuta katika Chuo Kikuu cha Taifa (SUZA) Aidha, katika kuimarisha elimu ya sayansi na teknolojia ya kisasa, Vyuo Vikuu viliopo nchini vimeanzisha programu za sayansi na IT kwa ngazi ya Shahada na Stashahada. Katika kuongeza wigo wa utoaji mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu ndani na nje ya nchi, idadi ya wanafunzi wanaodhaminiwa na Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu imeongezeka kutoka 1,022 mwaka 2010 (wanawake 534 na wanaume 488) na kufikia 2,658 (wanawake 1,372 na wanaume 1,286) mwaka. Kwa mwaka, Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu imewadhamini wanafunzi wapya 1,410. Kati ya hao 1,028 wamejiunga na masomo katika vyuo vya ndani ya Zanzibar, 370 vyuo vya Tanzania bara na 12 vyuo vya nje ya nchi. Jumla ya wanafunzi 2,823 ambao wanadhaminiwa na Bodi ya mikopo ya Elimu ya Juu, wanaendelea na masomo kwa vyuo mbalimbali ndani na nje ya nchi. Kiwango cha kukusanya madeni kwa wanafunzi waliokopeshwa 78

92 kupitia Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu imeongezeka kutoa Shilingi 8,200,000 mwaka 2011 hadi kufikia Shilingi 99,941,218 mwaka. Vilevile, Serikali imeboresha mazingira ya wawekezaji wa Sekta Binafsi kuendelea kuekeza katika elimu ya juu. Chuo Kikuu cha Zanzibar (Zanzibar University) kinaendelea kutoa mafunzo mbalimbali katika Shahada ya Kwanza na Shahada ya Pili. Chuo cha elimu Chukwani kimepandishwa hadhi na kuwa Chuo Kikuu kamili (Al-ssumait University) na hivyo kukiwezesha kutoa shahada za juu Kuimarisha Mafunzo ya Ualimu Serikali imeandaa Rasimu ya Sera ya Mafunzo ya Ualimu Kazini na imefanya mapitio ya Mtaala wa Diploma ya Msingi. Mtaala huo umeingiza masomo mapya yakiwemo ya Habari na Mawasiliano, Mafunzo ya Amali, Uongozi na Michezo. Kazi ya kutayarisha mtaala wa stashahada kwa walimu wa maandalizi inaendelea katika Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar (SUZA). Vilevile, mafunzo kwa wakufunzi wa vyuo juu ya matumizi ya mtaala mpya yalitolewa na mafunzo kazini ya masomo mbalimbali kwa walimu wa skuli za msingi na sekondari yametolewa. Jumla ya walimu wa skuli za msingi 1,539 walishiriki mafunzo ya sayansi na walimu 2,000 walishiriki mafunzo ya lugha ya kiingereza. Kwa upande wa skuli za sekondari walimu 150 walishiriki mafuzo ya sayansi na hesabati. Serikali imeendelea kutoa mafunzo maalum kwa wakufunzi wa TAP wapatao 19 (Unguja 12 na Pemba 7). Pia, mafunzo ya kompyuta yametolewa kwa walimu 120 Unguja na Pemba. Vilevile, vituo viwili vya ualimu vya Dunga na Kiembesamaki vimepatiwa kompyuta na vifaa vyake kwa ajili ya matumizi ya vituo, ukuzaji wa matumizi ya TEHAMA na kurahisisha uwekaji wa kumbukumbu. Aidha, walimu 16 walipatiwa mafunzo ya lugha ya kiingereza na mbinu za kufundishia kwa njia ya mtandao, Walimu saba (7) na Mkaguzi mmoja (1) walishiriki mafunzo hayo ya ufundishaji wa masomo ya sayansi yaliyotolewa kupitia Mradi wa SMASSE huko Nairobi. Serikali pia, imeendelea kutoa mafunzo ya ualimu kwa njia ya elimu masafa kwa walimu wa msingi wasiosomea ili kuweza kupunguza idadi ya walimu wasiosomea mafunzo hayo. Idadi ya walimu wasiosomea imepungua kutoka walimu 630 mwaka 2010 (wanawake 515 na 115 wanaume) hadi kufikia walimu 501 (445 wanawake na 56 wanaume) mwaka. Jumla ya wafanyakazi 2,867 79

93 wameendelezwa katika vyuo vya ndani na nje ya nchi katika ngazi za Cheti, Stashahada, Shahada ya Uzamivu na Uzamili Mafunzo ya Ualimu Mafunzo ya ualimu hutolewa katika vyuo vitatu ambavyo ni Chuo cha Kiislamu Mazizini, Chuo cha Kiislamu Kiuyu na Chuo cha Benjamin William Mkapa Pemba. Vyuo hivi vinatoa mafunzo ya ualimu katika ngazi ya Stashahada ya Sanaa Sekondari, Stashahada ya Sayansi Sekondari, Stashahada Ualimu Msingi, Stashahada ya somo la Dini na Kiarabu na Cheti cha Ualimu wa Elimu Mjumuisho. Kwa kipindi cha miaka mitano, vyuo hivyo vimesomesha jumla ya wanafunzi 5,009 (3,740 wanawake na 1,269 wanaume). Kati ya wanafunzi hao, wanafunzi 71 (66 wanawake na 5 wanaume) ni wa mafunzo ya Cheti cha Ualimu wa Elimu Mjumuisho Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Amali Serikali kupitia Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali imeendelea kutoa elimu ya amali kwa wanafunzi 3,130 (936 wanawake na 2,194 wanaume) katika vituo vitatu vya Mafunzo ya Amali vya Mkokotoni, Mwanakwerekwe na Vitongoji. Vituo hivyo vinatoa mafunzo ya fani mbalimbali za ufundi zikiwemo Useremala, Ushoni, Uhunzi, Upishi, Uchoraji na Uandishi wa alama, Uashi, Ufundi Bomba, Teknolojia ya Habari na Mawasiliano, Huduma za Chakula na Vinywaji, Ufundi magari, Umeme na Ufundi mafriji na Viyoyozi. Aidha, elimu ya ufundi inaendelea kutolewa katika Taasisi ya Karume ya Sayansi na Teknolojia. Idadi ya wanafunzi imeongezeka katika Taasisi hii kutoka 237 mwaka 2010 (wanawake 55 na wanaume 182) hadi kufikia wanafunzi 1,308 (wanawake 250 na wanaume 1,058) mwaka. Aidha, Taasisi ilikuwa na jumla ya wanafunzi 185 kwa mwaka 2011 (wanawake 36 na wanaume 149) na kuongezeka hadi wanafunzi 277 (64 wanawake na 213 wananume) wa ngazi ya stashahada (NTA 4 NTA 6) ambao wanaendelea na masomo katika fani za uhandisi ujenzi na usafirishaji, uhandisi mitambo, uhandisi magari, uhandisi mawasiliano ya anga, elektroniki na kompyuta na uhandisi umeme Kuimarisha Taasisi ya Karume ya Sayansi na Teknolojia Taasisi ya Karume ya Sayansi na Teknolojia imeimarishwa kwa ukarabati wa mfumo wa maji na umeme na ukarabati wa vyoo vya jengo la ICT pamoja na dahalia za wasichana na wavulana umefanyika. Pia, majengo ya taasisi hiyo yameunganishwa na nishati ya umeme wa jua ili 80

94 kupunguza gharama za umeme. Vilevile, vifaa mbalimbali vya kufundishia vikiwemo vitabu 150 vya masomo mbalimbali vimenunuliwa. Wanafundi wa Chuo cha Ufundi Karume wakiwa katika mafunzo ya vitendo Kuimarisha Skuli ya Ufundi Kengeja Katika kuimarisha Skuli ya Ufundi Kengeja, Serikali imenunua vifaa vya karakana ya umeme, vifaa vya workshop za uhunzi na kompyuta. Aidha, ujenzi wa madarasa manne (4) na ukarabati wa majengo na miundombinu ya maji umefanyika. 6.2 Sekta ya Afya Kama inavyofahamika kuwa afya ni suala la msingi kwa binadamu katika kujiletea maendeleo yao na taifa kwa ujumla. Kwa kuzingatia Ilani ya CCM mwaka 2010, Serikali imejikita katika kusimamia utekelezaji wa sera na programu mbalimbali zinazohusiana na Sekta ya Afya. Aidha, Huduma za Kinga na Tiba zimeimarishwa katika hospitali na vituo vya afya pamoja na kutolewa elimu ya afya kwa wananchi ili kujikinga na maradhi ya kuambukiza na yasiyo ya kuambukiza Huduma za Kinga Serikali imefanya utafiti wa kuangalia kiwango na sababu hatarishi zinazopelekea kupata maradhi yasioambukiza (National Non Communicable Disease Risk Factors Survey). Matokeo ya utafiti huo yanaonesha kuwa asilimia 14.3 ya watu wana uzito mkubwa (obesity), asilimia 33 ya watu walio katika umri wa miaka wana shindikizo la damu. Serikali inaendelea kuchukua juhudi 81

95 mbalimbali za kukuza uelewa wa jamii juu ya kujikinga na maradhi yasiyoambukiza yakiwemo kula vyakula vyenye chumvi nyingi, kuvuta sigara, kutokufanya mazoezi ya viungo na matumizi ya sukari kwa kiwango kikubwa. Uelewa huo umetolewa kupitia maonyesho maalum ya filamu na vipindi mbalimbali vya redio na televisheni. Serikali kwa kushirikiana na Jumuiya ya Watu Wanaoishi na Kisukari, imeshajiisha jamii kuanzisha vikundi vya mazoezi katika Wilaya zote za Unguja na Pemba kwa nia ya kujikinga na maradhi hayo. Hadi sasa jumla ya vikundi 10 vimeanzishwa katika maeneo mbalimbali Unguja na Pemba. Vikundi hivi vimekuwa vikitembelewa mara kwa mara na kupewa maelekezo na pia kualikwa katika Matamasha tofauti yanayohusiana na mazoezi. Katika kuendeleza utoaji wa elimu ya afya ya jamii, Serikali imeanzisha redio ijulikanayo kwa jina la Afya FM Redio ambayo inatoa elimu ya masuala ya afya kwa jamii Huduma za Tiba Serikali imeandaa muongozo wa matibabu ya maradhi yasiyoambukiza kama vile Shindikizo la damu, kansa na kisukari. Muongozo huu umezingatia matibabu ya maradhi yasiyoambukiza kwa upana wake. Aidha, Serikali imeweza kutoa huduma za maradhi ya moyo na shindikizo la damu katika hospitali za Wilaya za Chake Chake, Wete na Abdalla Mzee kwa kushirikiana na madaktari kutoka Hospitali ya Mnazimmoja. Pia, Serikali kwa kushirikiana na Jumuiya ya Wanafunzi wa Udaktari Tanzania Medical Students Association (TAMSA), imefanya uchunguzi wa maradhi ya Kisukari na Shindikizo la Moyo katika Wilaya za Mjini, Magharibi, Kati, Kusini, Kaskazini A na Kaskazini B. Jumla ya watu 1,800 walifanyiwa uchunguzi wa Kisukari na matibabu yalitolewa kwa waliogunduliwa na matatizo hayo. Vilevile, jumla ya watu 2,585 wamepatiwa huduma za uchunguzi wa macho kwa mashirikiano na uongozi wa Shirika la Al-nour Charitable Agency la Zanzibar na Shirika la Bilal Muslim Agency kutoka Arusha Tanzania Bara. Watu 220 walifanyiwa upasuaji wa mtoto wa jicho. Katika jitihada za kuondoa maradhi ya kichocho, Serikali imeandaa Mpango wa ufuatiliaji wa makonokono katika mito na mabwawa; mabadiliko ya tabia kwa wananchi dhidi ya maradhi ya Kichocho na ulishaji wa dawa za Kichocho. Aidha, ulishaji wa dawa za Kichocho, Minyoo na 82

96 Matende umeendelea kutolewa kwa lengo la kutibu na kupunguza maambukizo mapya ya maradhi hayo. Dawa hizi zilitolewa na zinaendelea kwa wale wote wanaostahiki ambapo jumla ya watu 915,954 kwa Unguja na Pemba walipatiwa dawa hizo, idadi hii ni sawa na asilimia 83 ya waliostahiki kutumia dawa hizo Huduma Bora za Afya kwa Wananchi Wote Ili kuhakikisha kuwa huduma bora zinatolewa kwa wananchi wote nchini, Serikali imeendelea kuviendeleza vituo vya afya 84 vikiwemo vya Daraja la Kwanza na Daraja la Pili ambavyo vinatoa huduma za ziada kama vile huduma za uzazi, maabara na huduma za meno. Aidha, Serikali imeifanyia mapitio Sera ya Afya ya mwaka 1999 na kuwa na Sera mpya ya mwaka 2011 pamoja na Sheria ya Afya ya Jamii ambazo zinakwenda sambamba na mahitaji pamoja na mikataba ya kitaifa, kikanda na kimatifa katika utoaji wa huduma za afya nchini. Vilevile, Sheria ya Mkemia Mkuu wa Serikali (Chief Government Laboratory Act No ) imeandaliwa ambayo inaifanya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali kufanya kazi zake kisheria. Tayari Mwenyekiti na wajumbe wa bodi itakayosimamia utekelezaji wa sheria hii wameshateuliwa na wameshaanza kazi rasmi. Ili kuhakikisha upatikanaji wa dawa muhimu katika vituo vya afya unakuwa wa kuridhisha kwa wananchi wake, Serikali inaendelea kutoa huduma hizo bila ya malipo katika hospitali zote na vituo vya Afya vikiwemo Chukwani, Fuoni, Mahonda, Donge Vijibweni, Uroa, Jambiani, Nungwi, Matemwe, Pwani Mchangani, Tumbatu Gomani na Bumbwini Misufini kwa Unguja na kwa upande wa Pemba ni Makangale, Konde, Wingwi, Mizingani, Kojani Ukutini, Fundo na Bogoa. Vituo vyote hivi vinafaidika na upatikanaji wa dawa chini ya mpango maalum ujulikanao kama Zanzibar Integrated Logistic System. Vilevile, Serikali imejenga Bohari Kuu ya Dawa iliyopo Maruhubi ambayo itarahisisha kupata na kutoa taarifa za hali ya upatikanaji wa dawa kutoka hospitali na vituo vya afya mbalimbali nchini. 83

97 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mheshimiwa Dkt. Ali Mohamed Shein akikagua Bohari Kuu ya Dawa - Maruhubi Aidha, Serikali imewasomesha wanafunzi 38 madaktari kwa kushirikiana na Serikali ya Cuba wakiwemo wanawake 19 na wanaume 19 ambao tayari wamemaliza masomo yao na hivyo kupata madaktari wengine wazalendo 38. Idadi hiyo imewezesha madaktari wote wanaotoa huduma Zanzibar kufikia 142, kati ya hawa madaktari 40 ni madaktari wa kigeni kutoka Cuba na China hali ambayo imepelekea kwa sasa kuwa na uwiano wa daktari mmoja kuhudumia wastani wa wagonjwa 9,708. Vilevile, Jumla ya wafanyakazi 142 wa kada mbalimbali wamepelekwa masomoni ndani na nje ya nchi wakiwemo Madaktari 9, Wasaidizi madaktari 12, Wauguzi 96 na wengine kada nyenginezo za afya na zisizo za Afya. Hivyo, kufanya idadi ya wafanyakazi wote wanaoendelea na masomo kufikia 246 (wanaume 110 na wanawake 136). Aidha, jumla ya wafanyakazi 44 wamerudi masomoni na kupangiwa kazi kwa mujibu wa taaluma zao Kuendeleza Huduma za Tiba Asili Baraza la Tiba Asili Serikali kupitia Baraza la Tiba Asili na Tiba Mbadala imeelimisha jamii kupitia vyombo mbalimbali vya habari, kutumia vipeperushi pamoja na kufanya mikutano na waganga wa tiba asilia kupitia Masheha, Madiwani na Wakuu wa Wilaya. Pia, Baraza limefanikiwa kutengeneza Kanuni (regulations) za Tiba Asili na kutoa elimu kwa waganga. Sambamba na hayo, Baraza limeweza kusajili jumla ya Waganga 193 na Waganga Wasaidizi 58, baada ya kutimiza masharti 84

98 yaliyowekwa ikiwa ni pamoja na kutenga sehemu maalumu ya kutoa huduma kwa wagonjwa. Aidha, jumla ya kliniki 18 za tiba asili na tiba mbadala, viringe au sehemu wanazofanyia kazi 125 na maduka ya dawa za asili 39 yamesajiliwa baada ya kutimiza masharti ya sheria za Baraza. Pia, sampuli 23 za dawa asilia zimechunguzwa na Maabara ya Bodi ya Chakula na Madawa (ZFDB). Katika kuhakikisha Baraza la Tiba Asili linafanya kazi zake vizuri na ipasavyo limejenga uhusiano mzuri kati ya madaktari wakisasa (Biomedical Practitioners) na waganga wa asili (Traditional Healers) Kuimarisha Chuo cha Taaluma za Sayansi ya Afya Chuo cha Taaluma cha Sayansi ya Afya kinaendelea kutoa taaluma za afya kwa kiwango cha Stashahada katika fani mbalimbali. Katika kipindi cha miaka mitano ( ) chuo kimezalisha wahitimu 1,629 wakiwemo Wauguzi 612, Wasaidizi Madaktari 198, Maafisa afya ya Mazingira 136, Ufundi Sanifu wa Maabara 122, Wasaidizi Madaktari wa Afya ya Kinywa na Meno 201, Wafamasia 127, Ufundi Sanifu wa Vifaa Tiba (Biomedical Engineers) 55, Afisa Maabara 74, Wasaidizi Tabibu 50 na Wakunga 54. Wanafunzi wa Chuo cha Taaluma ya Sayansi ya Afya Mbweni wakiwa darasani Ili kuweka mazingira mazuri kiutendaji na hatimae kuongezeka kwa motisha kwa wafanyakazi wa Chuo, muundo wa Utumishi kwa wafanyakazi wa Chuo umetayarishwa na tayari umeshawasilishwa Serikalini kwa hatua za utekelezaji. 85

99 Serikali imeendelea kukiimarisha Chuo cha Sayansi ya Afya kwa kujenga jengo litakalotumika na wanafunzi wa shahada ya kwanza pamoja na majengo mawili ya dakhalia kwa msaada wa Serikali ya Oman. Pia, chuo kimeandaa Mpango wa Kujiendesha Kibiashara (Bussiness Plan) ili kiweze kukidhi mahitaji yake. Vilevile, chuo kimeanzisha masomo ya kujiendeleza kwa wafanyakazi wenye cheti kwa muda mrefu ambao hawakupata bahati ya kujiendeleza kielimu katika fani za Afya ambapo jumla ya wafanyakazi wanafunzi 183 wanaendelea na mafunzo chuoni hapo. Wanafunzi 11 wanaendelea na mafunzo ya elimu masafa kupitia Shirika la AMREF. Serikali kupitia Chuo cha Sayansi ya Afya inaendelea kuufanyia mapitio Mtaala wa Kada ya Dawa (Pharmaceutical science). Pia, imetengeneza Mtaala wa Kada ya Maradhi ya Viungo (Physiotherapy) kwa lengo la kuanzisha masomo hayo katika muhula wa masomo 2014/15 ili kuimarisha huduma za afya kwa wananchi. Jengo jipya la Chuo cha Taaluma ya Sayansi ya Afya - Mbweni 86

100 Mahafali ya 21 ya Wanafunzi wa Chuo cha Taaluma ya Sayansi ya Afya - Mbweni Kuendeleza Mapambano dhidi ya Malaria, UKIMWI, Kifua Kikuu na Ukoma Malaria Serikali imeweza kupunguza ugonjwa wa Malaria katika jamii kutoka asilimia 0.9 mwaka 2010 hadi kufikia asilimia 0.03 mwaka. Katika jitihada za kutokomeza kabisa ugonjwa wa malaria, Serikali kupitia Wizara ya Afya imefanikiwa kuchunguza watu 8,126 katika shehia tisa (9) zilizokuwa na ongezeko kubwa la wagonjwa wa Malaria, watu 97 sawa na asilimia 1.2 waligundulika kuwa na vimelea vya Malaria. Uchunguzi huo ulihusisha shehia za Cheju, Ng ambwa, Uzi, Ukongoroni, Shakani, Bweleo, Donge Mchangani, Mtende na Kibuteni. Vilevile, katika kudhibiti kasi ya kuenea maradhi ya Malaria, Serikali kupitia Wizara ya Afya inaendelea kuwafuatilia wagonjwa wanaoripotiwa kuwa na dalili za Malaria majumbani ambapo watu 1,282 walifanyiwa uchunguzi na watu 282 wamegundulika kuwa na malaria na kupatiwa matibabu Usambazaji wa Vyandarua katika Vituo vya Afya. Serikali kupitia Wizara ya Afya chini ya Mradi wa Kumaliza Malaria kwa kushirikiana na wahisani mbalimbali imeweza kugawa vyandarua vilivyotiwa dawa ili kupunguza maambukizo. Katika mwaka jumla ya vyandarua 717,000 viligaiwa kwa wananchi Unguja na Pemba kwa wastani wa vyandarua vitatu (3) kwa kaya. 87

101 Aidha, Kitengo hiki kimebadilisha utaratibu wa kugawa vyandarua kutoka kwenye mgao wa pamoja na kuingia kwenye ugawaji endelevu wa vyandarua. Utaratibu huu unahusisha mama wajawazito, watoto wenye chanjo ya miezi tisa, wanaogunduliwa na malaria wakati wa ufuatiliaji pamoja na makundi yenye mahitaji maalum. Jumla ya Vyandarua 30,474 vimesambazwa katika Vituo vya Afya Unguja na Pemba. Watoto wakirudi kuchukuwa Vyandarua vilivyotiwa dawa kufuatia mgao wa vyandarua hivyo Upigaji Dawa Majumbani Serikali inaendelea na upigaji dawa majumbani ambapo jumla ya nyumba 57,385 zilipigwa dawa sawa na asilimia 96 ya lengo. Zoezi hili limefanyika katika Wilaya tisa (9) za Unguja na Pemba ambapo limelenga kuzifikia Shehia 38 ambazo zimeonekana kuwa na wagonjwa wa Malaria mara kwa mara na nyumba 59,462 zilizohusika katika zoezi hili. 88

102 Wapiga Dawa ya kuuwa Mbu wanaosababisha Malaria Majumbani UKIMWI Kiwango cha mambukizi ya UKIMWI kimeendelea kubakia kuwa asilimia 0.6 na idadi ya watu walioambukizwa virusi vinavyosababisha UKIMWI (VVU) waliosajiliwa ni 7,820 kati ya hao watu 5,375 wanapata huduma ya ARV. Katika kuendeleza mapambano dhidi ya UKIMWI, Serikali imeimarisha huduma za tiba, huduma za kuzuia maambukizi ya mama kwenda kwa mtoto, vituo vya ushauri nasaha na upimaji wa VVU. Uimarishaji huo umefanywa kwa kuhakikisha nyenzo za kufanyia uchunguzi zinapatikana kwa wakati, kufuatilia maambukizi ya VVU miongoni mwa makundi yaliyo katika hatari ya maambukizo pamoja na makundi maalum na kuendeleza kutoa elimu kwa jamii juu ya kupunguza unyanyapaa kwa watu wanaoishi na VVU. Pia, Serikali imesambaza mashine tatu mpya za CD4 ambazo zimepelekwa katika Hospitali ya Mnazi Mmoja, Mwembeladu, na Kivunge. Aidha, mashine aina mbili za Haematology na Chemistry zimesambazwa katika Hospitali za Micheweni, Makunduchi, na Mwembeladu. Vilevile, Serikali inaendelea kuwahamasisha wananchi kuwa na tabia ya kupima afya zao na kujiepusha na maambukizi mapya ya UKIMWI. Serikali kupitia Tume ya UKIMWI imeipatia Jumuiya ya Watu Wanaoishi na Virusi vya UKIMWI (ZAPHA+) jumla ya Shilingi 551,471,765 ili kuendelea na shughuli zao za kuelimisha jamii juu ya mapambano dhidi ya UKIMWI. Pia, vituo 89

103 vinavyotoa huduma ya ushauri nasaha na upimaji wa VVU vimeongezeka kutoka vituo 87 mwaka 2012 hadi kufikia vituo 91 mwaka, kati ya hivyo Unguja 58 na Pemba 33. Makamu wa Pili wa Rais Balozi Seif Ali Iddi katika Maadhimisho ya siku ya UKIMWI Duniani akikagua huduma ya kuchangia damu salama Kifua Kikuu na Ukoma Serikali kupitia Wizara ya Afya imeendelea kutoa matibabu ya Magonjwa ya Kifua Kikuu na Ukoma kwa wananchi, ambapo Mpango wa Ulishaji Dawa kwa Jamii (Community TB Care) umeendelea. Takwimu zinaonesha kwamba wagonjwa 2,865 wamegundulika na maambukizi katika kipindi cha miaka mitano iliyopita. Kwa upande wa maradhi ya ukoma jumla ya watu 598 waligundulika na maradhi haya, kati yao wagonjwa sita (6) walikua na ulemavu Daraja la Pili. Aidha, ununuzi wa vifaa vya kutengenezea miguu bandia na kiatu chake ulifanyika kwa walioathirika na Ukoma. Pia, Serikali imeendesha mafunzo kwa vijiji 24 vya Unguja na Pemba juu ya Elimu ya Ukoma ambapo jumla ya watu 1,280 (Unguja 805, Pemba 475) walihudhuria mafunzo hayo na watu saba (7) waligundulika na Ukoma. Vilevile, Serikali imeendesha mafunzo juu ya ugonjwa wa ukoma kwa watu 169 ambao ni jamaa za wagonjwa wa maradhi hayo. Elimu ya afya juu ya maradhi ya ukoma inaendelea kutolewa kwa wananchi Unguja na Pemba kupitia vyombo vya habari. 90

104 Katika hatua nyengine, vituo vitatu vya kutoa huduma za kujitunza vimeanzishwa ili wagonjwa wasiweze kupata ulevamu zaidi. Madhumuni ni kuwafundisha wagonjwa namna ya kujitunza na kujilinda na ulemavu na baadae waweze kujihudumia katika vikundi vyao Kuipandisha Daraja Hospitali ya Wete Katika jitihada za kuipandisha hadhi Hospitali ya Wete, Serikali imeiongezea majengo hospitali hiyo ikiwemo wodi mpya ya akina mama pamoja na jengo la huduma ya afya ya akili (Mental health Wing) na sehemu ya kuhifadhia maiti. Sambamba na hili, Serikali imefanya matengenezo ya wodi ya wanaume na kuiwekea samani. Vilevile, chumba cha kuhifadhia dawa na Kliniki ya watoto zimefanyiwa matengenezo. Aidha, hospitali imepatiwa mashine ya Ultrasound na mashine ya kupimia moyo (ECG). Kupatikana kwa mashine hizi pamoja na kupatikana kwa madaktari wawili (2) wa upasuaji kumeimarisha utoaji wa huduma katika hospitali hiyo Kuipandisha Daraja Hospitali ya Abdalla Mzee Pemba Katika azma ya kuipandisha daraja Hospitali ya Abdalla Mzee, Serikali imeendelea na mpango wake wa kuijenga upya hospitali hii ili iweze kutoa huduma bora na kuweza kufikia hadhi ya kuwa Hospitali ya Mkoa. Hatua iliyofikia kwa sasa ni kulipwa fidia kwa wote waliobomolewa nyumba zao ili kuwezesha kufanya upanuzi wa majengo. Jumla ya Shilingi Bilioni 1.2 zimelipwa kwa ajili ya fidia hizo. Wakandarasi wa Kampuni kutoka China tayari wameshawasili kuanza kazi ya ujenzi wa hospitali hiyo. Gharama za ujenzi huo zinatarajiwa kuwa ni Shilingi Bilioni

105 Hospitali ya Abdallah Mzee ikiendelea na ujenzi Michoro ya Jengo la hospitali ya Abdalla Mzee itakavyokuwa baada ya kumalizika kwa ujenzi wake Kuipandisha Daraja Hospitali ya Micheweni Serikali imeendelea na uimarishaji wa Hospitali ya Micheweni kwa lengo la kuifanya ifikie kuwa na hadhi ya Hospitali ya Wilaya. Hatua za awali za kujua mahitaji halisi ya majengo, wafanyakazi pamoja na vitendea kazi tayari zimefanyika. Kwa sasa Serikali imeweza kufanya upanuzi wa majengo ili kuboresha huduma katika hospitali hiyo ikiwemo wodi ya wazazi, chumba cha upasuaji na ujenzi wa maabara mpya na ya kisasa. 92

106 Makamu wa Pili wa Rais Mheshimiwa Balozi Seif Ali Iddi akishuhudia utiaji saini na kukagua ujenzi wa hospitali ya Micheweni - Pemba Kuipandisha Daraja Hospitali ya Kivunge Katika kuimarisha Hospitali ya Kivunge, Serikali imefanya matengenezo ya nyumba 12 za wafanyakazi, pamoja na chumba cha upasuaji na wodi mbili (2) za watoto. Vilevile, jengo jipya la wagonjwa wa nje (Out Patient Department) limejengwa ili kusaidia kupunguza msongamano ndani ya hospitali. Aidha, mashine za operesheni na ultrasound zimewekwa katika hospitali hiyo. Serikali kupitia Mradi wa HIPZ, imefanikiwa kuanzisha Kitengo cha Huduma za Dharura (Emergency Unit) kitakachotoa huduma za haraka kwa wagonjwa wanaohitaji huduma za dharura hospitalini hapo. Aidha, Serikali imeipatia hospitali hiyo incinerator kwa ajili ya kuchomea taka Kuimarisha Hospitali ya Makunduchi Katika jitihada za kuimarisha Hospitali ya Makunduchi, Serikali imejenga jengo jipya la kupokelea wagonjwa wa nje (outpatient department) pamoja na kukifanyia matengenezo chumba cha kuzalishia, wodi ya kina mama wajawazito, chumba cha matibabu ya meno pamoja na ununuzi wa vifaa vipya kwa ajili ya matibabu ya meno. 93

107 Makamu wa Pili wa Rais Mheshimiwa Balozi Seif Ali Iddi mara baada ya kulifungua jengo jipya la Wagonjwa wa nje katika hospitali ya Makunduchi Kuendelea Kuimarisha Huduma za Hospitali ya Mnazi Mmoja ili kufikia Hadhi ya Hospitali ya Rufaa Serikali kwa kushirikiana na Shirika la ICAP imefanya matengenezo makubwa katika maabara ya Hospitali ya Mnazimmoja. Matengenezo hayo yamehusisha idara zote muhimu ambazo ni microbiology, parasitology, haematology, biochemistry na blood transfusion. Matengenezo hayo yameifanya maabara hiyo kuwa katika kiwango kizuri cha utendaji ambacho kinalingana na maabara nyengine zilizo ndani ya nchi za Afrika mashariki. Jumla ya Shilingi milioni 300 zimetumika kwa ujenzi huo. Kutokana na matengenezo hayo hospitali inaweza kufanya vipimo 67 ukilinganisha na vipimo 30 ambavyo vilikuwa vikifanywa katika kipindi cha miaka mitano iliyopita na kuwezesha tiba ya maradhi kufanywa kwa ufanisi na usahihi. Aidha, huduma za histopathology kwa uchunguzi wa saratani zimeanza kutolewa na hivyo imewarahisishia wananchi wetu kupata huduma hizo hapa Zanzibar badala ya kuzifuata nje ya nchi. Vilevile, Maabara hiyo imeanza kutoa huduma ya uchunguzi wa maradhi ya kifua kikuu kwa kutumia mashine mpya ya kisasa (Gene expert) yenye uwezo mkubwa wa kugundua vimelea vya maradhi hayo kwa haraka na kubainika hata kama vimelea vya maradhi ni kidogo, hii imewezesha wagonjwa wa maradhi hayo kugundulika mapema na kupata tiba sahihi. Vilevile, hospitali imeanza kutoa huduma za uchunguzi wa maradhi na tiba za mfumo wa chakula (Gastro-enterology Endoscopic Services). Kitengo hiki kinaweza kuchunguza maradhi yote 94

108 yatokanayo na mfumo wa chakula na kupatiwa tiba sahihi kwa mujibu wa maradhi hayo. Pia, Serikali imeweza kuweka vifaa vya huduma nyengine za uchunguzi ikiwa ni pamoja na Laparascopy, CT scan, Fluoroscopy na Ultrasound kwa ajili ya uchunguzi wa maradhi mbalimbali. Aidha, huduma za macho zimeimarika kwa kuwekewa na kutumia vifaa vya kisasa vya uchunguzi kama vile slitlamp, A-P Scanner, darubini ya kuchunguza matatizo ya macho, kifaa cha kupima pressure ya macho pamoja na vifaa vya upasuaji wa macho. Sambamba na hayo, katika kuimarisha huduma za uchunguzi na matibabu ya maradhi ya moyo Serikali imeweza kununua mashine ya Echocardiography (ECG) na pia kupata daktari bingwa mzalendo wa maradhi ya moyo. Serikali imefanya matengenezo ya jengo la Kiwanda cha Dawa cha zamani ili kiweze kutoa huduma bora za mama na mtoto. Matengenezo hayo yamegharimu jumla ya Shilingi bilioni 18,643,200,000. Gharama hizi zinahusisha ujenzi, vifaa na mafunzo ya utumiaji wa vifaa. Aidha, Serikali imefanya matengenezo ya Vituo 19 vya Afya ya Msingi kwa Unguja na Pemba. Vilevile, Serikali imefanya ujenzi na uwekaji wa vifaa katika Kitengo cha Upasuaji wa Uti wa Mgongo (neorosurgical unit), jengo hilo tayari limeshaanza kutoa huduma. Ujenzi huo umefanywa kwa mashirikianao na Taasisi ya Neurosurgical Education and Development ya Hispania. Pia, Serikali inaendelea na ujenzi wa jengo jipya lenye wodi ya watoto ambayo inatarajiwa kuwa na vitanda 100 vya kulaza wagonjwa, kitengo kwa ajili ya wagonjwa mahututi pamoja na wagonjwa wenye matatizo ya figo. Rais wa Zanzibar Dkt. Ali Mohamed Shein akifungua Kitengo cha matibabu ya Uti wa Mgongo katika Hospitali ya Mnazi Mmoja 95

109 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein akikagua mashine za upasuaji katika Jengo jipya la Upasuaji wa Ubongo na Uti wa Mgongo (Neurosurgical Unit) katika Hospitali ya Mnanzi Mmoja Serikali imekifanyia ukarabati mkubwa Kitengo cha Wagonjwa Mahututi kwa kuwekewa vifaa vya kisasa vikiwemo mtambo wa kusambaza oxygen, uwekaji wa vipoza hewa, mechanical ventilater, Arterial blood gas analyser na electronic machines. Aidha, air vaccum imewekwa kwa wodi ya ICU, wodi ya wazazi na chumba cha upasuaji. Kitengo cha Wagonjwa Mahututi Kilichofanyiwa Matengenezo Makubwa katika Hospitali ya Mnazi Mmoja 96

110 Makamu wa Kwanza wa Rais Mheshimiwa Maalim Seif Sharif Hamad akikagua chumba cha Wagonjwa Mahtuti katika Hospital ya Mnazi Mmoja baada ya Kukifunguwa ikiwa ni miongoni mwa Shamrashamra za Miaka 51 ya Mapinduzi ya Zanzibar. Kwa upande wa Kitengo cha Meno (Dental Unit) cha Mnazi Mmoja Serikali imekifanyia matengenezo makubwa pamoja na uwekaji wa vifaa vipya vya kisasa. Vilevile, juhudi za uanzishwaji wa tiba kwa njia ya mawasiliano ya simu (Telemedicine) katika Hospitali ya Mnazi Mmoja tayari zimeanza kwa maradhi ya kawaida na ya upasuaji na uti wa mgongo. Hospitali pia, inatoa huduma za matatizo ya figo kwa wagonjwa. Katika kuhakikisha kuwa Hospitali ya Mnazi Mmoja inafikia hadhi ya kuwa hospitali ya rufaa, Serikali imefanikiwa kuongeza idadi ya madaktari wa kawaida (MD general) na kufikia 46 kati yao wazalendo 44 na wageni 2 kutoka Norway. Aidha, Serikali imeongeza idadi ya madaktari bingwa 44 kati yao 13 ni madaktari wazalendo na 31 ni wageni kutoka China, Cuba, Norway na Denmark. Vilevile, Serikali inawaendeleza madaktari 14 waliopo kuwa madaktari bingwa kwa maradhi ya saratani, maradhi ya watoto, maradhi ya kina mama, maradhi ya kawaida, daktari bingwa wa radiolojia, daktari bingwa wa maradhi ya mifupa (OT), upasuaji wa uti wa mgongo na maradhi ya macho. 97

111 Kwa sasa Hospitali ya Mnazi Mmoja inautaratibu wa kupokea madaktari bingwa kutoka Hispania na Uholanzi ili kutoa huduma za upasuaji wa mgongo na vichwa maji na upasuaji wa plastic surgery. Vilevile, Serikali ina makubaliano na Chuo Kikuu cha Hauckland cha Norway ya kuleta madaktari bingwa kufanya kazi na madaktari wazalendo. Sambamba na hayo, madaktari wa Zanzibar kutoka Hospitali ya Mnazi Mmoja nao hupata fursa ya kwenda Norway ili kufanya kazi katika hospitali ya chuo hicho. 6.3 MAJI Katika hatua za kuendeleza upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama kwa wananchi, Serikali inaendelea kutekeleza mipango mbalimbali ya kuwapatia wananchi maji safi na salama katika maeneo yote ya mijini na vijijini. Suala hili limepewa kipaumbele katika Ilani ya Uchaguzi ya CCM sambamba na mikakati ya Serikali ya kukuza uchumi na kupunguza umasikini Kuzifanyia Mapitio Sera na Sheria ya Maji Serikali inaendelea kuzifanya mapitio Sera na Sheria ya Maji ili kuondoa mapungufu yaliyomo na kuzifanya Sera na Sheria hizo kuendana na wakati na kwa mujibu wa mahitaji ya sasa na baadae. Kukamilika kwa Sheria na Sera ya maji kutaimarisha utoaji na upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama mijini na vijijini Kuendeleza Usambazaji wa Maji Safi na Salama Unguja na Pemba Usambazaji wa huduma ya maji safi na salama umeendelea kukua kutoka asilimia 75 mwaka 2010 hadi kufikia asilimia 87 mwaka kwa maeneo ya Mijini na kutoka asilimia 60 mwaka 2010 hadi kufikia asilimia 70 mwaka kwa upande wa vijijini. Jitihada hizo zimefanywa kupitia Serikali kuu, Wadau wa Maendeleo pamoja na nguvu za Wananchi. Aidha, Serikali kwa kushirikiana na Washirika wa Maendeleo imetekeleza mradi mkubwa wa Usambazaji Maji Safi na Usafi wa Mazingira ambao upo katika hatua ya majaribio. Kukamilika kwa mradi huu kutaongeza uzalishaji wa maji kwa lita milioni 17.6 kwa siku. Mradi umechimba visima 41, umejenga matangi 17 yenye ujazo wa viwango tofauti na ulazaji wa mabomba yenye urefu wa kilomita katika Mikoa yote ya Unguja na Pemba kama ifuatavyo:- Ujenzi wa matangi nne (4) ya Matemwe (Lita 3, 000,000), Nungwi (Lita 3, 000,000), Machui (Lita 1, 500,000) na Tunguu (Lita 1, 200,000). 98

112 Uchimbaji na ujenzi wa visima tisa (9) vya uzalishaji pamoja na kujenga vibanda vya kuendeshea mitambo na kufunga pampu. Uchimbaji na ulazaji wa mabomba kwa maeneo yote yaliokubaliwa ya Machui (kilomita 13.1), Dunga/Tunguu (kilomita 7.8) na Matemwe (kilomita 13.9) na Nungwi kilomita (5.8). Ujenzi wa Matangi saba (7) ambayo ni Ndagoni (Lita 1,000,000), Vikunguni (Lita 300,000), Vitongoji Ali Khamis Camp (Lita 300,000), Kambini (Bahanasa) (Lita 1,000,000 na Lita 300,000) Wambaa (Lita 500,000) na Mizingani (Lita 300,000). Uchimbaji wa visima 14 vya uzalishaji pamoja na kujenga vibanda vya kuendeshea mitambo na kufunga pampu. Ulazaji wa mabomba kwa maeneo yote yaliopangwa ya Wambaa (kilomita 10.2), Mizingani (kilomita 25.8), Ndagoni (kilomita 27.3), Vitongoji (kilomita 29.5) na Kambini (kilomita 41.3). Ujenzi wa matangi ya chini (ground tanks) ya Wete Taifu (Lita 2,500,000), Wete Mtemani (Lita 800,000), Chake-Chake (Lita 3,000,000) na Mkoani (Lita 800,000) pamoja na ujenzi wa chemba za matangi haya zimo katika hatua za mwishoni. Ujenzi wa matangi ya juu (elevated tanks) ya Chake-Chake (Lita 250,000) na Mkoani (Lita 250,000) unaendelea. Uchimbaji wa visima 18 vya uzalishaji tayari umekamilika. Ulazaji wa mabomba kwa maeneo yote yaliokubaliwa ya Chake-Chake (kilomita 31.2), Wete (kilomita 31.9) na Mkoani (kilomita 17.6) umekamilika. 99

113 Kazi ya Ulazaji wa Mabomba na Ujengaji wa Matangi ya Kuhifadhia Maji katika Maeno mbalimbali nchini Kupunguza kiwango cha Upotevu wa Maji Serikali inaendelea kuhamasisha wananchi kuwa na mwamko katika kuchangia huduma za maji ili ziwe endelevu na kutoa kipaumbele katika kulinda, kuhifadhi na kutunza rasilimali maji. Pia, Serikali inaendelea kufunga mita za maji katika makaazi ya wananchi wake ambapo jumla ya mita 2,581 zimefungwa. Kati ya mita hizo, mita 1,188 zimefungwa kwa wateja wa majumbani na mita 1,393 zimefungwa kwa wateja wa biashara. Ufungaji huo unalenga kupunguza kiwango cha upotevu wa maji na kuchangia huduma ya maji kwa mujibu wa matumizi. Vilevile, Serikali imeendelea kutoa elimu kwa umma mijini na vijijini kupitia vyombo vya habari pamoja na kufanya makongamano ili kushajiisha wananchi katika suala la uchangiaji wa huduma ya maji. Sambamba na hayo, zoezi la utambuzi wa mabomba yanayovuja (Leakage survey) umefanyika katika Mkoa wa Mjini Magharibi na maeneo yote yaliyobainika yameweza kufanyiwa matengenezo. Kazi hizo zimefanyika kupitia mafunzo ya vitendo kazini kupitia wataalamu wa JICA katika Mradi wa kuijengea uwezo ZAWA. Serikali ililazimika kuchukua maamuzi magumu ya kuendesha operesheni ya kuwahamisha waliojenga katika eneo la chemchem ya Mwanyanya na kuwatahadharisha wengine waliotaka 100

114 kuvamia katika eneo hilo na maeneo mengine ambayo yanakabiliwa na uharibifu mkubwa wa kimazingira ikiwemo ujenzi wa nyumba, ukataji wa miti na uchimbaji wa mchanga Kukamilisha Awamu ya Pili ya Mradi wa Usambazaji Maji Safi na Salama katika Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja Utekelezaji wa Mradi wa Maji wa Mkoa wa Mjini Magharibi Awamu ya Pili umekamilika kwa ujenzi wa matangi makubwa mawili maeneo ya Kinuni na Dole. Aidha, visima vitano (5) vimechimbwa katika maeneo ya Kizimbani na Msikiti Mzuri. Shughuli za ulazaji wa mabomba yenye urefu wa kilomita 21 zimefanyika katika maeneo ya Kinu Moshi hadi Tangi la Dole kutoka Dole kuelekea Bububu na kutoka Chunga kuelekea Kinuni, Magomeni hadi Kiembe Samaki. 6.4 MAKAAZI Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi imeiagiza Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kusimamia utekelezaji wa Sera ya Taifa ya Nyumba na kuandaa Sheria ya Condominium ili kuwezesha wananchi waliopangishwa katika nyumba za maendeleo mijini na vijijini kuuziwa sehemu ya majengo hayo. Serikali imekamilisha uandaaji wa Sheria ya Condominium na kuunda Bodi ya kusimamia utekelezaji wa Sheria hiyo. Aidha, Serikali kwa kuzingatia agizo hilo imeendelea kusimamia utekelezaji wa Sera ya Taifa ya Nyumba na kupitisha Sheria ya Shirika la Nyumba la Zanzibar ya mwaka Pia, Serikali inaendelea na zoezi la kuwashajiisha Wawekezaji kuwekeza katika Sekta ya Nyumba. Vilevile, Serikali inaendelea kuufanyia mapitio Mpango Mkuu wa Mji wa Zanzibar (Master Plan) ili kutenga maeneo maalum ya ujenzi wa nyumba za ghorofa na kupunguza tatizo la uhaba wa ardhi Kukamilisha Ujenzi wa Nyumba ya Maendeleo Bambi Serikali imekamilisha ujenzi wa jengo moja la Nyumba za Maendeleo Bambi (Mpapa) ambapo nyumba 24 zimekabidhiwa kwa wananchi wakati wa Maadhimisho ya Sherehe za miaka 50 ya Mapinduzi ya Zanzibar. 101

115 Jengo la nyumba ya Maendeleo Bambi Uendelezaji wa Mamlaka ya Mji Mkongwe Mji Mkongwe wa Zanzibar ni hazina kubwa na kivutio cha historia ya Zanzibar. Kwa kutambua hilo, Serikali kwa kushirikiana na watu binafsi na Mashirika ya Kimataifa inaendelea kuulinda, kuihifadhi na kutumika kama kivutio cha utalii na kubakisha dhana ya urithi wa dunia kwa kukarabati majengo yaliyomo bila kubadilisha uhalisia wake. Mamlaka ya Mji Mkongwe imefanya ukaguzi wa nyumba zilizo katika hali mbaya ya uchakavu na kuziingiza katika Mfumo wa Kuhifadhia Taarifa (database system) sambamba na kuwashajiisha wapangaji na wenye nyumba binafsi kufanya matengenezo mara tu athari zinapoanza kujitokeza. Ukaguzi huo umegundua kwamba majengo 42 yapo katika hali mbaya na majengo 267 yamefanyiwa matengenezo. Aidha, Mpango wa Matumizi Endelevu wa Eneo la Mji Mkongwe wa 1994 unaendelea kufuatwa kwa azma ya kuendeleza uhifadhi wa mji huu. Wakati huo huo, Mamlaka inaendelea kushirikiana na Jumuiya ya Miji ya Urithi wa Dunia (Organization of World Heritage City). Katika kusimamia utekelezaji wa Mpango wa Matumizi ya Magari na Vyombo vya Moto (Traffic plan) ndani ya Eneo la Mji Mkongwe, Serikali imetangaza utaratibu wa utumiaji barabara kwa njia zitakazotumika upande mmoja (one way road), njia zitakazotumika pande mbili (two way roads), njia zitakazofungwa, maegesho ya magari, pamoja na sehemu zisizoruhusiwa kupitwa (No entry) na mikokoteni na vyombo vya moto. 102

116 SEHEMU YA SABA 7.0 MAENEO MENGINE YA KIPAUMBELE 7. 1 Utamaduni na Michezo Kama inavyofahamika kuwa Utamaduni ni moja katika mambo muhimu katika Taifa lolote Duniani, Ilani ya Chama cha Mapinduzi imeielekeza Serikali kudumisha na kuendeleza mila na silka za jamii ya Zanzibar Kuandaa Sera ya Utamaduni na Michezo Serikali imeifanyia mapitio Sera ya Utamaduni ikiwa ni muongozo kwa taasisi zinazosimamia utamaduni ili kwenda na wakati kwa kuihusisha Sekta ya Utalii na Utamaduni. Aidha, katika kuufanya utamaduni uwe na tija zaidi, Serikali imekamilisha mchoro wa ramani ya utamaduni katika shehia za Unguja na Pemba. Pia, utafiti wa Urithi wa Utamaduni Usioshikika umekamilika katika mikoa yote ya Zanzibar na hatimaye kuhifadhiwa na kutangazwa kimataifa kwa kuingizwa katika orodha ya UNESCO ya Utamaduni zilizohifadhiwa. Urithi wa utamaduni usioshikika ni Kumbukumbu za Utamaduni zisizo na umbo linalogusika wala kushikika kama ufundi na ustadi wa utengenezaji wa vifaa vya kiasili, uhunzi, ubunifu wa sanaa, elimu ya tiba asilia, lugha, maigizo, matamasha, sherehe za kimila, nyimbo, imani, matambiko, mila, simulizi na itikadi Kusimamia Utekelezaji wa Sera na Sheria za Michezo na Utamaduni Serikali imezifanyia mapitio Sera ya Utamaduni na Sera ya Michezo kwa lengo la kuzifanyia marekebisho. Pia, Serikali imetoa mafunzo kwa wasanii wa kazi za mikono ili kuweza kuwahamasisha wasanii hao kuzalisha kazi zilizo bora zaidi. Vilevile, Mabaraza ya Michezo ya Wilaya zote za Zanzibar yameimarishwa kwa kupatiwa mafunzo juu ya namna ya kuendesha na kusimamia shughuli za michezo katika ngazi za Wilaya. Aidha, Serikali imekamilisha uandaaji wa Sheria ya Baraza la Sanaa na Sensa ya Filamu na Utamaduni, ambayo imeunganisha Bodi ya Sensa na Baraza la Sanaa ili kuleta ufanisi zaidi katika uimarishaji wa utamaduni nchini Kujenga Kiwanja cha Kisasa cha Michezo ya Ndani Serikali imefanya matayarisho ya ujenzi wa kiwanja cha kisasa cha michezo ya ndani katika Uwanja wa Amaan kwa kuandaa mchoro wa ujenzi wa kiwanja hicho kitakachotoa fursa zaidi kwa vijana kushiriki katika michezo hiyo ikiwemo kuogelea, mpira wa vinyoya na mpira wa meza. 103

117 Vilevile, ukumbi wa Zanzibar Budocan uliojengwa ndani ya Uwanja wa Amaan kwa kushirikiana na Serikali ya Japan umeanza kutumika kwa michezo ya Judo, Karati na michezo mingine ya ndani inayolingana na hiyo Kukamilisha Ujenzi wa Kituo cha Michezo Dole Serikali imejenga Kituo cha Michezo Dole ambacho kinatumika ili kukuza vipaji vya michezo kwa vijana wa Zanzibar. Vilevile, viwanja viwili (2) vya michezo vimeanzishwa katika kituo hicho ambapo zaidi ya vijana 3,000 wamepata mafunzo ya michezo na kupata fursa za kushiriki mashindano ya ndani na nje ya nchi kama vile SAMSUNG Youth Games Ujenzi wa Uwanja Mpya wa Michezo Serikali imeamua kuujenga upya Uwanja wa Mao Tse Tung uliopo mjini Unguja ili uweze kutumika kwa shughuli za michezo na sherehe za kitaifa. Aidha, michoro ya awali ya ujenzi huo imekamilika na kazi za ujenzi zimeanza. Serikali ya Watu wa China ndio inayosaidia ujenzi wa Uwanja huo Matengenezo ya Kuboresha Uwanja wa Gombani Pemba Serikali imeufanyia marekebisho uwanja wa Gomabani Pemba ili kuuwezesha uwanja huo kukidhi haja ya mashindano ya kimataifa ya mpira wa miguu. Aidha, matengenezo ya taa za uwanja huo yamekamilika ambayo yanauwezesha uwanja kutumika hata wakati wa usiku. Vilevile, Serikali imekamilisha ujenzi wa njia ya kukimbilia running track maarufu kama tatan ili kutoa fursa ya michezo ya riadha kufanyika kwa ufanisi mkubwa. Pia, kwa kushirikiana na Serikali ya Japan, Serikali imejenga kiwanja cha michezo ya ndani katika Uwanja wa Gombani Pemba ambacho kinatumika kwa michezo ya mpira wa meza, mpira wa wavu, mpira wa vinyoya, judo, karati na michezo mengine ya ndani. 104

118 Uwanja wa Gombani - Pemba Uliowekewa Nyasi Bandia Kuendeleza na Kuimarisha Vipaji vya Wanamichezo Serikali imeviwezesha vyama vya michezo kuandaa mashindano ya ndani kwa vilabu vyao pamoja na kushiriki katika mashindano ya kitaifa na kimataifa kwa michezo ya mpira wa miguu, riadha, judo, karati, mpira wa mikono, kunyanyua vitu vizito, mpira wa wavu na michezo mengine. Pia, hatua mbalimbali zimechukuliwa za kuendeleza na kuimarisha vipaji vya wanamichezo wetu kwa kuwapatia mafunzo ya utawala na uendeshaji kwa viongozi 20 na walimu wa michezo 150. Vilevile, Serikali imeendesha semina za mafunzo kwa Makatibu, Wenyeviti na Makocha kutoka Wilaya zote ili kuinua viwango vya michezo nchini. Timu ya Taifa ya Zanzibar (Zanzibar Heroes) imeshiriki katika michezo ya VIVA WORLD CUP nchini Kurdistan na katika mashindano ya Senior Challenge Cup yanayofanyika kila mwaka ambapo kwa mwaka 2012 timu ilishika nafasi ya tatu katika mashindano hayo. Pia, Timu za vijana chini ya umri wa miaka 13 na ile ya baina ya miaka za Mpira wa Miguu zimeshiriki katika mashindano ya Vituo vya Academia ya Michezo (Olympafrica Centres) vya Afrika Mashariki na Kati yaliyofanyika nchini Burundi na kufanikiwa kuwa Bingwa na kutunukiwa kombe lijulikanalo kwa jina la Daimler Cup 2010/2011. Kwa upande wa mchezo wa riadha, Serikali imewawezesha wanaridha 20 kushiriki katika mashindano ya vijana ya kitaifa na kimataifa yaliyofanyika Tanzania Bara na Botswana. Aidha, 105

119 Serikali imewawezesha wanamichezo mbalimbali kushiriki katika mashindano ya All Africa Games yaliyofanyika Maputo Msumbiji. Pia, timu ya Watu Wenye Ulemavu wa akili ilishiriki katika mashindano ya Special Olympic nchini Ugiriki na Kibaha Tanzania Bara. Kwa upande mwengine, Serikali imeziwezesha timu za Taifa za Judo na Riadha kushiriki Mashindano ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati yanayofanyika kila mwaka ikiwemo ya Zanzibar. Vilevile, timu za mpira wa mikono zimeshiriki katika Mashindano ya Kombe la Challenge, Nairobi na Mashindano ya Shirikisho la Michezo kwa Skuli za Sekondari, Afrika ya Mashariki (FEASSA) yaliyofanyika nchini Uganda Kuendeleza Kudumisha Mila, Silka na Maadili Mema ya Wazanzibari Serikali imechukua hatua za kuzikagua kazi za sanaa kwa lengo la kulinda na kuhifadhi mila na silka za Wazanzibari. Vilevile, imeandaa Kamusi ya Kipemba, Kimakunduchi na Kitumbatu kwa lengo la kupelekea wananchi kuzitumia Kamusi hizo ili kulinda na kuhifadhi utamaduni wa Kizanzibari. Pia, Bodi ya Sensa ya Filamu imefanya utafiti juu ya suala zima la maadili katika Wilaya za Zanzibar kwa lengo la kuweka mikakati ya kuendeleza juhudi za kulinda, kuhifadhi na kudumisha mila, silka, na maadili mema ya Wazanzibari. Matokeo ya utafiti huo yamechapishwa katika kitabu kiitwacho Hazina Inayopotea, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mheshimiwa Dkt. Ali Mohamed Shein akiwa na Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Ali Hassan Mwinyi wakiangalia watoto wakicheza ngoma za utamaduni Mangapwani Unguja 106

120 Aidha, Serikali kupitia Bodi ya Sensa ya Filamu imefanya uhakiki wa Matamasha, Matangazo ya Kibiashara, Video za Nyimbo, tenzi zenye maudhui mbali mbali na filamu tofauti katika maduka ya kukodishia kanda Unguja na Pemba. Bodi pia, imekagua vikundi vya ngoma, michezo ya kuigiza jukwaani, tenzi na mashairi ya kughani ili kuhakikisha mila, silka na utamaduni wa Kizanzibari hauathiriwi. Aidha, Serikali imejenga Studio ya kisasa ya kurekodia filamu na muziki kwa lengo la kuwapunguzia gharama za kurekodia kazi za wasanii wa Zanzibar. 7.2 VYOMBO VYA HABARI Vyombo vya habari vina jukumu kubwa la kuhabarisha, kuelimisha, kuhamasisha na kuburudisha jamii juu ya masuala mbalimbali ya kiuchumi, kijamii na kisiasa. Serikali imeweka mikakati na kutekeleza hatua mbalimbali za kukuza na kuendeleza uhuru wa vyombo vya habari nchini Kusimamia Utekelezaji wa Sera ya Habari na Kuendeleza Uhuru wa Vyombo vya Habari Serikali imeweza kufanya mageuzi makubwa katika kusimamia na kuendeleza vyombo vya habari kwa kuvipa uhuru na haki ya kuhoji, kutafuta, kupokea na kuchapisha habari na maoni kwa kuzingatia taratibu na sheria zilizopo. Kwa kutekeleza lengo hilo na kuzingatia demokrasia ya ushirikishwaji wa umma, Serikali imetoa fursa ya kuanzishwa kwa vyombo vya habari nchini na kutoa fursa kwa wananchi kuvitumia vyombo hivyo kwa maslahi yao na Taifa kwa ujumla. Hivi sasa jumla ya Redio tisa (9) za FM na Televisheni sita (6) zimeanzishwa katika kipindi cha 2010 hadi. Vyombo hivyo ni pamoja na Mtegani FM, Voice of Istiqama FM, Tumbatu FM, Mkanyageni FM, Marhaba FM, Bahari FM, Mkoani FM, Assalam FM, ABM FM, ZUKU Satallite TV, Star Times, Zenj TV, CCTV, Coconut TV na Azam TV. Aidha, idadi ya Magazeti na Majarida yaliyosajiliwa na kufanyakazi Zanzibar imeongezeka kutoka matano (5) mwaka 2010 hadi 50 mwaka. Pia, usambazaji wa Magazeti ya Serikali umeongezeka kwa kuwafikia wasomaji wengi zaidi katika mikoa yote ya Zanzibar na mikoa 14 ya Tanzania Bara Kusimamia Utekelezaji wa Muongozo, Kanuni na Sheria ya Vyombo vya Habari Serikali imeandaa na kusimamia utekelezaji wa Sheria ya Vyombo vya Habari, Kanuni na Miongozo kwa lengo la kuleta ufanisi katika mageuzi ya mfumo wa utangazaji kutoka Analogi kwenda Dijitali. Aidha, miongozo imetolewa kwa vyombo vya habari kuzingatia maadili ya uandishi wa habari na kuwajibika kwa jamii pamoja na kuheshimu haki za faragha kupitia semina 107

121 na mikutano. Vilevile, mafunzo ya umuhimu wa kuheshimu uhuru wa vyombo vya habari yametolewa kwa kutumia vyombo vya habari vya Serikali na watu binafsi. Pia, utaratibu wa ufuatiliaji wa matangazo na vipindi vya vituo vya redio na TV (Monitoring System) umeanzishwa na unafanyakazi kwa ufanisi ambapo hivi sasa vipindi vyote vinarikodiwa, kuhifadhiwa na kufuatiliwa. Sambamba na hayo, Sheria Namb. 4 ya mwaka 2013 ya kuunda Shirika la Utangazaji la Zanzibar (ZBC) imepitishwa na imeanza kufanyakazi Kuendeleza Mafunzo kwa Watendaji wa Vyombo vya Habari na Utangazaji Serikali imetoa mafunzo ya kuwaendeleza wanahabari mbali mbali ili waweze kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi mkubwa. Katika kulifanikisha hilo, waandishi 114 (wanawake 78 na wanaume 36) wameweza kupatiwa mafunzo katika ngazi tafauti zikiwemo PhD 4, Shahada ya Pili 13, Shahada ya Kwanza 20, stashahada 51 na Cheti 26. Vilevile, taaluma mpya ya teknolojia ya dijitali imetolewa kwa mafundi, watayarishaji vipindi, wapiga picha na viongozi wa vituo vya utangazaji vya Serikali na Binafsi vilivyopo Zanzibar Kuviimarisha Vyombo vya Habari ikiwemo ZBC TV na ZBC Redio Serikali imeviimarisha Vyombo vya Habari vya Zanzibar kwa kuvinunulia vifaa mbalimbali vya kisasa vinavyotumia teknolojia ya digitali. Studio za Televesheni Unguja na Pemba zimefungwa vifaa vipya vya kukusanyia na kurushia matangazo vyenye uwezo wa kuonekana na kusikika ndani na nje ya Zanzibar. Vifaa hivyo vya digitali vina thamani ya Shilingi Bilioni Aidha, mitambo ya digitali imefungwa katika vituo vya kurushia matangazo vilivyoko Rahaleo, Masingini, Muyuni, Nungwi, Mizemiumbi, Mkanjuni na Bungala kwa lengo la kuwawezesha wananchi kupata huduma mpya za matangazo hayo. Mitambo hiyo imegharimu jumla ya Shilingi Bilioni

122 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mheshimiwa Dkt. Ali Mohamed Shein akifungua Kituo cha kurushia matangazo ya Televisheni kwa mfumo wa Digitali kilichopo Rahaleo Matangazo ya Redio ya ZBC yameimarishwa kwa kuhamisha Mnara wa Masafa ya Kati (Medium Wave) kutoka Chumbuni kwenda Bungi ambayo imegharimu Shilingi 1, 496,600, 000. Uhamishwaji wa mnara huo pia unarahisisha utuaji wa ndege zinazoingia na kutoka nchini kwa usalama zaidi. Aidha, Ofisi, Studio na nyumba mbili (2) za kisasa za wafanyakazi wa familia nne (4) zimejengwa katika eneo hilo la Bungi ili kuimarisha utendaji mzuri wa kazi. Vilevile, kazi ya ukarabati wa mnara wa mawimbi mafupi (Short Wave) umefanyika kwa ushirikiano na Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China, ambapo Shilingi Bilioni 2,440,000,000 zimetumika. Ukarabati huo umeongeza nguvu za kusikika matangazo ya ZBC hadi nje ya Bara la Afrika Ujenzi wa Studio ya Wasanii Serikali imekamilisha mradi wa ujenzi wa studio ya kisasa ya kurikodia nyimbo na michezo ya kuigiza kwenye jengo la zamani la Utangazaji la Sauti ya Tanzania Zanzibar baada ya jengo hilo kufanyiwa matengezo makubwa. Tayari Serikali imenunua na kufunga vifaa vipya kwa ajili ya studio hiyo ambavyo vimegharimu jumla ya shilingi 291,534,000. Vifaa hivyo ni pamoja na Sony xdcamex, Camera tripods na Track dolly, Camera cran, Lens fish eye, Digital video mixer, Digital audio mixer na Power amplifier. 109

123 Kituo cha Kurushia Matangazo ya Redio pamoja na Mnara wa Masafa ya Kati viliopo Bungi - Zanzibar Kuendelea Kukiimarisha Chuo cha Uandishi wa Habari Serikali imekiimarisha Chuo cha Uandishi wa Habari kwa kuweka vifaa pamoja na kuajiri walimu wenye ujuzi ili kuweza kutoa wahitimu wenye uwezo wa kuzungumza na kuandika lugha fasaha katika vyombo wanavyovifanyia kazi. Idadi ya wanafunzi imeongezeka kutoka 75 mwaka 2010 hadi kufikia 180 kwa mwaka kwa ngazi ya cheti na stashahada. Vilevile, Chuo kimeweza kutengeneza nyaraka mbalimbali za kitaalamu ikiwemo Kitabu cha Miongozo wa Shughuli za Chuo (Prospectus), Mpango Mkakati (Strategic Plan) na Vipeperushi. Pia, Chuo kimeweza kuanzisha mafunzo ya lugha ya kichina kwa kushirikiana na Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China. Sambamba na hayo, Chuo kimekuwa na ushirikiano wa karibu na Redio ya Kimataifa ya Deutsche Welle (DW) ya Ujerumani ambayo imekuwa ikisaidia kuwajengea uwezo walimu na wanafunzi kwa kuwapatia mafunzo mbalimbali. Aidha, Chuo kimeimarishwa kwa kupatiwa eneo kwa ajili ya ujenzi wa jengo jipya la chuo katika eneo la Kilimani, mjini Unguja. 110

124 Moja ya Majengo Manne ya Chuo cha Uandishi wa Habari yaliyoanza kujengwa katika Eneo la Kilimani Mjini Zanzibar Kusimamia na Kudhibiti Uingizaji wa Vifaa vya Utangazaji Serikali imeendelea kuchukua juhudi za kukabiliana na hali ya ongezeko la uingizwaji wa vifaa vya utangazaji vya teknolojia ya analogia ambavyo havitumiki tena katika nchi nyingi. Ili kudhibiti Zanzibar isigeuzwe jaa la kutupia vifaa hivyo, mikakati imeandaliwa ya kuzuia uingiaji wa vifaa hivyo sambamba na mkakati wa mageuzi ya teknolojia ya Utangazaji kutoka analogia kwenda digitali. Aidha, semina, makongamano na warsha zimetolewa kwa wafanyabiashara ili kuwapa uelewa wa hasara ya kuendelea kuagiza vifaa vya utangazaji vya analogia kwa ajili ya kutunza mazingira na matumizi ya wananchi. Serikali pia imekuwa ikirusha vipindi maalumu kupitia vyombo vya habari vya kuwafahamisha wananchi athari za mageuzi ya teknolojia ya utangazaji wa digitali na matumizi makubwa ya nishati ya umeme kwa kutumia televisheni za analogia. Vilevile, Serikali imetoa miongozo ya utumiaji wa vifaa vya kupokea matangazo ya digitali ikiwa ni pamoja na kufanya semina elekezi kwa Watendaji Wakuu na Wamiliki wa Vituo vya Utangazaji nchini juu ya changamoto za digitali kupitia Mkakati wa Mawasiliano (Communication Strategy for Analogy to Digital Migration) sambamba na Mkakati wa Mageuzi ya Teknologia ya Utangazaji kutoka analogia kwenda digitali (Analogy to Digital Migration Strategy, 2011-). Pia, vikao 111

125 vya mashirikiano kati ya TCRA na Tume ya Utangazaji Zanzibar vimefanyika kwa lengo la kuzungumzia mikakati ya kudhibiti uingizaji wa vifaa vikongwe vya analogia Mradi wa E-Government Kwa lengo la kuimarisha huduma za mawasiliano Serikalini, Serikali imeanzisha mradi wa e- government mwezi Januari Hadi hivi sasa, jumla ya majengo 86 ya Serikali yameunganishwa katika mtandao huo na tayari yameanza kupata huduma ya internet bila ya malipo. Aidha, Serikali imo katika maandalizi ya kuiunganisha Zanzibar na Tanzania Bara kupitia Mkonga wa Taifa na ule wa Kimataifa. 7.3 MAJANGA NA HUDUMA ZA UOKOZI Katika jitihada za kukabiliana na maafa, Serikali imekamilisha utungaji wa Sera ya Kukabiliana na Maafa ya mwaka 2011 pamoja na Sheria ya Kukabiliana na Maafa ya mwaka ambazo zinatoa miongozo katika shughuli za kukabiliana na maafa na majanga pamoja na kutoa huduma za kibinadamu kwa waathirika. Aidha, Serikali imeandaa nyaraka za Muongozo wa Ufuatiliaji na Tathmini ya Sera, Muongozo wa Taifa wa Uendeshaji wa Sera ya Kukabiliana na Maafa, pamoja na Mpango wa Kujiandaa na Kukabiliana na Maafa Zanzibar na Utafutaji wa Rasilimali za Kukabiliana na Maafa. Vilevile, Serikali imeandaa mipango ya kukabiliana na maafa ya Wilaya tano ambazo ni Mjini, Magharibi, Kaskazini A, Micheweni na Wete. Pia, elimu ya kukabiliana na maafa kwa ajili ya kujenga uelewa juu ya majanga na maafa imetolewa kwa makundi mbalimbali Unguja na Pemba ikiwa ni pamoja na Waandishi wa Habari, Wanafunzi, Watu wenye Ulemavu na Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi. Serikali kupitia Idara ya Kukabiliana na Maafa inaendelea kutoa elimu kupitia kipindi kinachorushwa na ZBC redio kila siku ya Jumatatu na kuanzisha Tovuti na Jarida la TUKABILIANE NA MAAFA linalotoka kila baada ya miezi mitatu Kuanzisha na Kuimarisha Kamati za Maafa kwa Ngazi ya Taifa, Wilaya na Shehia Serikali imeanzisha Kamati 277 za Kukabiliana na Maafa katika ngazi ya Shehia Unguja na Pemba pamoja na kuzipatia mafunzo ya msingi ya kukabiliana na maafa. Kamati hizo ni sawa na asilimia 82 ya Shehia zote zilizopo Zanzibar. Aidha, Kamati za Maafa za Wilaya na Shehia Unguja na Pemba zimefanyiwa Makongamano, Warsha na Semina ili kuzijengea uwezo wa kujikinga na kukabiliana na maafa katika maeneo yao. Vilevile, Serikali inaendelea na kutoa huduma za 112

126 kibinaadamu kwa wahanga waliofikwa na maafa katika maeneo mbalimbali nchini kupitia Kamati zao. Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mheshimiwa Dkt. Ali Mohamed Shein akikagua Maeneo yaliyoathrika Kutokana na Maafa ya Mvua zilizonyesha Mwezi Mei,. Baadhi ya Wajumbe wa Sekreatrieti ya Kamati Maalum ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, walipotembelea maeneno yaliyofikwa na mafuriko kwa lengo la kuwafariji wananchi walioathirika na maafa hayo. 113

127 Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais ambaye pia ni Katibu wa Kamati ya Maafa Kitaifa akipokea misaada baada ya Maafa yaliyosababishwa na Mvua zilizonyesha Mwezi Mei, Kuimarisha Vikosi vya Uokozi Wakati wa Maafa Serikali imeendelea kushajiisha wananchi kuanzisha vikosi vya uokozi katika maeneo yao ili viweze kukabiliana na maafa. Aidha, Serikali inaendelea kuiwezesha Jumuiya ya Uzamiaji na Uokozi ya Zanzibar kwa kuipatia elimu ya kukabiliana na maafa na vifaa wakati wa matukio. Jumuiya hiyo inajumuisha vikosi vya kijamii vya uzamiaji na uokozi Kuimarisha Kikosi cha Zimamoto na Uokozi Serikali imeendelea kukiimarisha Kikosi cha Zimamoto na Uokozi kwa kununua gari nne (4), kati ya hizo gari mbili (2) za kuzimia moto na mbili (2) kwa ajili ya shughuli za utawala. Aidha, Kikosi kimepatiwa zana na vifaa vya kisasa vya uokozi na kuzimia moto na kuvisambaza katika vituo vyake vyote Unguja na Pemba. Hali ambayo imekiwezesha Kikosi kutoa huduma zake kwa ufanisi. Vilevile, Serikali imeendelea kuwajengea uwezo watendaji wake kwa kuwasomesha katika fani ya zimamoto na fani tofauti katika ngazi mabalimbali ndani na nje ya nchi. 114

128 Gari ya Kikosi cha Uokozi na Zimamoto katika Uwanja wa Ndege wa Zanzibar Serikali pia imeweza kusogeza huduma za zimamoto kwa wananchi kwa kila Wilaya za Unguja na Wilaya tatu (3) za Pemba (Mkoani, Wete na Chakechake) na kuanza kutoa huduma katika Bandari ya Malindi kwa Unguja na Mkoani kwa Pemba. Aidha, Kikosi kimefanikiwa kukuza uhusiano na mashirikiano ya namna ya kukabiliana na majanga mbalimbali kwa kushiriki katika vikao mbali mbali vya Afrika Mashariki DAWA ZA KULEVYA Kusimamia Utekelezaji wa Sheria ya Udhibiti wa Dawa za Kulevya Katika kusimamia utekelezaji wa Sheria ya Udhibiti wa Dawa za Kulevya, Serikali kupitia Tume ya Kitaifa ya Kuratibu Udhibiti wa Dawa za kulevya imeweza kuandaa Mpango Maalum (Road Map) wa utekelezaji wa Sheria ya Dawa za Kulevya ambapo uliwashirikisha wadau kutoka taasisi mbalimbali za Serikali na zisizo za Serikali ili kuhakikisha kwamba michango mbalimbali inatolewa kudhibiti uingizaji, usafirishaji, usambazaji na matumizi ya Dawa za Kulevya. Serikali imefanya vikao vya Kamati ya Kitaaluma ya Kupambana na Dawa za Kulevya na wadau wengine kwa lengo la kujadili njia mbalimbali za kuendeleza mbele mapambano juu ya udhibiti wa Dawa za Kulevya. Vilevile, Serikali imeandaa Sera ya Dawa za Kulevya na kufanya mikutano 115

129 na vyombo vya kusimamia sheria (Law Enforcement Agency- LEA) ili kukuza mashirikiano na vyombo hivyo katika kudhibiti mapambano ya Dawa za Kulevya Kushirikiana na Asasi za Kijamii Serikali imeweza kutoa taaluma kupitia taasisi mbalimbali kama vile sehemu za kazi, Skuli na Shehia mbalimbali za Unguja na Pemba kuhusu athari za matumizi ya dawa ya kulevya. Aidha, vipindi mbalimbali vya kuelimisha jamii juu ya athari za dawa za kulevya vimerushwa kupitia vyombo mbalimbali vya habari vya ndani na nje ya nchi. Vilevile, Serikali imeanzisha Mpango Maalum wa Taaluma juu ya Athari ya Dawa za Kulevya unaoshirikisha viongozi wa ngazi mbalimbali nchini Kuanzisha Vituo Maalumu vya Kurekebisha Vijana Walioathirika na Dawa za Kulevya Serikali inaendelea na ujenzi wa Kituo maalumu cha kurekebisha Vijana walioathirika na Dawa za Kulevya katika eneo la Kidimni Wilaya ya Kati. Aidha, Nyumba za Marekebisho ya tabia (Sober Houses) 13 zimeanzishwa ambazo zimetoa huduma kwa vijana 1,020 kwa Unguja na Pemba. Serikali imechukua jitihada kubwa ya kuziendeleza nyumba hizo ili ziweze kutoa huduma zinazostahiki Taaluma na Ushauri Nasaha kwa Wananchi Serikali kupitia Vituo vya Ushauri Nasaha imeendelea kutoa ushauri nasaha kwa waathirika wa dawa za kulevya. Taaluma juu ya athari ya dawa za kulevya imetolewa katika Shehia mbalimbali za Unguja na Pemba, Vikosi vya SMZ pamoja na Skuli kupitia Mikutano, Makongamano, Semina pamoja na utoaji wa Kalenda na Vipeperushi. Aidha, jumla ya watu wapatao 3,673 (wanawake 1,956 na wanaume 1,717) wamehamasishwa na kupima VVU. 7.5 DEMOKRASIA NA UTAWALA BORA Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010 imeiagiza Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kufuata misingi ya Demokrasia na Utawala Bora katika kuhudumia wananchi. Utekelezaji wa agizo hili umelenga katika masuala yafuatayo: 116

130 7.5.1 Kuzingatia Misingi ya Demokrasia na Utawala Bora Serikali imeendelea kudumisha muundo wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa kama ilivyoelekezwa na Katiba ya Zanzibar ya 1984, mabadiliko ya 10, Toleo la Aidha, Serikali imeendelea kuzingatia na kudumisha misingi ya kidemokrasia na utawala bora kwa kuunda na kuhakikisha kuwa mihimili mikuu mitatu (Mahakama, Serikali, na Baraza la Wawakilishi) ya demokrasia na utawala bora inafanya kazi zake kwa uhuru bila ya kuingiliana na chombo chengine. Vilevile, Serikali imetoa elimu juu ya Mfumo wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa kwa Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi, Maafisa wa SMZ, Maafisa Wadhamini, Maafisa Tawala wa Mikoa na Wilaya pamoja na Wawakilishi wa Jumuiya za Kiraia Unguja na Pemba. Aidha, Serikali imetoa vipeperushi juu ya mfumo huo kwa ajili ya kutumika katika kutoa elimu hiyo kwa makundi mbalimbali ya kijamii. Pia, Viashiria vya Kitaifa vya Utawala Bora vimeandaliwa na kutumika kwa ajili ya kusimamia uwajibikaji na ufanisi katika utendaji wa Shughuli za Serikali. Aidha, Serikali kupitia Baraza la Wawakilishi imepitisha jumla ya Miswada 63 ya Sheria ambayo yote imesainiwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein na tayari zimekuwa Sheria kamili. Pia, jumla ya maswali ya msingi 1,558 na maswala ya nyongeza 3,103 yameulizwa kwa Serikali na yamepatiwa majibu sahihi. Vilevile, Serikali imefanya vikao vyote vya kawaida na vya kisheria kwa lengo la kujadili Nyaraka kadhaa zikiwemo za Sheria, Sera pamoja na kupokea na kujadili taarifa mbali mbali. Aidha, Mikutano kati ya Mheshimiwa Rais wa Zanzibar na Viongozi wa Wizara za SMZ kujadili utekelezaji wa malengo ya Bajeti imefanyika. Rais wa Zanzibar Dkt. Ali Mohamed Shein akizungumza na viongozi wa Mawizara kujadili utekelezaji wa Malengo ya Bajeti 117

131 7.5.2 Kusimamia Utekelezaji wa Kazi na Majukumu ya Serikali Serikali imeandaa na kupitisha Sera ya Utawala Bora pamoja na Sheria Nambari 4 ya Mwaka ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa lengo la kuhakikisha kwamba Viongozi wa Umma wanafuata maadili ya kazi zao. Pamoja na mambo mengine Sheria imefafanua maswala mbalimbali ikiwemo jinsi ya kuondoa mgongano wa kimaslahi kwa jambo ambalo Kiongozi wa Umma ana maamuzi nalo. Vilevile, Serikali imetoa elimu ya Uraia kwa wananchi juu ya Sera ya Utawala Bora, Rushwa na Haki za Binaadamu kupitia vyombo vya habari, ziara za vijijini pamoja na kutumia vikundi vya sanaa za maonesho. Pia, Sheria na Kanuni za kuzuia rushwa na uhujumu uchumi zimetayarishwa na kuanza kutumika. Vilevile, Serikali imeiimarisha Mamlaka ya Kuzuia Rushwa kwa kuwasomesha watendaji wake na kuwapatia watumishi wake mafunzo kwa vitendo katika Mamlaka ya Kuzuia Rushwa Tanzania Bara (TAKUKURU) pamoja na kununua vifaa vinavyohitajika katika kufanya uchunguzi na uendeshaji wa ofisi Kuendeleza Kazi ya Utekelezaji wa Mkakati wa Elimu ya Uraia, Kidemokrasia, Haki za Binaadamu na Utawala Bora Serikali imeandaa Programu za Kujenga Uelewa kwa Wananchi juu ya Elimu ya Uraia, ikiwemo elimu ya kidemokrasia, haki za binaadamu na utawala bora. Vipindi mbalimbali vya redio na TV vimetayarishwa na kurushwa hewani kupitia Shirika la Utangazaji Zanzibar (ZBC) kuhusiana na programu hizo. Pia, elimu ya rushwa na uhujumu wa Uchumi imetolewa kwa shehia za Unguja na Pemba pamoja na kusambaza Vijarida juu ya mapambano dhidi ya rushwa na uhujumu wa uchumi. Aidha, vipindi mbalimbali kuhusu utawala bora vimerushwa hewani na Shirika la Utangazaji Zanzibar pamoja na redio binafsi za Zanzibar. Vilevile, Shehia za Zanzibar zimepatiwa elimu ya uraia juu ya Utawala Bora na Haki za Binaadaam kupitia ziara za vijijini. Pia, Elimu ya Haki za Binaadamu na Utawala Bora imetolewa kwa watu weye Ulemavu na Waandishi wa Habari. Serikali inasimamia utoaji wa taarifa za Mheshimiwa Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi kwa wananchi kupitia vyombo vya habari kwa wakati muafaka. Idadi ya vyombo vinavyotoa taarifa hizo vimeongezeka kutoka vyombo vinne (4) mwaka 2010 hadi 11 mwaka. Aidha, 118

132 Jarida la Ikulu matoleo 16 yamechapishwa na kusambazwa katika taasisi zote za Serikali na Binafsi na Tovuti (Website) ijulikanayo kwa jina la inatumika kutoa taarifa hizo Kuimarisha Ofisi ya Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali Serikali imeimarisha Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali ili iweze kuimarisha kazi za ukaguzi, kutoa ripoti za ukaguzi zilizokuwa na viwango vinavyokubalika Kimataifa na kwa wakati muafaka. Aidha, Serikali imejenga majengo ya kisasa ya Ofisi Unguja na Pemba pamoja na kuziwekea vifaa vya kisasa vikiwemo komputa, kamera na server kwa ajili ya kuwekea kumbukumbu za kazi za ukaguzi. Vilevile, Serikali inaendelea kuwapatia mafunzo ya muda mfupi na mrefu wafanyakazi wake katika fani za Ukaguzi wa Thamani (Value for Money Auditing), Ukaguzi wa Komputa (Computerized Auditing) na Ukaguzi wa Mazingira (Environmental Auditing). Sambamba na hayo, Muundo wa Utumishi (Scheme of Service) kwa ajili ya wakaguzi umeandaliwa ili kuwapatia maslahi yanayolingana na kazi zao. Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akikata utepe kulifungua Jengo la Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali Wete Pemba Kuanzisha Mahakama ya Biashara Zanzibar Katika kufanikisha juhudi za kuanzisha Mahakama ya Biashara Zanzibar, Serikali imekamilisha uandaaji wa Sheria ya Kuanzisha Mahakama hiyo na imelifanyia matengenezo jengo linalotumika kwa Mahakama ya Biashara. 119

133 7.6 OFISI YA MKURUGENZI WA MASHTAKA Serikali imeanzisha Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka Zanzibar kwa mujibu wa Sheria Nam. 2 ya Aidha, Kitabu cha Muongozo wa Uendeshaji Mashtaka kimetayarishwa na kuanza kutumika. Pia, Serikali imejenga jengo jipya lenye Maktaba ya Sheria iliyopo Unguja. Maktaba hiyo inatoa huduma kwa wafanyakazi na wanasheria wa Serikali kutoka taasisi mbalimbali pamoja na wanafunzi wa Sheria. Vilevile, Kituo cha Mafunzo na Utafiti wa Sheria kimeanzishwa rasmi mwaka 2012 ambacho kinasomesha masomo ya sheria ngazi ya Cheti na Diploma. Sambamba na hayo, Jarida la SHAHIDI limeanza kuchapishwa kuanzia 2010 ambapo Matoleo 11 yamechapishwa na kusambazwa kwenye Wizara, Idara, Taasisi za elimu na wananchi kwa lengo la kuelimisha umma juu ya masuala ya makosa ya jinai. Serikali inaendelea kujenga nyumba za Waendesha Mashtaka katika Wilaya za Kusini, Kaskazini A na Magharibi. Aidha, Serikali imelifanyia matengenezo jengo la Kitengo cha Uendeshaji wa Mashtaka katika Mahakama ya Wilaya Mwanakwerekwe, imejenga Kituo cha Mafunzo ya Sheria Miembeni na kukamilisha ujenzi wa Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka Makunduchi. Vilevile, Serikali pia imeajiri Wanasheria wapya 28 na Makarani wa sheria wanne (4) pamoja na kusomesha Wanasheria 33. Kati ya hao, wanane (8) Shahada ya Uzamili ya Sheria, wanne (4) Shahada ya Kwanza ya Sheria, wanne (4) ngazi ya Cheti na Wanasheria 17 wamepatiwa mafunzo ya muda mfupi. Serikali kupitia Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka imefungua na kusimamia kesi za jinai 5,276 katika Mahakama za Zanzibar katika ngazi tofauti. Serikali pia, imeanzisha utaratibu wa wahalifu kutumikia Jamii badala ya kutumikia katika Chuo cha Mafunzo. Mpango huo tayari umeanza kutumika ambapo hukumu za aina hiyo tayari zimeanza kutolewa katika Mahakama mbalimbali. Watuhumiwa 15 (10 Unguja na 5 Pemba) waliotiwa hatiani wamepewa hukumu za kuitumikia jamii. 7.7 Kuimarisha Kiwanda cha Upigaji Chapa na Mpiga Chapa Mkuu wa Serikali Kwa lengo la kutekeleza azma ya Serikali ya kukiimarisha Kiwanda cha Upigaji Chapa na Mpiga Chapa Mkuu wa Serikali kwa kurudisha hadhi yake na kuinua kiwango cha uzalishaji, Serikali imelifanyia matengenezo makubwa jengo lililokuwa Kiwanda cha Sigara Maruhubi ili kutumika 120

134 kwa shughuli za Kiwanda cha Upigaji Chapa na Mpigaji Chapa Mkuu wa Serikali. Aidha, Serikali imekipatia Kiwanda mitambo mipya ya kisasa ya Uchapaji (Digital Printing Machines) kwa Awamu ya Kwanza. Kwa sasa kiwanda kinatekeleza majukumu yake ya kuchapisha nyaraka zote za Serikali kwa ubora na ufanisi wa hali ya juu. Rais wa Zanzibar Mheshimiwa Dkt. Ali Mohamed Shein akikagua maeneo mbalimbali katika Kiwanda cha Uchapaji na Mpiga Chapa Mkuu wa Serikali 7.8 SERIKALI ZA MITAA Kwa lengo la kuziendeleza na kuziimarisha Serikali za Mitaa, Ilani ya Uchaguzi ya CCM (2010- ) inaelekeza Serikali kuzifanyia mapitio sera na sheria ili kuimarisha uwajibikaji na kuongeza ufanisi wa kazi. Katika kuitekeleza azma hiyo, Serikali imefanikiwa kuandaa Sera ya Serikali za Mitaa na kufanikisha kufanya mapitio ya Sheria mbili (Sheria Nam.1 ya 1998 ya Tawala za Mikoa na Sheria Nam. 3 na 4 ya Baraza la Manispaa) na kuwa na Sheria Nam. 8 ya mwaka 2014 ya Tawala za Mikoa na Sheria Nam 7 ya Mamlaka ya Serikali za Mitaa ya mwaka. Aidha, Serikali imewajengea uwezo wafanyakazi wa Serikali za Mitaa kwa kuwapa mafunzo ya muda 121

135 mrefu na mfupi pamoja na ziara za kimasomo ndani na nje ya nchi kwa azma ya kuimarisha Taasisi za Serikali za Mitaa ili kuendana na Mfumo mpya wa Mageuzi ya Serikali za Mitaa. Pia, elimu juu ya kuanzisha mfumo madhubuti wa ukusanyaji na utunzaji wa mapato ya Serikali za Mitaa (Data base System) katika Taasisi za Halmashauri zote za Unguja na Pemba imetolewa. Aidha, Serikali imeendelea kuboresha upatikanaji wa huduma za jamii katika miji ya Zanzibar na kuhifadhi eneo la Urithi wa Mji Mkongwe kupitia Mradi wa Huduma za Jamii Mjini (Zanzibar Urban Service Project). Kupitia mradi huu uwezo wa kitaasisi wa Baraza la Manispaa Zanzibar na Mabaraza ya Miji ya Pemba umeimarishwa kwa kufanya ukarabati wa majengo, kutoa mafunzo kwa wafanyakazi na ununuzi wa vifaa vya ofisi, gari na vifaa vya usafi. Ukarabati mkubwa wa Ofisi ya Baraza la Manispaa iliopo Darajani na Karakana kuu iliopo Saateni unaendelea. Aidha, kazi ya ujenzi wa vibaraza vya kuwekea makontena ya kutupia taka unaendelea. Vilevile, vifaa mbalimbali ikiwemo gari 10, vespa 25 na pikipiki 7 zimenunuliwa kwa matumizi ya ofisi na gari 8 za kuzolea taka, gari 3 za kubebea makontena, gari 3 za kunyonyea maji taka, na gari moja (1) ya kubebea magari yaliyoharibika zimepatikana. Aidha, Serikali imelipatia Baraza la Manispaa makontena ya taka 192, marikwama 70 pamoja vikapu 1,000 vya kutilia taka. Vifaa hivyo ni kwa ajili ya matumizi ya Baraza la Manispaa Zanzibar na Mabaraza ya Miji ya Pemba Kusimamia Suala la Usafi Serikali imeendelea kutoa huduma endelevu za usafishaji wa mji kwa kushirikisha jamii ili kuweka mazingira bora. Vilevile, Serikali kupitia Baraza la Manispaa na Halmashauri za Wilaya imeingia mikataba na vikundi vya kijamii kwa ajili ya kufanya usafi katika masoko, bustani, mitaro, barabara na kuondoa taka katika maeneo ya Zanzibar. Aidha, Serikali imeweza kuimarisha kikundi kazi cha kusimamia zoezi la uondoaji mifugo inayozurura ovyo maeneo ya Manispaa na vitongoji vyake. Sambamba na hilo, katika kuimarisha mandhari ya mji wa Zanzibar, Serikali imeziimarisha bustani za njia kuu za Mji. Serikali pia, imeweza kuweka taa za barabarani na taa za kuongozea magari zinazotumia umeme wa jua katika maeneo ya Darajani, Mkunazini na Kwamchina. 122

136 Taa za barabarani zinazotumia nishati ya jua katika mji wa Zanzibar Kuhamasisha Wananchi Kuunda Kamati za Maendeleo Serikali imewahamasisha wananchi kuunda Kamati za Maendeleo za Shehia na Majimbo ambapo Shehia zote 336 katika majimbo 50 ya Unguja na Pemba zimeunda kamati hizo. Jukumu kubwa la kamati hizo ni kusimamia miradi ya maendeleo ya wananchi katika majimbo yao. Aidha, Wenyeviti, Makatibu na Washika fedha wa kamati zote wamepatiwa mafunzo juu ya uibuaji wa miradi, utunzaji wa kumbukumbu na udhibiti wa fedha Kuvijengea Uwezo Vikosi Maalum vya SMZ Ilani ya CCM (2010-) imeagiza Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kuvijengea uwezo na mazingira mazuri ya kazi Vikosi vya SMZ ili kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi zaidi. Katika kulitekeleza hilo, Serikali imefanya ununuzi wa vifaa mbalimbali vya maofisa na wapiganaji wa Vikosi vya SMZ ikiwemo sare za wapiganaji, huduma ya chakula na ununuzi wa vifaa vya kambini. Aidha, Serikali imeendelea na ujenzi na kuyafanyia ukarabati majengo mbalimbali ya vikosi Unguja na Pemba. Pia, maafisa na askari wamejengewa uwezo wa kitaaluma katika fani mbalimbali na viwango tofauti ikiwemo fani za Afya, Sheria, Uzamiaji, Utawala, Manunuzi na Ugavi, Usimamizi wa Fedha, Rasilimali watu, Ubaharia pamoja na masomo mbalimbali ya ufundi. 123

137 Kikosi Maalum cha Kuzuia Magendo (KMKM) Katika hatua za kukiimarisha Kikosi cha KMKM, Serikali imetoa mafunzo ndani na nje ya nchi kwa wapiganaji wake katika fani mbalimbali kuendana na kada zao. Pia, Serikali imefanya matengenezo ya majengo mbalimbali ya Kikosi cha KMKM kwa Unguja na Pemba, Aidha, Serikali imekipatia Kikosi hicho vifaa vya mawasiliano na huduma nyengine muhimu. Vilevile, Serikali imekiimarisha Kitengo cha Uzamiaji kwa ununuzi wa vifaa vya kisasa kwa ajili ya mafunzo ikiwemo troller kwa shughuli za uzamiaji. Sambamba na hayo, Serikali imefanya ukarabati wa vyombo vikubwa ikiwemo KM Miwi na KM Bawe pamoja na ukarabati wa magari yote ya KMKM. Serikali inaendelea kukiimarisha Kikosi cha KMKM ili kiendelee kufanya shughuli zake za doria za ulinzi na usalama baharini na nchi kavu pamoja na uokozi wakati wa majanga ya baharini. Boti za Kikosi cha KMKM zikiwa katika doria zake za kawaida Vilevile, Serikali imeendelea kuimarisha utoaji wa matibabu kwa wapiganaji na raia kwa kujenga Hospitali kubwa ya kisasa katika eneo la Kibweni pamoja na ununuzi wa vifaa mbalimbali vya matibabu na maabara. 124

138 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akikagua Hospital ya KMKM baada ya kuifungua Kibweni,Zanzibar Jeshi la Kujenga Uchumi (JKU) Ilani ya CCM imeitaka SMZ kuendeleza juhudi za kuliimarisha Jeshi la Kujenga Uchumi na kuimarisha miundombinu ya kambi zake ili kuwavutia vijana wengi zaidi kujiunga kupata mafunzo ya ukakamavu, uzalendo na stadi mbalimbali za maisha ili waweze kujitegemea. Katika kulitekeleza hilo, Serikali imeanzisha mafunzo ya stadi mbalimbali za maisha ikiwemo ufundi wa ushoni, ufundi bomba na useremala katika Chuo cha JKU Mtoni. Serikali pia, imekamilisha ujenzi wa miundombinu ya Kambi za JKU ikiwemo jengo la ghorofa 3 la Skuli ya Sekondari ya JKU, mabweni ya kulala wanafunzi, vyoo na nyumba za familia za askari. Katika kipindi cha miaka mitano (5) iliyopita, jumla ya vijana 8,000 wamepata nafasi ya kujifunza katika Chuo cha Amali cha JKU na katika kambi zake Unguja na Pemba. Vilevile, jumla ya Wapiganaji 86 wamekamilisha mafunzo ya uongozi mdogo na Wapiganaji 57 wanaendelea na masomo katika fani mbalimbali ikiwemo Afya, Sheria, Habari na Kilimo. 125

139 Rais wa Zanzibar Mheshimiwa Dkt. Ali Mohamed Shein akizindua rasmi na kukagua Mradi wa Kilimo cha Mboga mboga katika Shamba la JKU - Bambi Kikosi Cha Valantia Zanzibar Katika kukiimarisha Kikosi cha Valantia Zanzibar, Serikali imekamilisha ujenzi wa jengo la Makao Makuu ya Kikosi pamoja na kujenga makaazi ya wapiganaji na Maofisa wa Kikosi hicho. Aidha, Serikali imewajengea uwezo kwa kuwapa mafunzo ya muda mrefu na mfupi wafanyakazi wake katika fani mbalimbali. 126

140 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein, alipotembelea Makao Makuu ya Kikosi cha Valantia Mtoni Kikosi Cha Mafunzo Serikali imeendelea kukiimarisha kikosi cha Vyuo vya Mafunzo kwa kufanya ukarabati wa majengo katika kambi zake za Unguja na Pemba. Aidha, Serikali tayari imeshafanya upimaji wa maeneo ya Langoni, Kinumoshi, Ubago na Eneo la Ofisi Pemba ili kuyakinga maeneo hayo na uvamizi. Vilevile, maafisa na wapiganaji mbalimbali wa Kikosi cha Mafunzo wamejengewa uwezo katika fani na ngazi mbalimbali. 7.9 Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Serikali imekamilisha uandaaji wa Sera ya Hifadhi ya Jamii na kuanza utekelezaji wake. Lengo la sera hiyo ni kujenga mfumo wa hifadhi ya jamii unaolenga kutoa huduma bora za hifadhi kwa watu wote, hasa maskini na wanaoishi katika mazingira magumu zaidi, pamoja na kuimarisha mfumo wa uratibu wa huduma za hifadhi ya jamii. Kwa kutambua umuhimu wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii, Serikali imeimarisha ufuatiliaji wa utekelezaji wa Sheria ya mfuko huo. Katika kipindi cha Mfuko wa Hifadhi ya Jamii umesajili waajiri kutoka Serikali Kuu 295, Mashirika ya Serikali 80 na Taasisi Binafsi 3,472 pamoja na wanachama 66,111 kutoka Serikali Kuu, Mashirika ya Serikali na Taasisi Binafsi. Aidha, kwa kutambua umuhimu wa hifadhi ya jamii kwa wananchi, Mfuko umeanzisha Mfumo wa Uchangiaji wa Hiari (Zanzibar Voluntary Social 127

141 Security Scheme) ili kuhakikisha wananchi wengi zaidi wanafikiwa na kunufaika na matunda ya hifadhi ya jamii yanayotolewa na Mfuko huo. Tokea kuanzisha kwa mfumo huo mwaka 2012, Mfuko umeshasajili wanachama 4,970 kutoka vikundi mbalimbali vya uzalishaji, wajasiriamali, watu binafsi pamoja na Wazanzibari wanaofanya kazi nje ya nchi na kukusanya Shilingi milioni 122 hadi kufikia mwezi Juni Angalia Jadweli Namba 4 na 5. Jadweli namba 4: Takwimu za usajili wa wanachama waajiri ( ) Mwaka Serikali kuu Mashirika ya Serikali Taasisi Binafsi 2009/ / / / Jadweli namba 5: Takwimu za usajili wa wanachama waajiriwa ( ) Mwaka Serikali kuu Mashirika ya Serikali Taasisi Binafsi 2009/ ,674 2,631 23, / ,410 2,603 25, / ,953 2,735 28, / ,300 2,644 30,167 Katika kuhakikisha watoto wetu wanapata maeneo ya kucheza na kufurahi, Serikali kwa kushirikiana na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii imekijenga upya Kiwanja cha Kufurahishia Watoto cha Uhuru kiliopo kariakoo kwa gharama za shilingi bilioni 15. Kiwanja hicho kimefunguliwa rasmi tarehe 8 January wakati wa shamrashamra za Miaka 51 ya Mapinduzi ya Zanzibar. Aidha, Serikali inaendelea na matengezo ya Kiwanja cha Kufurahishia Watoto cha Tibirizi Pemba ambapo matengenezo hayo yako katika hatua za mwisho. Pia, Serikali kwa kushirikiana na Mfuko huo imeweza kuwekeza katika miradi mbalimbali ya maendeleo. Miongoni mwa miradi hiyo ni ujenzi wa Mnara wa Kumbukumbu ya miaka 50 ya Mapinduzi ya Zanzibar na ujenzi wa nyumba kumi (10) za makaazi Mbweni. 128

142 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein akifungua Kiwanja cha Kufurahishia Watoto cha Uhuru - Kariakoo Mjini Zanzibar Wananchi wakifurahika katika Kiwanja cha ZSSF-Uhuru Aidha, Mfuko wa Hifadhi ya Jamii umekuwa ukitoa mikopo kwa Serikali, Taasisi za Serikali na Taasisi Binafsi ikiwa ni moja ya njia ya kuwekeza fedha zinazotokana na michango ya wanachama wa Mfuko kama inavyoelezwa katika Sheria ya Mfuko ikiongozwa na Sera ya Uwekezaji ya Mfuko huo. Fedha hizo huwekezwa kwa kuzingatia usalama, faida, urahisi wa upatikanaji fedha, 129

143 mgawanyo na faida ya kiuchumi na kijamii. Katika kipindi cha 2010 hadi Mfuko umezikopesha taasisi mbalimbali jumla ya Shilingi bilioni 14.7 kama ifuatavyo; Chuo cha Usimamizi wa Fedha (ZIFA), TZS 1.8 bilioni kwa ajili ya ujenzi wa Hostel. Bodi ya Mapato Zanzibar (ZRB), TZS 5.0 bilioni kwa ujenzi wa ofisi Mazizini. Coastal Fast Ferries, USD 4,000,000 kwa ajili ya uboreshaji wa huduma za usafiri wa baharini. Zanzibar cable Television (ZCTV), TZS 329 milioni kwa uboreshaji wa huduma za matangazo ya televisheni. Halmashauri ya Kaskazini B, TZS milioni kwa ajili kuanzisha biashara ya uuzaji na usambazaji wa vifaa vya ujenzi kwa wananchi kwa gharama nafuu. 130

144 SEHEMU YA NANE 8.0 KUYAENDELEZA MAKUNDI MBALIMBALI 8.1 WATOTO Katika juhudi za Serikali za kuimarisha haki na maendeleo ya watoto, imeandaa Sheria ya Mtoto ya 2011 na kutengeneza Kanuni za kusimamia utekelezaji wa Sheria hiyo. Kanuni hizo zinahusu Masuala ya Hifadhi ya Mtoto, Usajili wa Vituo na Makaazi ya Kulelea Watoto, Ukaazi na Ulezi wa Kambo pamoja na Kinga Maalum Kuhusu Hifadhi, Ridhaa ya Kupima UKIMWI na Matibabu. Aidha, Serikali imeandaa Mkakati wa Masuala ya Sheria kwa Watoto ( ) kwa lengo la kuifanyia kazi Sheria ya Mtoto ili kuhakikisha kunakuwepo mfumo mzuri wa haki na ustawi wa watoto wa Zanzibar. Vilevile, Serikali imeendelea kuimarisha Mfumo wa Hifadhi ya Mtoto ikiwemo uanzishwaji wa Mahakama za Watoto. Pia, Serikali imo katika hatua za mwisho za kuifanyia marekebisho Sera ya Uhai, Hifadhi na Maendeleo ya Mtoto ya mwaka 2001 ili iende sambamba na mahitaji mapya yanayojitokeza kulingana na mabadiliko ya maendeleo na mahitaji ya mtoto. Serikali imesimamia uundwaji wa Mabaraza ya Watoto nchini ambapo jumla ya Mabaraza 239 yameundwa katika shehia mbalimbali za Unguja na Pemba. Mabaraza hayo yameundwa kwa lengo la kuwakutanisha watoto kuzungumza masuala yanayowahusu pamoja na changamoto zinazowakabili. Aidha, kupitia Mabaraza haya, ushiriki wa watoto katika kutoa maoni yao juu ya mambo yanayowahusu umeongezeka, watoto wamepata uelewa zaidi juu ya haki na wajibu wao na wanaweza kuelimishana. Pia, katika kukusanya maoni ya uanzishwaji wa Katiba Mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, jumla ya watoto 150 kutoka katika mabaraza 131 ya Unguja na Watoto 105 kutoka katika mabaraza 22 ya Pemba walishiriki katika utoaji wa maoni. Vilevile, Serikali imekamilisha ujenzi wa Nyumba ya Kulelea Watoto iliyopo Mazizini na tayari watoto wanalelewa katika nyumba hiyo. Serikali pia, imeandaa na kuisambaza Miongozo ya Uanzishaji na Uendeshaji wa Nyumba za Kulelea Watoto kwa taasisi binafsi pamoja na kuandaa kitini cha kufundishia watendaji wa vituo hivyo kwa lengo la kuimarisha malezi ya watoto katika vituo hivyo. Aidha, Serikali imefanya zoezi la kuvitambua vituo 13 vya kulelea watoto na kusimamia utekelezaji wake. Vilevile, Serikali inaendelea na usajili wa kuwatambua watoto walio katika mazingira magumu ambapo jumla ya watoto 12,453 wamesajiliwa na kutambuliwa mahitaji 131

145 yao kutoka Unguja na Pemba. Serikali inaendelea kutoa misaada ya kibinaadamu ikiwemo vyakula na mavazi kwa familia mbalimbali zinazoishi na watoto walio katika mazingira magumu. 8.2 VIJANA Kusimamia Utekelezaji wa Sera ya Maendeleo ya Vijana Kwa lengo la kuwaendeleza na kuzipatia ufumbuzi changamoto za Vijana, Serikali imesimamia na kuratibu utekelezaji wa Sera ya Maendeleo ya Vijana pamoja na kuzijengea uwezo taasisi za Vijana zipatazo 158 katika nyanja mbalimbali, ikiwemo kuwapatia mafunzo na semina za ujasiriamali, stadi za maisha na kusaidia upatikanaji wa ruzuku ili kusaidia utekelezaji wa Sera hiyo. Aidha, Serikali kwa kushirikiana na Asasi za Kiraia imekuwa ikiendelea kutoa elimu zaidi juu ya Sera hiyo kwa Vijana na wahusika wengine wa masuala ya maendeleo ya vijana Unguja na Pemba. Pia, kutokana na utekelezaji wa Sera hiyo, vikundi 258 vya Vijana vimeanzishwa kupitia SACCOS mbili (2) kubwa za vijana Unguja na Pemba. Vilevile, Serikali imeweza kuanzisha mashamba mawili (2) ya mfano Unguja na Pemba ili kuwawezesha vijana kujiajiri kupitia shughuli za kilimo. Vilevile, Serikali kwa kushirikiana na Taasisi zisizo za kiserikali zimeweza kuwapatia vijana mafunzo ya ujasiriamali, vifaa pamoja na kuwawezesha kujiajiri wenyewe. Aidha, Serikali imeanzisha Mfuko Maalum wa Vijana ambao unatoa mikopo nafuu kwa kupitia vikundi vyao walivyoanzisha. Mfuko huu tayari umeshawapatia vijana mikopo yenye thamani ya jumla ya Shilingi milioni 813,800,000 kwa vijana 2,285 kupitia vikundi 258 Unguja na Pemba Kukamilisha Uanzishaji wa Baraza la Taifa la Vijana Serikali imekamilisha uandaaji wa Sheria na Kanuni ya kuanzisha Baraza la Vijana Zanzibar lenye lengo la kuwashirikisha vijana katika ngazi mbalimbali za maamuzi. Aidha, Baraza hilo tayari limeshaundwa na Katibu wa Baraza la Vijana tayari ameshateuliwa na Mheshimiwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi. 8.3 WANAWAKE Katika utekelezaji wa Sera ya Hifadhi na Maendeleo ya Wanawake ya mwaka 2001, Serikali imeweza kuwajengea uwezo na uthubutu wanawake wa kutumia fursa za kujiendeleza kiuchumi, 132

146 kijamii na kisiasa. Wanawake wengi hivi sasa wameweza kumiliki mitaji na kufanya biashara kubwa na ndogo zinazoendesha maisha yao, familia zao na kuchangia uchumi wa Taifa. Aidha, kutokana na utekelezaji mzuri wa sera hiyo, wanawake wameweza kuhamasika na kujitokeza kugombea nafasi mbalimbali za uongozi katika ngazi zote za maamuzi. Idadi ya wanawake katika vyombo vya utoaji maamuzi na ngazi mbalimbali za uongozi ni kama ifuatavyo: Baraza la Wawakilishi asilimia 40, Madiwani asilimia 14, Mawaziri asilimia 25, Makatibu Wakuu asilimia 25, Wakurugenzi asilimia 42, Wakuu wa Mikoa asilimia 20, Wakuu wa Wilaya asilimia 20, Makatibu Tawala asilimia 20, Majaji asilimia 33 Mahakimu asilimia 21 na Masheha asilimia 8. Aidha, Serikali imewashajiisha na kuwawezesha wanawake na makundi mengine ya wanaharakati kutathmini juhudi wanazozichukua katika kupambana na vitendo vya ukatili na udhalilishaji wa kijinsia, kubaini changamoto na kupanga mipango ya baadae. Pia, Kwa kushirikiana na Shirika la Action AID, Serikali imeanzisha Nyumba Salama kwa ajili ya kuwahifadhi na kuwahudumia waathirika wa vitendo vya udhalilishaji wa wanawake na watoto, pamoja na kufuatilia kesi zao Mahakamani ambapo hadi sasa jumla ya waathirika 26 wamepatiwa huduma ya hifadhi katika nyumba hiyo. Katika kipindi cha miaka mitano iliyopita malalamiko mbalimbali yanayohusu haki za wanawake (udhalilishaji, kutelekezwa na kukosa matunzo) yameripotiwa na kushughulikiwa katika vyombo vya kisheria. Sambamba na hayo, Serikali imeanzisha na kuzijengea uwezo Kamati za Kupambana na Ukatili na Udhalilishaji wa Kijinsia kutoka ngazi ya Taifa hadi Shehia, imeunda Mtandao wa Wanaume wa kupambana na vitendo vya udhalilishaji wa kijinsia, imetayarisha miongozo ya kufundishia na kushirikiana na viongozi wa dini katika mapambano hayo. Aidha, Serikali imefanya uchambuzi wa sheria na kanuni zinazohusiana na udhibiti wa vitendo vya udhalilishaji wa kijinsia, na kuweza kubaini mapungufu mbalimbali ambayo tayari yameanza kufanyiwa kazi. Serikali inaendelea na juhudi zake za kuvipatia mafunzo, kuvihamasisha, kuvishauri na kuvitembelea vikundi vya wanawake vya uzalishaji mali, wajasiriamali na SACCOS kwa lengo la kuviimarisha na kuvifanya vijitegemee ili vichangie katika kupiga vita umasikini na kukuza hali zao kiuchumi. Jumla ya vikundi vya wanawake 551 (Unguja 209 na Pemba 362) na SACCOS 53 (Unguja 24 na Pemba 29) zimetembelewa na kuhamasishwa. Wanawake wengi wamehamasika 133

147 kujiunga katika vikundi vya uzalishaji pamoja na SACCOS Unguja na Pemba na kuweza kujikwamua na hali ngumu ya kiuchumi. 8.4 WAZEE Katika juhudi za kuwapatia hifadhi ya makaazi, huduma za afya na misaada ya kijamii wazee wasiojiweza na wasio na jamaa, Serikali inaendelea kuwatunza na kuwahudumia wazee 91 katika Nyumba za Wazee za Serikali zilizopo Unguja na Pemba na kupatiwa chakula, mavazi na huduma za afya. Aidha, wazee 149 wanapatiwa fedha za posho ya kujikimu kimaisha kila mwezi. Vilevile, Serikali imeiyafanyia matengenezo makubwa majengo ya Nyumba za Wazee Sebleni. Ukumbi wa Mikutano na Msikiti pamoja na kuzungushiwa ukuta katika makazi hayo. Pia, vifaa vyote muhimu vimenunuliwa na kuimarisha miundo mbinu ya maji na umeme katika makaazi hayo. Hatua hizo zimeimarisha hali ya wazee pamoja na utulivu na usalama wao. Makamu wa Pili wa Rais Mheshimiwa Balozi Seif Ali Iddi akifungua Majengo ya Nyumba za Wazee Sebleni zilizofanyiwa Ukarabati mkubwa. Aidha, katika juhudi za kuimarisha maslahi ya wazee, Serikali imeamua kuanzisha Mpango wa Malipo ya Pencheni Jamii kwa Wazee Wote (Universal Pension). Mpango huu utawahusisha wazee wenye umri wa miaka 70 na kuendelea ambapo kila mzee atapewa 20,000 kwa mwezi. Mpango huu utatekelezwa na Serikali kupitia Sekta ya Uwezeshaji na Ustawi wa Jamii Kuhamasisha Jamii Kuendeleza Utamaduni wa Kuwaheshimu, Kuwaenzi na Kuwatunza Wazee wetu 134

148 Serikali inaendelea na kuihamasisha jamii kuendeleza utamaduni wa kuwaheshimu, kuwaenzi na kuwatunza wazee wetu. Kila ifikapo siku ya tarehe 01 Oktoba ya kila mwaka Serikali inasimamia maadhimisho ya Siku ya Wazee Duniani kwa lengo la kutathmini mafanikio na changamoto zilijitokeza katika jitihada za kuwatunza, kuwaheshimu na kuwaenzi wazee ikiwa ni pamoja na kuihamasisha jamii na wadau wengine kuongeza juhudi za kuendeleza kuwaheshimu, kuwaenzi na kuwatunza wazee. Aidha, Serikali inakamilisha matayarisho ya kuwapatia pencheni Jamii kwa wazee wote wenye umri wa kuanzia miaka 70 na kuendelea. 8.5 WATU WENYE ULEMAVU Kubaini Watu Wenye Ulemavu Wanaoweza Kufanyakazi za Uzalishaji Mali Ili kuwa na takwimu sahihi za Watu wenye Ulemavu na aina ya Ulemavu walionao pamoja na kurahisisha upangaji wa Sera, Mikakati ya Mipango mbalimbali hapa nchini, Serikali imefanya usajili katika Wilaya zote za Unguja na Pemba na jumla ya watu wenye ulemavu 542 (321 Unguja na 259 Pemba) wamesajiliwa. Watu hao wanajishughulisha na kazi mbalimbali zikiwemo ufundi magari, useremala, ufinyanzi, ufundi wa TV, uashi, ufundi umeme na ushoni. Aidha, Serikali imetayarisha Sera ya Watu wenye Ulemavu pamoja na Mpango wa Utekelezaji wa Sera. Pia, muongozo wa kuombea ruzuku kwa Jumuiya za Watu wenye Ulemavu umeandaliwa. Vilevile, vikao mbalimbali vya kawaida vya Baraza la Taifa la Watu wenye Ulemavu na vikao vya maafisa waratibu vimefanyika. Usajili wa Watu wenye Ulemavu unaendelea kufanyika pamoja na kuwapatia Watu wenye Ulemavu visaidizi na Dawa kwa Unguja na Pemba. Serikali imeendelea kutoa elimu inayohusu mikataba, haki, fursa na wajibu wa Watu wenye Ulemavu katika Shehia zote za Unguja na Pemba. Pia, Serikali inaendelea kutoa ruzuku kwa Jumuiya za Watu wenye Ulemavu Unguja na Pemba ili ziweze kutimiza malengo yao. Jumuiya hizo ni CHAVIZA, ZANAB, UWZ, JMZ, SADZ, JUWAUZA, ZAPDD, na SOZ. Serikali imeendelea Kuratibu Mfuko wa Maendeleo ya Watu Wenye Ulemavu Zanzibar. Hadi kufika Septemba 2013 mfuko umekusanya jumla ya Shilingi milioni WAFANYAKAZI Kuandaa Sera ya Hifadhi ya Jamii na Kufanya Mapitio ya Sheria za Kazi Serikali ina jukumu la kuzifanyia mapitio Sheria za Kazi ambapo Kanuni kumi (10) za Sheria ya Ajira Nambari 11 ya mwaka 2005 zimetayarishwa na kuanza kutumika. Kanuni hizo zinahusu 135

149 mambo mbalimbali yakiwemo Maslahi ya Wafanyakazi katika Sekta Binafsi, Usajili na Utendaji kazi wa Vyama vya Wafanyakazi, Mikataba, Likizo Bila ya Malipo na Makundi Maalum ya Wafanyakazi. Kukamilika kwa kanuni hizi kutarahisisha utekelezaji wa Sheria za Kazi katika maeneo yaliyotajwa. Pia, Kanuni za Utumishi wa Umma zimeshatayarishwa na zimeshasambazwa kwa wahusika wote. Vilevile, Serikali kwa kushirikiana na Shirika la Kazi Duniani imezinduwa rasmi Toleo Maalumu la Sheria za Kazi katika lugha nyepesi. Toleo hilo limefafanuwa vipengele muhimu vya Sheria tano (5) za kazi zikiwemo Sheria ya Ajira, Sheria ya Uhusiano Kazini, Sheria ya Usalama na Afya Kazini, Sheria ya Mfuko wa Hifadhi ya Jamii, Sheria ya Fidia pamoja na Sheria moja ya Usafiri Baharini Kusimamia Utekelezaji wa Sera ya Ajira Serikali imeufanyia mapitio ya Mpango wa Ajira kwa Vijana wa mwaka 2009 na kuandaa Mpango mpya wa mwaka Mpango huo tayari umesambazwa katika Taasisi za Umma na Taasisi Binafsi. Mpango huo ni Dira katika suala zima la ajira na kuwawezesha vijana kujiajiri. Katika hatua za msingi za utekelezaji wa Mpango huo, Serikali imeandaa Makongamano na Semina mbalimbali za kujadili Mpango wa Ajira kwa Vijana wa miaka minne kuanzia mwaka kwa vijana kutoka Unguja na Pemba. Aidha, Serikali imezindua mfuko wa uwezeshaji wananchi kiuchumi kwa kuunganisha Mfuko wa Kujitegemea, Mfuko wa AK/JK na Mfuko wa Vijana ili kuweza kukabiliana na tatizo la ajira na kuinua uchumi wa Zanzibar. Vilevile, kwa mashirikiano na taasisi mbalimbali za Serikali na Binafsi, Serikali imeendelea kuishughulikia changamoto ya upatikanaji wa ajira hasa kwa vijana nchini kwa kuwaorodhesha watafuta kazi kupitia Kituo cha Kutoa Taarifa za Soko la Ajira ili kuweza kuwaunganisha na waajiri. Jumla ya vijana 2,473 wameorodheshwa, ambapo vijana 1,978 wamefanikiwa kuajiriwa ndani na nje ya nchi kupitia Kituo hicho. Jadweli namba 6: Idadi ya Vijana Waliosajiliwa Kuomba Kazi Katika Kituo cha Kutoa Taarifa za Ajira 2010 hadi Mwaka Wanawake Wanaume Jumla

150 ,232 Jumla 1,031 1,442 2,473 Jadweli namba 7: Idadi ya Vijana Walioajiriwa kwa Kuunganishwa na Waajiri Kupitia Kituo cha Kutoa Taarifa za Ajira 2010 hadi Mwaka Wanawake Wanaume Jumla ,000 Jumla 1, , Kuimarisha Mashirikiano kati ya Serikali, Shirikisho la Vyama Huru vya Wafanyakazi na Waajiri Serikali imeendelea kuimarisha mashirikiano ya UTATU kati ya Shirikisho la Vyama Huru vya Wafanyakazi, Jumuiya ya Waajiri na Serikali. Mashirikiano hayo yamewezesha kufanyika kwa majadiliano ya pamoja katika mambo ya maslahi ya wafanyakazi, kuweko kwa utulivu na amani katika maeneo ya kazi na pia utatu huo umeiwezesha Zanzibar kutekeleza mikataba na maazimio yanayohusiana na masuala ya ajira ambayo Tanzania imetia saini na kuyaridhia Kuendelea Kuimarisha Mazingira bora na Maslahi ya Wafanyakazi Serikali imefanya tathmini na ufuatiliaji wa utekelezaji wa Muundo wa Utumishi kwa Wizara, Mashirika ya Serikali na Taasisi za Umma. Wizara 13 zimeweza kufavyiwa tathmini Unguja na Pemba. Pia, Serikali imeandaa muongozo unaolenga kupima uzito na kufanya tathmini ya kazi (Job evaluation and grading) ili kuondoa malalamiko katika malipo ya mishahara kwa watumishi 137

151 wa Umma. Vilevile, katika kuimarisha mazingira bora na maslahi ya wafanyakazi, Serikali inaendelea na uandaaji wa Sera ya Malipo kwa Watumishi wa Umma kwa lengo la kuimarisha mfumo mzima wa malipo ya mishahara na stahiki nyengine za Watumishi. Aidha, Serikali inaendelea na uandaaji wa upangaji wa taarifa za wafanyakazi kupitia malipo ya mishahara kwa ajili ya kutoa muongozo na kutatua changamoto zinazojitokeza katika Utumishi wa Umma. Vilevile, Serikali imefanya mapitio ya mishahara na malipo mengine ya Watumishi wa Umma Unguja na Pemba, pamoja na kufanya marekebisho ya nyongeza za mishahara kwa watumishi wenye uzoefu usiopungua miaka 15 ya utumishi kwa kada zote. Serikali imepandisha kima cha chini cha mshahara kutoka TZS. 125,000/= hadi TZS. 150,000/= hii ni sawa na ongezeko la asilimia 20. Kwa upande wa Sekta Binafsi, Serikali imeweka kima cha chini cha mshahara kuwa TZS.145,000/= kutoka TZS. 70,000/= cha mwaka 2010 ikiwa ni ongezeko la asilimia 107. Aidha, Serikali imeendelea na kazi ya kutoa taaluma ya utayarishaji wa Mkataba wa Utoaji Huduma kwa Mteja kwa Wizara 16. Katika kusimamia utekelezaji wa Sheria Nambari 8 ya mwaka 2005 ya Usalama na Afya Kazini, Serikali imefanya Ukaguzi Kazi na ukaguzi wa Usalama na Afya Mahala pa Kazi kwa taasisi zote za watu binafsi katika Mikoa yote ya Unguja na Pemba. Miongozo imetolewa juu ya mapungufu yaliyobainika na kuagiza kurekebishwa kasoro hizo. Vilevile, hatua mbalimbali za kisheria zimechukuliwa dhidi ya waajiri walioonekana kukiuka Sheria za Kazi kwa makusudi, licha ya ushauri uliotolewa awali wa kurekebisha kasoro hizo. Aidha, sehemu za kazi 351 zimesajiliwa ili kuzitambua na kuweka taarifa zao kwenye Daftari la Usajili wa Sehemu za Kazi. Utambuzi huu unarahisisha shughuli za ukaguzi kwa kutambua mapema mazingira ya kazi zao, hatari zinazoweza kutokea katika sehemu hizo na hivyo kutoa ushauri na maelekezo yanayofaa, kabla ya kutokea tatizo au ajali. Jadweli Namba 8 na 9 linachanganua hali ya Ukaguzi Kazi na Ukaguzi Afya na Usalama kazini. Jadweli namba 8: Taasisi Zilizofanyiwa Ukaguzi Kazi 2010 hadi Mwaka Mjini Magharibi Kusini Unguja Kaskazini Unguja Kusini Pemba Kaskazini Pemba Jumla 138

152 Jumla ,067 Jadweli namba 9: Ukaguzi wa Usalama na Afya Kazini Mwaka Mjini Kusini Kaskazini Kusini Kaskazini Jumla Magharibi Unguja Unguja Pemba Pemba Jumla SEHEMU YA TISA 139

153 9.0 MAENEO MENGINEYO MUHIMU 9.1 SEKTA YA SHERIA Katika kuimarisha Sekta ya Sheria, Ilani ya CCM ya mwaka imeagiza Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kuimarisha Mahakama kwa kujenga majengo mapya na kuzipatia vifaa vya kisasa, kujenga nyumba za Mahakimu Unguja na Pemba na kufanya marekebisho ya Sheria na Kanuni za Utendaji kazi wa Mahakama. Katika kutekeleza maagizo hayo, Serikali imefanya matengenezo makubwa ya jengo la Mahakama Kuu Vuga, Mahakama ya Makunduchi, Mahakama ya Kadhi wa Wilaya Mwanakwerekwe, majengo ya Mahakama Chwaka na matengenezo ya jengo la Mahakama Kuu Chake chake Pemba. Aidha, Serikali imenunua vitendea kazi na kusomesha wafanyakazi 78 katika kada na ngazi mbalimbali ili kuimarisha utendaji kazi wa Mahakama. Vilevile, katika juhudi za kuondoa matatizo ya ushughulikiaji wa kesi za watoto, Serikali imeanzisha Mahakama ya Watoto ambayo tayari inaendelea kufanya kazi zake. Kwa upande wa Majaji Serikali imefanikiwa kuongeza idadi yao kutoka wawili (2) mwaka 2011 hadi sita (6) (wakiwemo wanawake wawili (2)) mwaka Vilevile, kwa upande wa Mahakimu wa ngazi mbalimbali Serikali imefanikiwa kuongeza idadi yao kutoka 43 mwaka 2010 hadi kufikia 85 mwaka hii ni sawa na ongezeko la asilimia Kuwaendeleza Wataalamu wa Sheria za Mikataba Serikali kupitia Ofisi ya Mwanasheria Mkuu imeanzisha Kitengo kinachohusiana na masuala ya Mikataba, ambacho kina wataalamu wanaoshughulikia masuala yote ya mikataba ya Serikali. Aidha, Serikali imewapatia mafunzo maafisa wa Sheria kutoka Taasisi mbalimbali juu ya uandishi wa sheria, utatuzi wa migogoro, ufungaji na uingiaji wa mikataba ya kitaifa na kimataifa. Mafunzo hayo yamedhaminiwa na Serikali kwa mashirikiano na UNDP kupitia Mradi wa Mageuzi katika Sekta ya Sheria (Zanzibar Legal Sector Reform Program). 140

154 9.1.2 Kuyatafutia Ufumbuzi Masuala ya Mrundikano wa Kesi Mahakamani Serikali imeajiri mahakimu wapya na kufanya matengenezo ya majengo yake ili kupunguza changamoto ya mrundikano wa kesi katika Mahakama zake. Serikali kupitia Mahakama imeanzisha Kamati ya Kusukuma Kesi kwa kuwashirikisha wadau wote wa masuala ya kesi. Kamati hiyo inakutana kila baada ya miezi mitatu kujadili namna ya kuendesha na kuharakisha kesi hizo. Vilevile, Mahakama kupitia Mradi wa Mageuzi ya Sekta ya Sheria inaendelea na utaratibu wa kuanzisha Mfumo wa Kisasa wa Usimamizi wa Uendeshaji Kesi (Case Management System). Aidha, Serikali imezipatia Mahakama zote vifaa ili kusadia kupunguza mrundikano wa kesi Kuwapatia Mafunzo Mahakimu wa Mahakama ya Mwanzo Katika azma ya kuwaendeleza Mahakimu, Serikali kupitia Programu ya Mabadiliko katika Sekta ya Sheria, imewapatia mafunzo Majaji, Mahakimu na Waendesha Mashtaka ili kuwazidishia ujuzi katika utendaji wa kazi zao za kila siku. Miongoni mwa mafunzo yaliyotolewa ni pamoja na teknolojia ya habari na sheria, uendeshaji wa kesi na utoaji wa haki, usimamizi wa kesi, na uandishi wa sheria Kukamilisha Mchakato wa Kutenganisha Shughuli za Upelelezi na Uendeshaji Mashtaka Jengo la Mahakama Kuu baada ya kufanyiwa Matengenezo Vuga Mjiji Zanzibar Katika kukamilisha utaratibu wa kutenganisha shughuli za upelelezi na uendeshaji wa mashtaka, Serikali imeajiri Waendesha Mashtaka katika Mahakama za Wilaya. Hivi sasa Waendesha 141

155 Mashtaka wapo katika Mahakama Kuu, Mahakama zote za Mkoa na Mahakama sita (6) za Wilaya ambazo ni Mjini, Magharibi, Chake Chake, Mkoani, Micheweni na Wete. Hatua za kupeleka Waendesha Mashtaka katika Mahakama nne (4) za Wilaya zilizobaki zinaendelea, ambazo ni Mkokotoni, Mfenesini, Mwera na Makunduchi Msaada wa Kisheria Serikali inaendelea na utayarishaji wa Sera ya Msaada wa Kisheria (Zanzibar Legal Aid Policy). Sera hiyo itakapopitishwa itatoa fursa kwa makundi maalum ikiwemo watoto, wanawake, watu Wenye Ulemavu na masikini kupata haki zao Kupeleka Huduma za Mahakama Karibu na Wananchi Serikali imepeleka huduma za Mahakama karibu na wananchi kwa kuendesha vipindi vya redio na televisheni, mikutano ya hadhara katika shehia na maskuli na kutoa na kusambaza kwa wananchi Matoleo mbalimbali ya Jarida la Mahakama la Shahidi kwa ajili ya kuelimisha wananchi kuhusu huduma na masuala ya Mahakama na jinai. Katika kipindi cha 2010 hadi, jumla ya kesi 28,870 zilisajiliwa katika Mahakama mbalimbali Unguja na Pemba, ambapo kesi 14,267 sawa na asilimia 49 zilitolewa uamuzi. Aidha, Serikali imekamilisha uchapishaji wa seti 890 za Sheria za Zanzibar kuanzia mwaka 1980 hadi Kwa kawaida seti moja inachukua Volume 14. Sheria hizo tayari zimesambazwa kwa wadau. Vilevile, Serikali imefanya kazi ya kuziweka pamoja Sheria za Zanzibar (consolidation) kuanzia mwaka 1959 hadi 2010, Rasimu ya Mwanzo kwa mwaka 1980 hadi 2010 imekamilika. Ofisi ya Mwanasheria Mkuu imeweza kuandaa Miswada ya Sheria 69, Kanuni 8, Matangazo na Machapisho 650 ya kisheria, Ofisi pia imeweza kusimamia kesi 53 dhidi ya Serikali na kutoa ushauri kwa Taasisi za Serikali. 142

156 Jengo Jipya la Wizara ya Katiba na Sheria lilopo Mazizini Mjini Zanzibar Jengo la Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar lilopo Mazizizni Mjini Zanzibar Mapambano Dhidi ya Rushwa na Uhujumu wa Uchumi Kutokana na umuhimu wa kupambana na rushwa na uhujumu uchumi, Serikali imetunga Sheria na. 1 ya mwaka 2012 ambayo imetoa mamlaka ya kuanzishwa kwa Kitengo cha Kupambana na rushwa na uhujumu Uchumi Zanzibar. Aidha, Serikali imeandaa Kanuni za utekelezaji wa Sheria pamoja na kutoa elimu juu ya mapambano dhidi ya rushwa na uhujumu uchumi kwa kutumia njia mbalimbali zikiwemo vipindi maalum vya redio na televisheni, majarida, vipeperushi, stika, 143

ENERGY AND WATER UTILITIES REGULATORY AUTHORITY (EWURA)

ENERGY AND WATER UTILITIES REGULATORY AUTHORITY (EWURA) ENERGY AND WATER UTILITIES REGULATORY AUTHORITY (EWURA) In the matter of an Application by the BABATI URBAN WATER SUPPLY AND SEWERAGE AUTHORITY ( BAWASA ) For a Tariff Application, Submited on 22 nd May

More information

6.0 Hitimisho JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA. Ifahamu Sekta ya Biashara. TOLEO Na. 1, Desemba, 2012

6.0 Hitimisho JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA. Ifahamu Sekta ya Biashara. TOLEO Na. 1, Desemba, 2012 6.0 Hitimisho Wafanyabiashara wanahamasishwa kutumia fursa zitokanazo na Mikataba mbali mbali ya biashara ambayo Tanzania imesaini ili kujiletea mafanikio katika biashara zao na kukuza pato, kuinua uchumi

More information

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA MAKAMU WA RAIS

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA MAKAMU WA RAIS JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA MAKAMU WA RAIS HOTUBA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, WAKATI WA KUWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI KWA MWAKA WA FEDHA 2015/16 Mhe.

More information

HOTUBA YA WAZIRI WA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI, MHESHIMIWA SAMUEL J. SITTA (MB.), AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA

HOTUBA YA WAZIRI WA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI, MHESHIMIWA SAMUEL J. SITTA (MB.), AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA HOTUBA YA WAZIRI WA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI, MHESHIMIWA SAMUEL J. SITTA (MB.), AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA KWA MWAKA 2011/2012 i Kama mjuavyo tarehe 1 Julai, 2010

More information

Sauti Yangu Isikilizwe! Kuwasaidia watu wenye ulemavu wa akili kushiriki katika masuala ya kijamii na harakati za kisiasa.

Sauti Yangu Isikilizwe! Kuwasaidia watu wenye ulemavu wa akili kushiriki katika masuala ya kijamii na harakati za kisiasa. Sauti Yangu Isikilizwe! Kuwasaidia watu wenye ulemavu wa akili kushiriki katika masuala ya kijamii na harakati za kisiasa. Warsha kwa ajili ya Watetezi Binafsi (Watu Wenye Ulemavu wa Akili) na Familia

More information

Thursday, December 03,

Thursday, December 03, Jamhuri ya Muungano wa Tanzania MABADILIKO YA TABIANCHI: MIKAKATI YA UTEKELEZAJI NA VIPAUMBELELE VYA KITAIFA RICHARD MUYUNGI OFISI YA MAKAMU WA RAIS Thursday, December 03, 2009 1 YALIYOMO Utangulizi Mikakati

More information

East African Currency...

East African Currency... East African Currency... This will definitely take you back to some old memories! Hope that you haven't forgotten your Swahili... From German to Gt. Britain gov'ts, check out the old E. A. currency from

More information

Welcome Karibuni. By Moses Kulaba, Agenda Participation Tanzania Corruption Tracking System /

Welcome Karibuni. By Moses Kulaba, Agenda Participation Tanzania Corruption Tracking System  / Welcome Karibuni UTAWALA BORA NA UWAJIBIKAJI -TANZANIA: USHIRIKI WA WANANCHI KUIMARISHA USIMAMIZI WA RASILIMALI ZA UMMA NA WABUNGE- PARLIAMENTARY OVERSIGHT By Moses Kulaba, Agenda Participation 2000- Tanzania

More information

KUMBUKUMBU ZA MKUTANO NA MAANGALIZO

KUMBUKUMBU ZA MKUTANO NA MAANGALIZO MKUTANO KATI YA IDARA YA WANYAMAPORI, JUMUIA ZA KIJAMII ZILIZOIDHINISHWA (AA) ZA MAENEO YA HIFADHI ZA WANYAMAPORI ZA JUMUIA (WMA), WAWAKILISHI WA VIJIJI, WILAYA NA MAKAMPUNI YA KITALII JUU YA KANUNI ZA

More information

How best to promote the Conservation of Zanzibar Stone Town. By Mahmoud Thabit Kombo -Chairman ZSTHS (JUHIMKO)

How best to promote the Conservation of Zanzibar Stone Town. By Mahmoud Thabit Kombo -Chairman ZSTHS (JUHIMKO) How best to promote the Conservation of Zanzibar Stone Town By Mahmoud Thabit Kombo -Chairman ZSTHS (JUHIMKO) The Meaning of World Heritage Site Definition by UNESCO A site of outstanding value for the

More information

TUKIO (Event) WAHUSIKA (Participants) WASIMAMIZI ENEO(Coverage) MAHALI (Place)

TUKIO (Event) WAHUSIKA (Participants) WASIMAMIZI ENEO(Coverage) MAHALI (Place) TAREHE (Date) JAN FEB TUKIO (Event) WAHUSIKA (Participants) WASIMAMIZI ENEO(Coverage) MAHALI (Place) 1 3 Mapumziko ya Mwaka Mpya Watendakazi Watendakazi 06 Sabato ya Kufunga na Kuomba Wachungaji & Wazee

More information

KANUNI ZA UONGOZI. d nnnnnnnnnnn.

KANUNI ZA UONGOZI. d nnnnnnnnnnn. MAADILI KANUNI ZA UONGOZI YA KITAIFA NA d nnnnnnnnnnn www.kippra.or.ke KUHUSU KIPPRA Maadili ya Kitaifa na Kanuni za Uongozi T aasisi ya Kenya ya Utafiti na Uchanganuzi wa Sera za Umma (KIPPRA) ni Shirika

More information

Wanafunzi waliofukuzwa Ndanda kurejeshwa shuleni

Wanafunzi waliofukuzwa Ndanda kurejeshwa shuleni Sauti ya Waislamu ISSN 0856-3861 Na. 996 RABBIUL AWWAL 1433, IJUMAA JAN. 27 - FEB. 2, 2012 BEI TShs 500/=, Kshs 50/= Uhalali wa muungano kwanza katiba baadae Uk. 2 Wanafunzi waliofukuzwa Ndanda kurejeshwa

More information

Mwongozo wa Utekelezaji wa vikwazo vilivyowekewa Korea Kaskazini - Changamoto zinazokumba nchi barani Afrika

Mwongozo wa Utekelezaji wa vikwazo vilivyowekewa Korea Kaskazini - Changamoto zinazokumba nchi barani Afrika Mwongozo wa Utekelezaji wa vikwazo vilivyowekewa Korea Kaskazini - Changamoto zinazokumba nchi barani Afrika Imetayarishwa na Shirika la Kimataifa la Utiifu na Uwezo Septemba 2018 Washington, DC Marekani

More information

MAMLAKA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI STADI (VETA)

MAMLAKA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI STADI (VETA) MAMLAKA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI STADI (VETA) TANGAZO LA KUJIUNGA NA MAFUNZO YA UFUNDI STADI DARAJA LA TATU (LEVEL III) VETA INAPENDA KUWATANGAZIA WATANZANIA WOTE KUWA MAFUNZO KWA DARAJA LA TATU YATAANZA

More information

WIZARA YA KAZI NA AJIRA TAARIFA KWA UMMA ORODHA YA MAKAMPUNI YALIYOIDHINISHWA NA SERIKALI KUENDESHA HUDUMA ZA WAKALA BINAFSI WA AJIRA NCHINI

WIZARA YA KAZI NA AJIRA TAARIFA KWA UMMA ORODHA YA MAKAMPUNI YALIYOIDHINISHWA NA SERIKALI KUENDESHA HUDUMA ZA WAKALA BINAFSI WA AJIRA NCHINI WIZARA YA KAZI NA AJIRA TAARIFA KWA UMMA ORODHA YA MAKAMPUNI YALIYOIDHINISHWA NA SERIKALI KUENDESHA HUDUMA ZA WAKALA BINAFSI WA AJIRA NCHINI 1. Tarehe 27/1/2014, Mhe. Waziri wa Kazi na Ajira, Bibi Gaudentia

More information

Lesson 34a: Environment

Lesson 34a: Environment bahari / bahari ziwa / maziwa kisiwa / visiwa pwani / pwani bara / bara mto / mito mlima / milima mbingu / mbingu mti / miti nyasi / nyasi ua / maua tawi / matawi jani / majani mchanga udongo msitu / misitu;

More information

GALIL. 1 Liter INSECTICIDE. An insecticide for the control of thrips, aphids and whitefly nymphs on roses

GALIL. 1 Liter INSECTICIDE. An insecticide for the control of thrips, aphids and whitefly nymphs on roses GALIL An insecticide for the control of thrips, aphids and whitefly nymphs on roses Sumu ya kuua wadudu aina ya thrips, aphids na whitefly nymphs kwenye maua aina ya rosa SCAN FOR WEBSITE FLAMMABLE LIQUID

More information

DEFERRED LIST ON 14/8/2018

DEFERRED LIST ON 14/8/2018 DEFERRED LIST ON 14/8/2018 SN WP.NO Employer Applicant name Decision made 1 WPD/8480/16 M/s. Light in Africa Children's Home Mrs. KYNN Kaziah Elliott Awasilishe Lost Report ya vyeti 2 WPC/3216/18 M/s.

More information

IN MEMORIAM JOHN FRANCIS MARCHMANT MIDDLETON

IN MEMORIAM JOHN FRANCIS MARCHMANT MIDDLETON SWAHILI FORUM 17 (2010): 3-8 IN MEMORIAM JOHN FRANCIS MARCHMANT MIDDLETON It was with immense sadness and sense of loss that the students, colleagues and friends of John Middleton received the news of

More information

LEARNING BY EAR The Promised Land - A Story of African Migration to Europe. EPISODE TEN: Two Faces of Migration

LEARNING BY EAR The Promised Land - A Story of African Migration to Europe. EPISODE TEN: Two Faces of Migration LEARNING BY EAR 2011 The Promised Land - A Story of African Migration to Europe EPISODE TEN: Two Faces of Migration AUTHOR: Chrispin Mwakideu EDITORS: Katrin Ogunsade, Klaus Dahmann PROOFREADER: Pendo

More information

4,834, , Dar es Salaam Safety Nets Chama cha Utafiti wa Magonjwa Sugu na UKIMWI kwa Tiba Asilia Tanzania,

4,834, , Dar es Salaam Safety Nets Chama cha Utafiti wa Magonjwa Sugu na UKIMWI kwa Tiba Asilia Tanzania, Page 1 of 3 4,177,913,520 disbursed for RSG, MG and RDG project in November 2006 Name of Organisation Thematic Areas Funding Applications Round 3, RSG September 2006 1 Campaign for Travellers Safety, P.O.

More information

When greeting someone older than you in Swahili, you say

When greeting someone older than you in Swahili, you say They call me Yame When greeting someone older than you in Swahili, you say shikamoo to show respect. Only 2.5 percent of Tanzania s population is over 65. In our village, that includes about 140 people.

More information

SOCIO ECONOMIC SURVEY 2013

SOCIO ECONOMIC SURVEY 2013 Zanzibar Official Statistics Provider Quick Figures 2013 GDP Growth Rate: 7.4 per cent GDP per Capita: TSH 1,077,000 Inflation Rate: 5.0 per cent Population : 1.3M Population Growth Rate : 2.8 SOCIO ECONOMIC

More information

MUSOMA MUNICIPAL COUNCIL. (All communication should be addressed to the Municipal Director)

MUSOMA MUNICIPAL COUNCIL. (All communication should be addressed to the Municipal Director) MUNICIPAL COUNCIL. (All communication should be addressed to the Municipal Director) Tel:No. 028-2622560/2622550 Fax No. 028-2620550 E-mail: md@musomamc.go.tz The Municipal Director's Office P.O. Box 194

More information

SOCIO ECONOMIC SURVEY 2012

SOCIO ECONOMIC SURVEY 2012 Zanzibar Official Statistics Provider Quick Figures 2012 GDP Growth Rate: 7.0 per cent GDP per Capita: TSH 1,003,000 Inflation: 9.4 per cent Population : 1.3M Population Growth Rate : 2.8 SOCIO ECONOMIC

More information

AMAZING HOW ADVANCE ZANZIBAR WAS: 1901 January

AMAZING HOW ADVANCE ZANZIBAR WAS: 1901 January AMAZING HOW ADVANCE ZANZIBAR WAS: 1901 January Tea: the first packet of tea made in East Africa was packed in Dunga. The leaves were the first products of the garden that was laid out there in 1899. It

More information

WORKSHOP ON COMPILATION OF INTERNATIONAL MERCHANDISE TRADE STATISTICTS ADDIS ABABA, 8-11 NOVEMBER, 2004 COUNTRY REPORT

WORKSHOP ON COMPILATION OF INTERNATIONAL MERCHANDISE TRADE STATISTICTS ADDIS ABABA, 8-11 NOVEMBER, 2004 COUNTRY REPORT WORKSHOP ON COMPILATION OF INTERNATIONAL MERCHANDISE TRADE STATISTICTS ADDIS ABABA, 8-11 NOVEMBER, 2004 COUNTRY REPORT BY: SALEH MZEE SALEH THE CHIEF GOVERNMENT STATISTICIAN (OCGS) ZANZIBAR- TANZANIA NOVEMBER,

More information

United Republic of Tanzania

United Republic of Tanzania KEY FACTS Joined Commonwealth: 1961 Population: 47,783,000 (2012) GDP p.c. growth: 2.2% p.a. 1990 2012 UN HDI 2012: world ranking 152 Official languages: Time: Currency: Geography Kiswahili, English GMT

More information

ZANZIBAR INVESTMENT GUIDE

ZANZIBAR INVESTMENT GUIDE ZANZIBAR INVESTMENT GUIDE 2018-2019 Executive Director P.O. Box: 2286, Zanzibar - Tanzania Tel: +255 24 2233026/ 2237353 Fax: +255 24 2232737 Email: zipa@zipa.co.tz info@zipa.co.tz Website: www.zanzibarinvest.org

More information

PARASTATAL'S REVENUES, EXPENDITURES, AND PROFIT AND LOSSES FOR THE YEAR ENDED 30 JUNE, 2014

PARASTATAL'S REVENUES, EXPENDITURES, AND PROFIT AND LOSSES FOR THE YEAR ENDED 30 JUNE, 2014 PARASTATAL'S REVENUES, EXPENDITURES, AND PROFIT AND LOSSES FOR THE YEAR ENDED 30 JUNE, 2014 S/NO NAME TOTAL NON PROFIT ORIENTED INSTITUTIONS WHICH RECEIVE S Agency for Development 1 Education Management

More information

3.0. OPENING STATEMENT BY H.E. JAKAYA MRISHO KIKWETE, PRESIDENT OF THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA.

3.0. OPENING STATEMENT BY H.E. JAKAYA MRISHO KIKWETE, PRESIDENT OF THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA. DRAFT PROCEEDINGS OF THE 6 TH INTERNATIONAL INVESTORS ROUND TABLE MEETING HELD ON 12 TH MARCH 2007 AT NGURDOTO MOUNTAIN LODGE, ARUSHA. 1.0. ATTENDANCE. attached list on page 168. 2.0. OPENING. 2.1. Mr.

More information

ZNCCIA Members Qualify to the GIZ Creating Perspectives Project.

ZNCCIA Members Qualify to the GIZ Creating Perspectives Project. 03: ZAYEE ZNCCIA Joins the World to Celebrate Entrepreneurship 04: Zanzibar Chamber signs an MOU with FEI 05: Mwanamke Chakarika: Bridging the Zanzibar Youth Unemployment Gap ZNCCIA Members Qualify to

More information

Land Planning Authorities and Sustainable Tourism Development in Zanzibar. Zanzibar s Profile

Land Planning Authorities and Sustainable Tourism Development in Zanzibar. Zanzibar s Profile Land Planning Authorities and Sustainable Tourism Development in Zanzibar Abdul-Nasser Hikmany (Zanzibar, Tanzania) Zanzibar s Profile Zanzibar consists of sister islands named Unguja and Pemba Has it

More information

NATIONAL OVERVIEW OF PROTECTED AREAS IN TANZANIA AND THEIR TOURISM POTETIALS

NATIONAL OVERVIEW OF PROTECTED AREAS IN TANZANIA AND THEIR TOURISM POTETIALS NATIONAL OVERVIEW OF PROTECTED AREAS IN TANZANIA AND THEIR TOURISM POTETIALS PRESENTED BY MR. ALLAN J.H. KIJAZI (DIRECTOR GENERAL- TANZANIA NATIONAL PARKS) BACKGROUND Tanzania has set aside 40.5% of her

More information

TANZANIA FOOD AND NUTRITION CENTRE

TANZANIA FOOD AND NUTRITION CENTRE TANZANIA FOOD AND NUTRITION CENTRE INVENTORY FOR NUTRITION INFORMATION EXCHANGE PARTNERS With Contact Addresses of Key Nutrition Information Exchange Partners in Tanzania 2007 BY: Sylvia Shao Charles Mamuya

More information

BUSINESS OPPORTUNITIES IN TANZANIA

BUSINESS OPPORTUNITIES IN TANZANIA BUSINESS OPPORTUNITIES IN TANZANIA FACT PACK June 2015 Business Sweden in Nairobi TANZANIA BRIEF FACTS BASIC FACTS Population: 49,639,138 (2014) Area: 947,300* sq. km Capital: Dar es Salaam Languages:

More information

The Rt. Honourabe Daniel Fred Kidega, Speaker of East African Legislative Assembly; The Chairperson and Council of East African Community Ministers;

The Rt. Honourabe Daniel Fred Kidega, Speaker of East African Legislative Assembly; The Chairperson and Council of East African Community Ministers; 1 SPEECH BY THE PRESIDENT OF ZANZIBAR AND CHAIRMAN OF THE REVOLUTIONAY COUNCIL; H. E. DR. ALI MOHAMED SHEIN AT THE COMMENCEMENT OF THE 2 ND MEETING OF THE 5 TH SESSION OF THE 3 RD ASSEMBLY- AT ZANZIBAR

More information

Honourable Dr. Mary Michael Nagu, MP Minister of State, (Investment and Empowerment)

Honourable Dr. Mary Michael Nagu, MP Minister of State, (Investment and Empowerment) REMARKS FOR H.E. DR. MOHAMED GHARIB BILAL, VICE PRESIDENT OF THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA, DURING TABORA REGIONAL INVESTMENT FORUM, 19 TH JULY, 2013 Honourable Dr. Mary Michael Nagu, MP Minister of

More information

Embassy of the United Republic of Tanzania

Embassy of the United Republic of Tanzania Statement on Sino-Tanzania Relations Embassy of the United Republic of Tanzania Beijing, China H.E. Benjamin W. Mkapa, former President of the United Republic of Tanzania described the relations between

More information

Tanzania's famous Olduvai Gorge has provided rich evidence of the world's pre history, including fossil remains of some of man's earliest ancestors.

Tanzania's famous Olduvai Gorge has provided rich evidence of the world's pre history, including fossil remains of some of man's earliest ancestors. Welcome to Tanzania "The beach perfectly matched my vision of paradise: fine white sand and vivid blue sea set against a lush palm forest. I never want to leave this magical place!" Tanzania has long been

More information

FIRST PAN-AFRICAN CONFERENCE ON: SUSTAINABLE TOURISM MANAGEMENT IN AFRICAN NATIONAL PARKS AND PROTECTED AREAS: CHALLENGES AND OPPORTUNITIES

FIRST PAN-AFRICAN CONFERENCE ON: SUSTAINABLE TOURISM MANAGEMENT IN AFRICAN NATIONAL PARKS AND PROTECTED AREAS: CHALLENGES AND OPPORTUNITIES Madrid, October 2012 FIRST PAN-AFRICAN CONFERENCE ON: SUSTAINABLE TOURISM MANAGEMENT IN AFRICAN NATIONAL PARKS AND PROTECTED AREAS: CHALLENGES AND OPPORTUNITIES Arusha, Tanzania, from 15 to 18 October

More information

Ministry of Natural Resources and Tourism Tourism Division. The 2009 Tourism Statistical Bulletin

Ministry of Natural Resources and Tourism Tourism Division. The 2009 Tourism Statistical Bulletin Ministry of Natural Resources and Tourism Tourism Division The 2009 Tourism Statistical Bulletin INTRODUCTION THE COUNTRY Tanzania covers 945,234 sq. km made up 942,832 sq. km of mainland Tanzania (formerly

More information

Premiere Era July.2017

Premiere Era July.2017 Premiere Era July.2017 Airport work expected to boost tourism Chinese finance and expertise is helping Zanzibar create greater capacity for flights. The Export-Import Bank of China is in the final stages

More information

FLY WITH US TO THE LAND OF KILIMANJARO, ZANZIBAR & THE SERENGETI

FLY WITH US TO THE LAND OF KILIMANJARO, ZANZIBAR & THE SERENGETI FLY WITH US TO THE LAND OF KILIMANJARO, ZANZIBAR & THE SERENGETI CLUB 2016 ABOUT US Proudly Tanzanian. Established in 2004. Holder of an Air service License and Air operators certificate granted by Tanzanian

More information

3rd International Forum on sustainable Tourism 20th to 22nd October 2008 Bamako - Mali

3rd International Forum on sustainable Tourism 20th to 22nd October 2008 Bamako - Mali TANZANIA S POLICY ON TOURISM DEVELOPMENT 3rd International Forum on sustainable Tourism 20th to 22nd October 2008 Bamako - Mali Ministry of Natural Resources and Tourism - Tanzania 1 Tanzania basic facts

More information

The United Republic of Tanzania Ministry of Natural Resources and Tourism TOURISM DIVISION The 2013 Tourism Statistical Bulletin

The United Republic of Tanzania Ministry of Natural Resources and Tourism TOURISM DIVISION The 2013 Tourism Statistical Bulletin The United Republic of Tanzania Ministry of Natural Resources and Tourism TOURISM DIVISION The 2013 Tourism Statistical Bulletin INTRODUCTION THE COUNTRY Tanzania covers 945,234 sq. km made up 942,832

More information

ZANZIBAR AIRPORTS AUTHORITY PROJECTS

ZANZIBAR AIRPORTS AUTHORITY PROJECTS ZANZIBAR AIRPORTS AUTHORITY PROJECTS ZANZIBAR AIRPORTS AUTHORITY INTRODUCTION Zanzibar is a part of United Republic of Tanzania It consists of two main Islands, Unguja and Pemba, and several other smaller

More information

GCRMN Number of sites regularly monitored

GCRMN Number of sites regularly monitored GCRMN Number of sites regularly monitored What is being Monitored Monitoring Partnerships Engagement in international efforts Outputs/reports Recent key findings Notable successes and challenges Presented

More information

Anderson, J.D. & Gates, P.D South Pacific Commission Fish Aggregating Device (FAD) Manual. Vol. 1. Planning FAD Programmes.

Anderson, J.D. & Gates, P.D South Pacific Commission Fish Aggregating Device (FAD) Manual. Vol. 1. Planning FAD Programmes. 6. APPENDIX 6.1 Bibliography Anderson, J.D. 1994. The interaction between artisanal and fish aggregation devices (FADs). Unpub. Final Report. FMSP Programme, ODA. MRAG Ltd., London. Anderson, J.D. & Gates,

More information

NATIONAL REPORT OF TANZANIA ON SEA LEVEL ACTIVITIES AND OBSERVING NETWORK

NATIONAL REPORT OF TANZANIA ON SEA LEVEL ACTIVITIES AND OBSERVING NETWORK NATIONAL REPORT OF TANZANIA ON SEA LEVEL ACTIVITIES AND OBSERVING NETWORK Mohammed Ngwali Tanzania Meteorological Agency, Zanzibar Office P. O. Box 340, Zanzibar, Tanzania. Tel: +255 24 2231958; Fax: +

More information

OPENING REMARKS BY HIS EXCELLENCY JAKAYA MRISHO KIKWETE, PRESIDENT OF THE UNITED REPUBLIC. President of Zanzibar and Chairman of the Zanzibar

OPENING REMARKS BY HIS EXCELLENCY JAKAYA MRISHO KIKWETE, PRESIDENT OF THE UNITED REPUBLIC. President of Zanzibar and Chairman of the Zanzibar OPENING REMARKS BY HIS EXCELLENCY JAKAYA MRISHO KIKWETE, PRESIDENT OF THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA AT THE 6 TH INTERNATIONAL INVESTORS ROUND- TABLE FOR TANZANIA, NGURDOTO MOUNTAIN LODGE, ARUSHA, 12

More information

78% AREA 64 YEARS. in Climate. Capital NAIROBI. Literacy. Population: 46,790,758. Time Zone. Language. Economics $141.6 BILLION 580,367 KM 2

78% AREA 64 YEARS. in Climate. Capital NAIROBI. Literacy. Population: 46,790,758. Time Zone. Language. Economics $141.6 BILLION 580,367 KM 2 2006 in 2006 THE 410 BRIDGE STARTED IT S WORK IN KENYA. Climate VARIES FROM TROPICAL ALONG COAST TO ARID IN INTERIOR Population: 46,790,758 (JULY 2016, WORLD FACTBOOK) Time Zone UTC +3 7-8 HOURS AHEAD

More information

OPENING REMARKS BY H.E

OPENING REMARKS BY H.E OPENING REMARKS BY H.E. JAKAYA MRISHO KIKWETE, PRESIDENT OF THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA AT THE PRESIDENTIAL ECONOMIC COMMISSION MEETING BETWEEN UNITED REPUBLIC OF TANZANIA AND THE REPUBLIC OF SOUTH

More information

UWANDAE EXPO 2019 EVENT CONCEPT

UWANDAE EXPO 2019 EVENT CONCEPT UWANDAE EXPO2019 EVENT CONCEPT UWANDAE EXPO 2019 EVENT CONCEPT TANZANIA S FIRST DOMESTIC TOURISM TRADE FAIR (INAUGURAL EVENT) 15th 17th FEBRUARY 2019 THE NATIONAL MUSEUM GROUNDS, DAR ES SALAAM PREPARED

More information

TANZANIA ATOMIC ENERGY COMMISSION LIST OF CENTRES UNDER CLOSURE AS AT 12TH OCTOBER 2018 ARUSHA

TANZANIA ATOMIC ENERGY COMMISSION LIST OF CENTRES UNDER CLOSURE AS AT 12TH OCTOBER 2018 ARUSHA TANZANIA ATOMIC ENERGY COMMISSION LIST OF CENTRES UNDER CLOSURE AS AT 12TH OCTOBER 2018 ARUSHA S/No. NAME OF CENTRE 1. MONG OLA HEALTH CENTRE P.O. BOX 12150, ARUSHA. 2. KANSAY HEALTH CENTRE P.O. BOX 200,

More information

MSI Self Assessment NAVAREA VII. Submitted by: South Africa SUMMARY

MSI Self Assessment NAVAREA VII. Submitted by: South Africa SUMMARY MSI Self Assessment NAVAREA VII 1 SAIHC10-5.2 Submitted by: South Africa SUMMARY 1. Background. The Coordinator of NAVAREA VII, in conjunction with the South African Meteorological Service, promulgates

More information

THE TANZANIAN SEA LEVEL NETWORK: A NATIONAL REPORT (DRAFT)

THE TANZANIAN SEA LEVEL NETWORK: A NATIONAL REPORT (DRAFT) THE TANZANIAN SEA LEVEL NETWORK: A NATIONAL REPORT (DRAFT) Shigalla B. Mahongo Tanzania Fisheries Research Institute P.O. Box 9750, Dar es Salaam, Tanzania [Tel: +255 51 650045; Fax: +255 51 650043; Email:

More information

ZANZIBAR YEARBOOK OF LAW VOLUME 5 VOLUME ZANZIBAR YEARBOOK OF LAW INTO PASSION TRANSFORM JUSTICE

ZANZIBAR YEARBOOK OF LAW VOLUME 5 VOLUME ZANZIBAR YEARBOOK OF LAW INTO PASSION TRANSFORM JUSTICE ZANZIBAR YEARBOOK OF LAW VOLUME 5-2015 ZANZIBAR YEARBOOK OF LAW TRANSFORM JUSTICE VOLUME 5 2015 INTO PASSION The Anglican cathedral Christ Church (or Church of Christ) situated at Mkunazini in Stone Town

More information

Market Brief on Tanzania

Market Brief on Tanzania Market Brief on Tanzania January 2018 Location Facts and Figures Tanzania is located in the African Great Lakes region on the East coast of the continent. It is bordered by Kenya and Uganda to the north;

More information

AIRLIFT STRATEGY PRESENTATION TO INDUSTRY GROWTH & SAFETY CONFERENCE: DATE: NOVEMBER 2014

AIRLIFT STRATEGY PRESENTATION TO INDUSTRY GROWTH & SAFETY CONFERENCE: DATE: NOVEMBER 2014 AIRLIFT STRATEGY PRESENTATION TO INDUSTRY GROWTH & SAFETY CONFERENCE: DATE: 04-06 NOVEMBER 2014 Table of Contents Section 1 Section 2 Section 3 Section 4 INTRODUCTION & EXECUTIVE SUMMARY OBJECTIVES MANDATE

More information

See more:

See more: Tanzania - Best Business Opportunities, Identification and Selection of right Project, Thrust areas for Investment, Industry Startup and Entrepreneurship See more: http://goo.gl/xyryiv Introduction Tanzania

More information

Market Brief on Tanzania

Market Brief on Tanzania Market Brief on Tanzania February 2017 Location Facts and Figures Total Population 50,7 million (2015) Tanzania is located in the African Great Lakes region on the East coast of the continent. It is bordered

More information

Reporting and Supporting Coral Reef Sustainability In The Western Indian Ocean

Reporting and Supporting Coral Reef Sustainability In The Western Indian Ocean Reporting and Supporting Coral Reef Sustainability In The Western Indian Ocean Nairobi Convention Science-Policy workshop 8 July 2018 Durban, South Africa On the contributions of the Coral Reef Task Force/Coral

More information

Tanzania Banking on Results from its 1st Tourism Investment Forum by Jerry W. Bird

Tanzania Banking on Results from its 1st Tourism Investment Forum by Jerry W. Bird Tanzania Banking on Results from its 1st Tourism Investment Forum by Jerry W. Bird The Tanzania Tourism Investment Forum, hosted by the Honorable Zakia Hamdani Meghji, MP, Tanzania's Minister of Natural

More information

ZANZIBAR YEARBOOK OF LAW

ZANZIBAR YEARBOOK OF LAW ZANZIBAR YEARBOOK OF LAW ZANZIBAR YEARBOOK OF LAW VOLUME 3-2013 TRANSFORM JUSTICE INTO PASSION VOLUME 3 2013 i Transform Justice Into Passion ii Published by: ZANZIBAR LEGAL SERVICES CENTRE (ZLSC) House

More information

JABALI AFRICAN ACROBATS TEACHER'S NOTES

JABALI AFRICAN ACROBATS TEACHER'S NOTES JABALI AFRICAN ACROBATS TEACHER'S NOTES Brought to you by Class Act Performing Artists & Speakers; 800-808-0917 JABALI ACROBATS This incredible Kenyan troupe combines Chinese and African traditions of

More information

AN OVERVIEW OF TOURISM DEVELOPMENT IN THE SOUTHERN CIRCUIT

AN OVERVIEW OF TOURISM DEVELOPMENT IN THE SOUTHERN CIRCUIT DEVELOPMENT AND FUTURE OF TOURISM IN THE SOUTHERN CIRCUIT IN TANZANIA AN OVERVIEW OF TOURISM DEVELOPMENT IN THE SOUTHERN CIRCUIT Mr. S. A. Pamba Director of Tourism Ministry of Natural Resources and Tourism

More information

LOCAL NGOs. Tanzania Agriculture Capacity Building (TACAB) P.O BOX Cell: Tanzania Agricultural Development Trust (TADT)

LOCAL NGOs. Tanzania Agriculture Capacity Building (TACAB) P.O BOX Cell: Tanzania Agricultural Development Trust (TADT) LOCAL NGOs Tanzania Agriculture Capacity Building (TACAB) P.O BOX 12831 Cell: 0718809543 Tanzania Agricultural Development Trust (TADT) Uhuru Street, Mwalimu House, 3rd Floor, P.O Box 72833, Dar es Salaam

More information

Enging asia enaidura engerai oingat naji Namunyak Maajabu ya uhamaji wa mtoto wa nyumbu anayeitwa Bahati The Amazing Migration of Lucky the Wildebeest

Enging asia enaidura engerai oingat naji Namunyak Maajabu ya uhamaji wa mtoto wa nyumbu anayeitwa Bahati The Amazing Migration of Lucky the Wildebeest Enging asia enaidura engerai oingat naji Namunyak Maajabu ya uhamaji wa mtoto wa nyumbu anayeitwa Bahati The Amazing Migration of Lucky the Wildebeest An Adventure by Monica Bond and Derek Lee designed

More information

China Hi-Tech Fair Organizing Committee 1 June 2017

China Hi-Tech Fair Organizing Committee 1 June 2017 2017 China Hi-Tech Fair in Germany China Hi-Tech Fair Organizing Committee 1 June 2017 1. Brief on China Hi-Tech Fair Date: November 16-21 Frequency: Annually (initiated in 1999) Venue: Shenzhen Convention

More information

ZANZIBAR YEARBOOK OF LAW

ZANZIBAR YEARBOOK OF LAW ZANZIBAR YEARBOOK OF LAW VOLUME 4-2014 ZANZIBAR YEARBOOK OF LAW TRANSFORM JUSTICE INTO PASSION VOLUME 4 2014 Transform Justice Into Passion ii Published by: ZANZIBAR LEGAL SERVICES CENTRE (ZLSC) House

More information

The historic Stone Town with its narrow winding streets, vivid markets and colorful bazaars makes for an interesting cultural visit.

The historic Stone Town with its narrow winding streets, vivid markets and colorful bazaars makes for an interesting cultural visit. The Clove Island - Zanzibar Brief Description Situated in the Indian Ocean, 36 km off the coastline of mainland Tanzania lies Zanzibar. Zanzibar officially refers to the archipelago that includes Unguja

More information

MSI Self Assessment NAVAREA VII CPRNW VII Submitted by: South Africa

MSI Self Assessment NAVAREA VII CPRNW VII Submitted by: South Africa MSI Self Assessment NAVAREA VII CPRNW9-3.2.1-VII Submitted by: South Africa 1. Action Required: The Commissions attention is drawn to paragraph 11 below. 2. Background: The Co-coordinator of NAVAREA VII

More information

High Commission of India Dar es Salaam

High Commission of India Dar es Salaam High Commission of India Dar es Salaam No. Dar/Com/201/1/2011 07 March, 2011 Economic and Commercial Report for the month of February 2011 1. Gross Domestic Product: Tanzania s GDP growth for the year

More information

COMESA VACANCIES OFFICE OF THE SECRETARY GENERAL

COMESA VACANCIES OFFICE OF THE SECRETARY GENERAL COMESA VACANCIES OFFICE OF THE SECRETARY GENERAL VACANCY NOTICE I. EXECUTIVE SECRETARY OF COMESA CLEARING HOUSE II. DIRECTOR OF COMESA MONETARY INSTITUTE Background The Common Market for Eastern and Southern

More information

Attracting Investment in Tanzania s Tourism Sector: The Investor Outreach Program A Case Study in MIGA s 1 Investing in Development Series

Attracting Investment in Tanzania s Tourism Sector: The Investor Outreach Program A Case Study in MIGA s 1 Investing in Development Series Attracting Investment in Tanzania s Tourism Sector: The Investor Outreach Program A Case Study in MIGA s 1 Investing in Development Series Iain T. Christie Senior Research Associate, GWU 1. Multilateral

More information

African Initiative for Combating Desertification to Strengthen Resilience to Climate Change in the Sahel and Horn of Africa

African Initiative for Combating Desertification to Strengthen Resilience to Climate Change in the Sahel and Horn of Africa African Initiative for Combating Desertification to Strengthen Resilience to Climate Change in the Sahel and Horn of Africa Kenichi Shishido Deputy Director, Global Environment Department, JICA Shishido.Kenichi@jica.go.jp

More information

Where are the poor: Region and District Poverty Estimates for Tanzania, 2012

Where are the poor: Region and District Poverty Estimates for Tanzania, 2012 Where are the poor: Region and District Poverty Estimates for Tanzania, 2012 Blandina Kilama bkilama@repoa.or.tz SK Conference Room, Umoja House Building, Ground Floor 30 June 2016 Outline Overview Population,

More information

A BRIEF ON MY 100 DAYS IN OFFICE

A BRIEF ON MY 100 DAYS IN OFFICE A BRIEF ON MY 100 DAYS IN OFFICE 1 On the 25 th of November 2015, President Uhuru Kenyatta made a reshuffle of his cabinet and returned me to the Ministry of Tourism where I had previously and successfully

More information

Tanzanian Family Owned and Operated Safari Company

Tanzanian Family Owned and Operated Safari Company Tanzanian Family Owned and Operated Safari Company I wish to introduce Daigle Tours, a leading independent Safari Tour Operator based out of Dar es Salaam, Tanzania. We are legally licenced by the Goverment

More information

AFRICAN ANIMAL BINGO

AFRICAN ANIMAL BINGO AFRICAN ANIMAL BINGO Using the printables make 4 bingo cards and print 2 sets set of named animal cards. Laminate or cover with clear sticky backed plastic for durability How to play Game 1-Up to 4 players

More information

ABBREVIATIONS... ii MESSAGE FROM THE MINISTER FOR NATURAL RESOURCES AND TOURISM Investment opportunities in the National parks...

ABBREVIATIONS... ii MESSAGE FROM THE MINISTER FOR NATURAL RESOURCES AND TOURISM Investment opportunities in the National parks... ABBREVIATIONS ATIA - African Trade Insurance Agency BOT - Build, Operate and Transfers CEO - Chief Executive Officer DALP - Development Action License Procedures DBOFOT - Design, Build, Finance, Operate

More information

TABORA REGION MUNICIPAL DIRECTORS OFFICE TEL: /6088 P. O. BOX 174

TABORA REGION MUNICIPAL DIRECTORS OFFICE TEL: /6088 P. O. BOX 174 REGIONAL ADMINISTRATION AND LOCAL GOVERNMENT TABORA MUNICIPAL COUNCIL TABORA REGION MUNICIPAL DIRECTORS OFFICE TEL: 026 2604315/6088 P. O. BOX 174 FAX: 026-2604835 TABORA - TANZANIA INVESTMENT OPPORTUNITY

More information

THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA MERCHANT SHIPPING NOTICE MSN 1613

THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA MERCHANT SHIPPING NOTICE MSN 1613 THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA MERCHANT SHIPPING NOTICE MSN 1613 REVALIDATING A CERTFICATE OF COMPETENCY: NEW REQUIREMENTS FOR MASTERS AND OFFICERS This notice is hereby issued to all Ship Owners, Managers,

More information

DPG-W Field Trip - The Zanzibar Water Sector Jan

DPG-W Field Trip - The Zanzibar Water Sector Jan Produced by the DPG Water Secretariat DPG-W Field Trip - The Zanzibar Water Sector Jan 29 31 2007 Context of the field trip After the DPG-Water field trips in 2005 (Lake Victoria) and 2006 (Dar es Salaam),

More information

POSITIVE IMPACT AND SUSTAINABILITY

POSITIVE IMPACT AND SUSTAINABILITY ANNUAL REPORT 2015-2016 AFRICANSPIRIT GROUP LIMITED 25 At Asilia, one of our key goals is to have a positive impact on Africa s wild places, translating as benefi ts to the environment and local people

More information

INFRASTRUCTURE DEVELOPMENT IN TANZANIA

INFRASTRUCTURE DEVELOPMENT IN TANZANIA INFRASTRUCTURE DEVELOPMENT IN TANZANIA PROF JOSEPH MSAMBICHAKA MBEYA UNIVERSITY OF SCIENCE AND TECHNOLOGY 50 TH YEARS ERB ANNIVERSARY 5 TH TO 7 TH SEPTEMBER 2018 PRESENTATION LAYOUT 1. DEFINITION OF INFRASTRUCTURE

More information

Tanzania Coastal Management Partnership

Tanzania Coastal Management Partnership Tanzania Coastal Management Partnership Preliminary Assessment of Coastal M a n a g ement Initiatives in Zanzibar Farhat Mbarouk, Jeremiah Daffa, Tom Bayer and Siddharth Kamalia ICM Technical Group 2003

More information

Tanzania. Kenya. Uganda. Zanzibar

Tanzania. Kenya. Uganda. Zanzibar COMPANY PROFILE Tanzania Kenya Uganda Zanzibar COMPANY OVERVIEW... Welcome to Seven Wonders Safaris L.T.D based in Arusha Tanzania. We organize safaris holidays trips to Tanzania, Kenya, Uganda. The Company

More information

The 2016 International Visitors Exit Survey Report

The 2016 International Visitors Exit Survey Report The 2016 International Visitors Exit Survey Report a TANZANIA TOURISM SECTOR SURVEY THE 2016 INTERNATIONAL VISITORS EXIT SURVEY REPORT October 2017 i TABLE OF CONTENTS LIST OF TABLES... iv LIST OF CHARTS...

More information

A little bit about Zanzibar

A little bit about Zanzibar A little bit about Zanzibar April 1, 2014 Archana Shah, Associate Director Helene and Grant Wilson Center for Social Entrepreneurship Pace University, 163 William St, New York, NY 10038 +1-212-346-1326

More information

The Great Lakes Private Sector Investment Conference (PSIC) Kinshasa, DRC February 2016

The Great Lakes Private Sector Investment Conference (PSIC) Kinshasa, DRC February 2016 The Great Lakes Private Sector Investment Conference (PSIC) Kinshasa, DRC 24-25 February 2016 Brussels roadshow 26 November 2015 Trevor Williams Consultant Allan Mukungu Senior Economics Affairs Officer

More information

INFORMATION NOTE Dar es Salaam United Republic of Tanzania June 2011

INFORMATION NOTE Dar es Salaam United Republic of Tanzania June 2011 INFORMATION NOTE Dar es Salaam United Republic of Tanzania 20 23 June 2011 DATE AND PLACE The 2011 UN Public Service Forum on the theme of Transformative Leadership in Public Administration and Innovation

More information

Price list applicable to EAC passengers on flights operated from 1st April 2016 upto 31st March 2017 issued on 22 November 2016

Price list applicable to EAC passengers on flights operated from 1st April 2016 upto 31st March 2017 issued on 22 November 2016 Via West,,,, Pangani,,. and 1 Via West,,, 152 Via West,,,, Pangani Via West,, Via West,,,, Pangani,,, Pangani,,, West, Kiligolf :25, :45,, Pangani,, and West :15,, Pangani, :55 Via,. On inducement of 4

More information

5 DAY SAFARI SELOUS & ZANZIBAR

5 DAY SAFARI SELOUS & ZANZIBAR 5 DAY SAFARI SELOUS & ZANZIBAR HIGHLIGHTS You ll stay in luxury at the exclusive Selous Kinga Lodge strategically positioned on the banks of the awesome Rufiji River with abundant wildlife all around you

More information

Regional outlook Sub-Saharan Africa 24/11/2015. Share commodities in good exports. Share commodities in goods imports

Regional outlook Sub-Saharan Africa 24/11/2015. Share commodities in good exports. Share commodities in goods imports Table 1: Economic structure indicators Number of Inhabitants (m.) Size of the economy (in USD bn.) Size of the economy (% of world GDP) Share commodities in good exports Share commodities in goods imports

More information

At Ang'ata Camps & Safaris we only have one boss : The Guest

At Ang'ata Camps & Safaris we only have one boss : The Guest At Ang'ata Camps & Safaris we only have one boss : The Guest Since we opened our first Ang ata Camp in Ndutu in December 2011 we have come a long way. Our good reputation has grown rapidly in the local

More information

KENYAADVENTURE SAFARI ON THE WILD SIDE. Want to Test Your Limits?

KENYAADVENTURE SAFARI ON THE WILD SIDE. Want to Test Your Limits? KENYAADVENTURE SAFARI Want to Test Your Limits? If you like to travel with a sense of adventure, then Kenya is the place for you. The dedicated thrill-seeker will find a world of challenges awaiting them.

More information

COUNTRY BRIEF SUB-SAHARAN AFRICA KEY FIGURES million $16.2 billion $1,200 (PURCHASING POWER PARITY) 52 years. Public Disclosure Authorized

COUNTRY BRIEF SUB-SAHARAN AFRICA KEY FIGURES million $16.2 billion $1,200 (PURCHASING POWER PARITY) 52 years. Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized SUB-SAHARAN AFRICA KEY FIGURES POPULATION GDP GNI PER CAPITA LIFE EXPECTANCY 40.4 million $16.2 billion $1,200 (PURCHASING POWER PARITY) 52 years 48601 Public Disclosure Authorized

More information